Nina eneo maeneo ya Mwenge DSM, nahitaji mjasiriamali tuwekeze!

Mgagao

Member
Joined
Sep 12, 2016
Posts
33
Reaction score
34
Changamoto inayonikabili mimi ni upungufu wa mtaji, na mtaji nilio nao mm ni Eneo zuri maeneo ya Mwenge DSM, nahitaji mtu ambae tutawekeza pamoja, Habari niliyoifikia mm ni ufugaji wa kuku wa nyama, kama tutatengeneza mabanda tunaweza kufuga kuku zaidi ya 1500, eneo lina ukubwa wa zaidi ya 400sq,
Kama kuna mtu ana wazo tofauti tunaloweza kupata faida pamoja basi tunaweza kujadili!
Mimi nina eneo ww una pesa basi tuwekeze pamoja, nahitaji mtu ambaye yupo serious, kama yupo nipm!
 
MGAGAO ilikuwa ni camp iliyohifadhi raia wa afrika kusini(wakimbizi)kipindi wanapigania uhuru wao kutoka kwa mkaburu,ipo Iringa,wilayani kilolo kama sikosei,na jamaa waliacha mbegu ya kutosha ya kizazi chao pale,wanapaita south ndogo,is that the real meaning of ur name mkuu?
 
Hapana mkuu nina original yake,
 
Tafuta mwekezaji uweke apartments,uwe na share ya 40%
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…