Nimfanyeje mtu huyu afunguke akili?

Nimfanyeje mtu huyu afunguke akili?

Vituka

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2011
Posts
2,266
Reaction score
1,264
Rafiki yangu ni mlemavu wa viungo. Kuna kipindi alikuwa vibaya kiuchumi, and that time wadada wengi walikuwa wanamkataa alipowatongoza. Mungu mkubwa akatokea mdada ambae alimpenda sana pamoja na kuwa mlemavu na hana hali nzuri kifedha. Pitapita mdada kapata mimba na wakati ana mimba jamaa mazali ya pesa yakamuuangukia. Kifupi life ikabadilika. Yule dada alikuwa wa kawaida sana (sio mrembo sanaaa au dada du) na elimu yanke ni form four ila ni mdada wa heshima.

Sasa ivi jamaa kifedha yuko poa, mademu kitaa wote wanamtaka, sasa yeye anadai yule dada sio chaguo lake (alozaa nae), kampata ambae ni chaguo lake. Hataki kuishi na yule mdada na mtoto tena, na kapata dada du mmoja tena msomi (ana Masters) na ni mzuri sana kwa kweli kiasi kwamba ye mwenyewe hana amani kabisa. Bro wangu kasoma na uyo demu, anasema bonge la kicheche.

Kwa mtazamo wangu nilimshauri asiachane na yule alozaa nae coz nadhani ndo mwenye mapenzi ya dhati kwake. Yeye anadai sio chaguo lake na ana imani anaweza kupata mke mwingine msomi (kama aliyenae) na wakaishi happily. Nifanyaje nimnusuru jamaa na ili zigo analotaka kulibeba?
 
Du Jamaa yako mwache tu aende asije kujuta au nayeye ana tabia kama za Amyner? Huyo demu aliyempenda mwanzo wkt hana kitu ndio wa kua nae karibu sana aachane huyo wa masters anataka fedha tu huyooo!
 
Huyo jamaa (mlemavu) ni **** na asiyetumia akili kufikri alikotoka.Pesa ni maua muda wowote yananyauka,mwambie akumbuke alikotoka na ikiwezekana mkutanishe na bro wako apate ukweli kuhusu huyo dada anayempenda now.
 
Msichana mpaka kufika Masters kashaona direction ya maisha yake inaelekea wapi!ukicheche wake nahisi upo damuni,lakini hamfati huyo bro.wako kwa ajili ya pesa,anamengine huyo.Pesa anazo,sema ukicheche upo damuni.

Atulie na huyo mama watoto wake wa form four.
 
Huna haja ya kumstua. Atastuka baada ya kumkuta yatakayomkuta. Balaa litaanza mama atakapotaka uhuru wake kufaidi elimu yake wakati jamaa akijishuku kuliwa vyake kutokana na hali yake. Kimsingi huyo jamaa yako hana maana na amini kuna siku atalipwa kiasi cha kutoamini macho yake. Hakuna kitu kibaya kama wizi wa fadhili. Analitafuta la kulitafuta na haraka atalipata piga ua. Mara zote limbukeni akizidaka lazima aingizwe mjini ili alie baadaye.
 
Kama haelewi mwache, kwani atakuja kulazimika kuelewa.
Asifyeke kitasa alichojikinga mvua baada ya jua kuwaka na mvua kukatika.
 
Subiri yamkute ndiyo atatia akili............................!
 
Muambie aoe hiyo masters banaa! Kwanza ana hela, mwanamke wa form four hamfai manake kazoea shida. Sio wa hadhi yake na hajui ku-spend. Afu akipata wa phd achangamkie tenda.
If there were no women, what will do with all the useless money they earn? I always wonder!
 
yah wengio ndivyo walivyo, eti akipata hela sio chaguo lake weye uliyekuwa nae kipindi cha ukata..... inauma haswaa!
na ni mlemavu wa aje lakin?? nways ngoja yamkuta afunzwe na dunia atakoma ni limbukeni wa mapenzii huyoo hajayajua fresh ss ngoja yampe darasa atulie.
 
mwambie asidharau dafu , embe ni tunda la msimu ...

amepata mwanamke wa matumizi mwache atumie ila asije lalamika baadae
 
Kwa mtazamo wangu nilimshauri asiachane na yule alozaa nae coz nadhani ndo mwenye mapenzi ya dhati kwake. Yeye anadai sio chaguo lake na ana imani anaweza kupata mke mwingine msomi (kama aliyenae) na wakaishi happily. Nifanyaje nimnusuru jamaa na ili zigo analotaka kulibeba?

mtoto akililia wembe mpe ajikate mwenyewe....................baadaye yakimfika atajifunza ya kuwa kitunze kikutunze........
 
