Dah,clemmy umenikumbusha mbali sana!kuna mdada wakati niko 1st yr chuo,tumefukuzwa mgomo nikakutana nae karibia na home. her perfume ndo ilini-strike sana,coz she was smelling devine. quick hug ananiambia bado tu unasoma jamani,utazeeka! i am married na 3 kids sasa! mwanaume wa mbuguni (unajua cha arusha tena,lol). mumewe akaja na kipikipiki chao tukaagana. aisee,nilimind kweli! sad enough 5 yrs later nikamuona,i had to stop na kumsalimia. amechoka mbaya! namuuliza mr hajambo? ananiambia jamaa alipata chombo kipya,akampiga chini. so yuko kwa wazazi na wanae 4,anatafuta cheti cha kufoji akasome secretarial!ilibidi nimyeyushe abt my whereabouts manake alianza maswali ya kitoto.
bt anyways,std 7 tulifaulu kama 15 hivi, wengine wali-dropout b4 form 4 bt mostly wengi wako kwenye maofisi mjini. nilifarijika sana at a desperate moment kwenye ofisi moja naitwa na mkaka,kumbe tulikuwa nae primary,he was one class behind me.akanisaidia chap chap. wengi tunakutana na kuwasiliana kwa kweli,japo vidole havilingani. wengine ni drug addicts (mwingine unamuwaza hivi wakati ule ananitokea ningeingia line sijui ningeishia kuwa addict mwenzie ama ningemsaidia asiwe kumbaf?)
Kweli yeye ni Ebenezer, hata sasa Mungu bado ananisaidia