Nina hofu fulani kumhusu Joash Onyango

Albinoomweusi

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2016
Posts
3,433
Reaction score
8,585
Kila mtu ana maoni yake, yangu ni haya; Dirisha lililopita la usajili, lile kubwa na dogo, Simba walifanya sajili kwa utulivu wa hali ya juu sana. Walitulia na kuangalia mahitaji ya timu, ndiyo maana sura zao mpya zimelipa sana.

Kuanzia kwa Larry Bwalya, Bernard Morrison, Thadeo Lwanga na Chris Mugalu. Sidhani kuna hata mmoja ambaye, Simba wanajuta kumsajili.

Ukiniuliza mimi, usajili bora zaidi wa Simba katika dirisha lililopita, sitahitaji hata sekunde ya kufikiria, jibu langu litakuwa wazi na lililonyooka, 'JOASH ONYANGO'

Ni beki anayejua maana ya kulinda lango lake. Ni mtu ambaye jina lake unatakiwa ulitaje la kwanza kabisa unapoulizwa mfano wa 'STOPPER' mmoja wa uhakika.

Joash anakaba sakafuni, anacheza hewani tena uhakika sana. Achana na hilo, Onyango ni mwepesi sana wa kusoma madhaifu ya wenzake hivyo anasawazisha makosa yao kwa urahisi mno.

Jina la Chama, show za Bwalya na Miquissone, na magoli ya Mugalu na Kagere, yanafanya baadhi ya kazi za wachezaji wengine zionekane za kawaida, kama inavotokea kwa Onyango.

Nafikiri kati ya wachezaji watatu bora wa msimu wa Simba, jina lake linapaswa kutokea. Joash ni habari nyingine aisee. Kwa mabeki wa kati Ligi kuu Tanzania Bara Onyango anatokea dunia yake kabisa[emoji119]
.
[emoji871]@deo_mwanasoka
 
hana kasi man to man na mtu kama TK au Makarani hawezi kabana nao. Mipira anayocheza yote inamkuta ktk eneo alilopo hawezi kufukuza ndiyo maana anaokoa mipira mingi kwa tackoling koz anakuwa nyuma ya straiker mwenye kasi anawasaidia simba kwa kujua jinsi ya kujipposition tu...siku akicjheza na mtu style ya Mkarana au Ton wa Merreikh utaona zaidi uwezo wake....
 
Kasi ipi, wachezaji hawawez kulingana spidi hata sku moja mbona chama hana kasi lakin ana mchango mkubwa kwenye matokeo ya simba!?

Yeye anajua kukaa sehem sahihi ili iwe rahis kuokoa mipira ndo aman una sema mipira mingi inamkuta tuu.

Unaweza ona n kazi rahisi lkn jaribu kulunganisha makosa ya Simba msimu ulopita na huu, utofauti upo.
 
Mchambuzi umedadavua kwa ufanisi mkubwa sana,kwasasa hapa Bongo akuna stoper kama Onyango,hata Wawa tumempunguzia lawama kwasababu madhaifu yake yanafichwa na huyu kiumbe.
 
Mbona au merekh tushacheza nao
Huyo makarani si juzi kapigwa 5
 
NUSU MTU NUSU CHUMA.

Mchezaji bora kabisa kwangu ni Thadeo Lwanga.

Mtu anapiga pasi zote Acurecy dhidi ya AS Vita kwa Asilimia 100%
 
Al Merrikh ipi? Hawa tuliowapiga 4 au kuna wengine?
 
Muhimu anaokoa kwa usahihi haijalishi ni namna gani anaokoa.
 
Mbona kichwa cha habari hakina uhusiano na habari yenyewe kabisa ni mbingu na ardhi

Sent from my Nokia 3.2 using JamiiForums mobile app
 
Kwani hajacheza nao hao you need to some point give a credit to person when it deserves

Sent from my Nokia 3.2 using JamiiForums mobile app
 
DJ naomba utuweke wimbo wa SIMBA umeimbwa na dulamakabila
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…