Sometimes nasema simba akikosa nyama hata majani atakula,..Jamaa kala majani anakuja kupata nyama kumbe ni kibudu mara mia angebaki kula majani.,ajui ila atakapo jua atajuta sana,la muhimu mwanamke aliye mzalisha apiganie haki zake kisheria juu ya mtoto na atulie na maisha yake wala asiangaike na huyo tamaambele.Ipo siku atakuja kuona umuhimu wake.
 
Sometimes nasema simba akikosa nyama hata majani atakula,..Jamaa kala majani anakuja kupata nyama kumbe ni kibudu mara mia angebaki kula majani.,ajui ila atakapo jua atajuta sana,la muhimu mwanamke aliye mzalisha apiganie haki zake kisheria juu ya mtoto na atulie na maisha yake wala asiangaike na huyo tamaambele.Ipo siku atakuja kuona umuhimu wake.

Demu alozaa nae anamdharau sana. kuna siku alikuja kwangu uyo demu akanambia rafiki yako kanambia niende kokote coz chaguo lake anakuja home so hataki matatizo tena akamwambia aende na mtoto coz hataki uyo mwenye mastaz akasirike! Ni kwa vile jamaa ni mlemavu tu ila angekuwa mzima ningemtwanga mangumi. Dem kakaa kwetu hadi saa 3 usiku ndo anampigia simu arudi eti mastaz kaondoka, lol!
 
yah wengio ndivyo walivyo, eti akipata hela sio chaguo lake weye uliyekuwa nae kipindi cha ukata..... inauma haswaa!
na ni mlemavu wa aje lakin?? nways ngoja yamkuta afunzwe na dunia atakoma ni limbukeni wa mapenzii huyoo hajayajua fresh ss ngoja yampe darasa atulie.

Miguu imepooza na nimifupi so anatembelea magongo!
 
Rafiki yangu ni mlemavu wa viungo. Kuna kipindi alikuwa vibaya kiuchumi, and that time wadada wengi walikuwa wanamkataa alipowatongoza. Mungu mkubwa akatokea mdada ambae alimpenda sana pamoja na kuwa mlemavu na hana hali nzuri kifedha. Pitapita mdada kapata mimba na wakati ana mimba jamaa mazali ya pesa yakamuuangukia. Kifupi life ikabadilika. Yule dada alikuwa wa kawaida sana (sio mrembo sanaaa au dada du) na elimu yanke ni form four ila ni mdada wa heshima.

Sasa ivi jamaa kifedha yuko poa, mademu kitaa wote wanamtaka, sasa yeye anadai yule dada sio chaguo lake (alozaa nae), kampata ambae ni chaguo lake. Hataki kuishi na yule mdada na mtoto tena, na kapata dada du mmoja tena msomi (ana Masters) na ni mzuri sana kwa kweli kiasi kwamba ye mwenyewe hana amani kabisa. Bro wangu kasoma na uyo demu, anasema bonge la kicheche.

Kwa mtazamo wangu nilimshauri asiachane na yule alozaa nae coz nadhani ndo mwenye mapenzi ya dhati kwake. Yeye anadai sio chaguo lake na ana imani anaweza kupata mke mwingine msomi (kama aliyenae) na wakaishi happily. Nifanyaje nimnusuru jamaa na ili zigo analotaka kulibeba?

huyo majuto yanamtafuta...
 
Demu alozaa nae anamdharau sana. kuna siku alikuja kwangu uyo demu akanambia rafiki yako kanambia niende kokote coz chaguo lake anakuja home so hataki matatizo tena akamwambia aende na mtoto coz hataki uyo mwenye mastaz akasirike! Ni kwa vile jamaa ni mlemavu tu ila angekuwa mzima ningemtwanga mangumi. Dem kakaa kwetu hadi saa 3 usiku ndo anampigia simu arudi eti mastaz kaondoka, lol!

jamaaaani,huyo rafiki yako mbona kama na utu wake umelemaa?yaani anamtenda hivi mdada wa wenyewe kweli?malipo yake hayatakawia na hatayasahau.
 
jamaaaani,huyo rafiki yako mbona kama na utu wake umelemaa?yaani anamtenda hivi mdada wa wenyewe kweli?malipo yake hayatakawia na hatayasahau.


Eti alisali sana ndo akaoneshwa mke mwema, mastaz girl! Kiukweli walemavu wengi niliowaona wameona au kuolewa na walemavu wenzao. Wachache sana wameoa au kuolewa na wasio walemavu (ye mwenyewe analifahamu hilo) ila jamaa anadai its impossible ye mlemavu na God ampe mke mlemavu. I told him mbona God keshakupa uyo ambae sio mlemavu na keshakuzalia mtoto kabisaa!Anadai sio chaguo lake.

Mie ntasitisha zoezi la kumshauri, mana siku zinavyoenda jamaa anazidi kunchukia asije nifikiria namtaka mastaz wake buree!
 
Ipo njia ya mtu ionekanayo njema machoni pake mwenyewe, lakini mbele ni njiaya mauti.
 
Back
Top Bottom