Nina $ 23,000 ila sijui biashara gani inanifaa

Mkuu hiyo hela inatosha sana kufanya miradi mbalimbali. Ila ushauri wangu kwako ni usimamizi.

Chagua mradi ambao ni rahisi kuusimamia, biashara nyingi zinapata tabu kutokana usimamizi ambao sio mzuri.
 
Hiyo pesa unao uwezo wa kui triple ndani ya mwaka. Ziko biashara za non perishable tangiable products ambazo zina guarantee ya kuuza inapofika season yake na supply inakuwa hai satisfy demand miaka yote.
Ni zipi hizo mkuu?
 
Nimepitia uzi wote.
Mawazo yaliyotolewa mengi ni mazuri, japo mengine hayana uhalisia.
Kila biashara hata mlizoziona hazifai zina matajiri wake au watu wanaozifanya kwa mafanikio.
Hivyo, unaweza kufanikiwa katika biashara yeyote endapo;
1. Unaipenda na una nia na aina hiyo ya biashara (Penye nia, pana njia)
2. Una uelewa wa kutosha kuhusu biashara hiyo (ukimuona mhindi chuo, ujue anasomea fani fulani eg udaktari, bima, etc ili baada ya hapo ajiajiri)
3. Una uwezo wa kifedha kumudu biashara husika (usiwe na 50M ukafanya biashara ya 5M, utazipoteza hata hizo zilizobaki. Ni kheri uwe na 50M then uungane na ndugu yako mfanye biashara ya 100M)
4. Kuna fursa katika biashara husika (kila hali ni fursa kwa mjasiriamali)
5. Kuna mfumo wa usimamizi (mfumo ambao unaumudu ie kuisimamia mwenyewe au kuweka taratibu za uendeshaji)
Nawatikia kila kheri wote wenye kujituma na nia ya mafanikio.
Penye nia pana njia
 
Mmeruka ruka weeeeee ila mmedharau kuweka mazao store .......

Haijwahi kutokeo mchele na maharage yakawekwa store na bei isipande,never.

Nakupa mfano hai Mbeya sehemu inaitwa mbalizi nilinunua debe la maharage kibrangeti kwa sh.18,000/- grade one kwa sh 18000+2000 ya kiroba+dawa+store debe Ni 20000/- mwezi wa tatu trh 15 mwaka Jana.Maharage ya Tshs.7,000,000/- debe 350.Mwezi wa tano trh 15 nikauzA haraka sana maana mwezi wa sita Kuna maharage ya mwezi wa sita.Bei niliyouza Ni 25,000/- nikapata 8,750,000/-ndani ya miezi miwili.Minimum risk,no tax.

Mwezi wa sita mwaka Jana,nikanunua ya 8,500,000 kwa 18000/- debe+kiroba+dawa+store jumla 20000/-debe.Nikauza mwezi wa 11 kwa debe 33,000/-.

kumbuka Nauza yote kwa jumla, nikapata milioni 14+.huu Ni mwaka Jana ....

Mchele sijaongelea Bado..

Achana na mahindi. Huna stress yeyote ile unaenjoy maisha tu
 
Ni pesa nyingi sana hyo mkuu kwa biashara walizoshaur hapo juu waweza igawa hata mara tatu kwa biashara tofauti na ukatoboa, ubia na watu makini ni muhimu wakati mwingne, Tchao, Muuza Nyanya
 
Mbalizi sehemu gani mkuu..na mchele je mbeya ikoje
 
Viwanja ni pesa ngp?? huko!
 
Mkuu samahani US $ 1 ni sawa na shilingi ngapi ya kibongo...?
 
Fanya Biashara inayotrend sasa hivi mjini na vijijini ya Kutengeneza Mifuko mbadala.Imagine una kakiwanda chako kidogo cha mashine za kichina na kuzalisha halafu unasuply nchi nzima.Ukitaka kufanikiwa fanya hii ukitaka kupoteza muda endelea kusoma ideas.Ukipendezwa na hii nicheki tuyajenge.(Machine,Materials na Strategies).
 

Nimekuelewa sana mkuu! Nitakutafuta Inshaalah!
 
Mkuu kwanza nikupe hongera kwa kuweza kupata kiasi hicho cha pesa kama walivyosema wakuu wengine ni nyingi lakin pia ni kidogo.Mim nashindwa kukushauri vizuri kwa sababu sjajua uko wapi na unafanya nin lakin generally unaweza kuzingatia ushauri wa mkuu aliekuambia utafute eneo nnje ya mji ambako ujenzi unaendelea ufungue hardware.

Jambo la pili pia unaweza kuwekeza kwenye mazao( nafaka kwa ujumla kama alivyoshauri mdau mmoja hapo juu) ila zingatia pia ushauri wa mdau mmoja alosema pesa sio kikwazo pekee cha kufanikiwa kwenye biashara tafsiri yake ni kwamba utafute mentor ambaye atakupa elimu kwanza ya kile ulichochagua kukifanya.Binafsi naamini kwamba pesa ni hitaji la tatu kwenye biashara baada ya idea( good), timing ndo inafuata pesa.Mim wakati namfungulia mwenzangu biashara kariakoo alifanya kazi bure kwenye duka la mentor kwa miezi mitatu ndo baadae akafungua la kwake na anaendelea vizuri kwa kweli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…