Nina Dharura nahitaji mkopo 6M kwa dhamana ya Gari

Nenda Platimum Credit Ltd. Wapo Karibu na Airtle.HQ. Wanatoa mikopo ya namna hiyo. Kwanza wanaifanyia gari valuation kijua thamani yake. Valuer unamlipa kama sh. 50,000. Kisha gari linatakiwa liwe na bima comprehensive. Wanafunga tracking kwenye gari lako. Then unapata mkopo. Kwa mkopo.wa muda mfupi tiba inafikia asilimia 7 kwa mwezi. Na pesa unayoweza kupata ni nusu ya thamani ya gari kama ni aina ya Toyota na brands nyingine ni asilimia 30 ya thamani ya gari.

Hawacheleweshi ila hayo ndo masharti.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…