Nina Mil 7, nataka kununua bajaji ama kirikuu, kipi ni kizuri kwa biashara?

Mkuu nunua carry ipeleke mkoa. Ikapige kazi vijijini. Carry mjini nyingi. Bajaj sikushauri... ila carry ongeza bajeti. Walau 7m
Asante sana mkuu ni kweli hilo ni zuri ila nikijiuliza mimi kikazi ni dar je kule kijijini nitaipeleka wapi? maana kwa wazazi sidhani kama nitapata return nitakayo maana hapo undugurazation utakuwepo katikati
lakini bajaji as ofisini kutoka saa 11 jion nitaweza kumfuatilia nitakaempa aendeshe lakini bado ugumu unakuja kwenye kumpata mwaminifu na ipi ninunue mpya au used? na wengi ninaowauliza waliopo hizi carrier wanadai ili uione pesa yako lazima uendeshe mwenyewe sasa hii duuh ni chagua moja kazi au uendeshe mwenyewe


na kwanini hunishauri bajaji mkuu natumai kuna kitu mkuu
 
kupanga ni kuchagua. Kama unataka uwe mtumwa wa boss basi endelea na kazi yako.

Lakini kama unatafuta uhuru wa kifedha basi kujiajiri ni suluhisho la kutoka utumwani.
 
Niliwahi kusimamia bajaj 5 za ndugu yangu. Yeye alikuwa busy.. mkuu aisee ni balaa. Pesa haionekani sound kibao. Yaani ujanja ujanja mwingi mara akwambie kazi ngumu yaani we acha tu. Mara iibiwe dereva auliwe yaani ilikuwa ni visanga kila siku. Kuhusu gari tafuta rafiki kijijini unayemuamini muandikishiane umkabidhi gari fanya ndugu zaKO wasijue. Mimi nakushauri suzuki carry.
 
kupanga ni kuchagua. Kama unataka uwe mtumwa wa boss basi endelea na kazi yako.

Lakini kama unatafuta uhuru wa kifedha basi kujiajiri ni suluhisho la kutoka utumwani.
Ni kweli mkuu mimi nimefanya biashara nikaingiza zaidi ya million nane matokeo yake ikayumba na nikala hasara na kilichoniokoa ni kazi bila hii ningekuwa nishaanguka kabisa kuisimamisha biashara hasa mwanzo ni ngumu sana ndio maana najiongeza na hapo inatakiwa niipate million 20 hii naamini itasaidiana na kazi na hiki nitakachokinunua kati ya bajaji na suzuki carry
hizi ni short term zinifikishe long term ambapo hiyo hata kuacha kazi nitakuwa huru KUACHA BILA KUIONA NJIA duuuuh

na hiki wafanyakazi wengi kinatusumbua HEBU NISHAURI NIKIWA KAZINI NA HICHO NIKIFANYE PIA nilizofikiria hizo mbili bajaji au suzuki katika kujiongeza ushauri wako muhimu
 
Asante sana mkuu nashukuru ngoja nianze kulifiria mimi nilikuwa naona uzito ingawa wazo la kijijini lilikuwa linakuja shida nani umpe? ingawa bado ugumu unanijia marafiki wa siku hizi hasa mlieachana zamani ndio itabidi umtafute

but asante noted mkuu
 
tirika kidogo hapa mkuu
 
duuuh huyu ndo wa kwenda kujifunza but nimepata kitu je bora ununue mpya au used
 
words! kirikuu sio,wakati mwingine ukubali kugawana faida 1/2 na dereva....
 
Kama upo dar nivizuri nikuelekeze biashara ambayo tutakuwa wabia maana nimeanzisha vifaa vya utendaji kazi nimekwama mtaji na hiyo biashara kwa walio wengi wanaidharau na kutokuijua wengi wanunuzi ni wachina pesa cash na bidhaa ipo ukiitaji njoo pm tuyajenge ila kwa nia nzuri sio kuniibia aidia yangu.
 
jaribu kuweka wazi mkuu huenda wengine tukavutiwa katika biashara usiogope kuibiwa wazo maana hakuna jipya hapa duniani ni kubeba na kuliboresha zaidi
kwahiyo punguza uoga wa kuibiwa weka wazi tushauriane
 
Tafuta mtu mwenye familia ndio ataweza kuisimamia bajaji yako.
Hawa masharobaro wasiokuwa na uchungu na maisha watakutia stress.
Mtu mwenye familia kidogo ataifanya km hiyo ni ajira inayotunza familiabyake.
Atakuwa na heshima
 
Tafuta mtu mwenye familia ndio ataweza kuisimamia bajaji yako.
Hawa masharobaro wasiokuwa na uchungu na maisha watakutia stress.
Mtu mwenye familia kidogo ataifanya km hiyo ni ajira inayotunza familiabyake.
Atakuwa na heshima
thanks mkuu nashukuru ila hilo jina Ibilisi duuuuuh
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…