Jamani naombeni ushauri.
Nilipanga nyumba self, doubleroom, miezi 6 kwa ths 80,000 kila mwezi, mwenye nyumba alisema baada ya wiki 2 umeme na maji vitakuwa vimeingia...hivyo sikuona shaka. Sasa mwezi umeisha na majibu yake ni yale yale tu kwamba ooh nimeshalipia tanesco blah blah blah. Na mimi kazi yangu inategemea umeme 100%, nimepoteza dili kibao mpaka sasa.
Kuna jinsi yoyote sheria inaweza nisaidia? ingawa hatukuandikishana kwenye kikaratasi kuhusu hayo mambo mawili (ujio wa maji na umeme) lakini watu walisikia na nina mashahidi. Maana siwezi kuendelea tena. Nianzie wapi? Itanigharimu vipi?
Asanteni.