Nina Milioni 45, msaada wanaJF

Naomba namba yako nikupigie tuongee ila sio kuwa nitakuomba Hela zako kaka. Nakupatia tu mawazo. Mana hata MIE Nilikuja kuomba mawazo humu afu nikajumlisha na ya kwangu ndo nikapata linalonifaa
Sawa ndugu
 
Biashara yoyote inalipa provided mtaji ni wa kutosha na usimamizi ni imara, hayo mengine ni nyongeza. Penda kufanya kile roho yako inapenda, hatuwezi kufanya wote kitu kimoja. Mfano mimi napenda sana niwekeze kwenye kilimo siku pesa na nafasi itakaporuhusu.

Kwa wewe mkuu nimekusoma unapenda biashara ya daladala. Ni biashara nzuri ukifuata misingi yake. Tafuta msimamizi mzuri tena awe ndugu wa karibu na mwaminifu. Huyu atasimamia mahesabu (mfano konda). Mfanye awe sehemu ya mapato mnayoyapata sio kumtumikisha tu. Pia wakati biashara inaendelea jifunze ABC za magari ili ujue vitu kama service, route zenye faida etc

Mwisho ukubali faida na hasara ni sehemu ya biashara yako, kuna siku mambo yatakua mazuri sana na kuna siku hayatakua sawa.
NB: Usinunue gari bovu, litakuliza ujutie. Usitegemee daladala yako 100%. Fanya biashara unayoipenda mkuu
 
Ndugu mimi ndo naanza sina uzoefu aise je nikimpa akalipigisha kazi likaaribika alafu yeye akalala mbele mda wa kushinda mahakamani ntautoa wapi ndugu
Nimejaribu kufuatilia namna unavyo respond kwenye baadhi ya comment za wanaokushauri nimegundua vitu vifuatavyo:-

1. Una uoga wa asili

2. Hauna uwezo wa kukabili changamoto

3. Umekulia mazingira ya wasomiwasomi wengi au

4. Umesoma sana

Nianze na namba 3 na 4, watu wengi waliokulia mazingira ya wasomi wasomi au waliosoma sana (hata degree ya kwanza ni kusoma sana pia) na mazingira hayo yakawa hayana hata mfanyabiashara au mjasiriamali tunakosa uzoefu wa kufanya kitu nje ya ajira.

Namba 1 na 2 vinaweza kuwa matokeo ya namba 3 na 4.

Mtu muoga anaogopa kuanza.
Mtu muoga anawaza hasara kwanza badala ya faida
Mtu muoga hataki usumbufu
Mtu muoga hataki kukosana na watu

Kwenye biashara hivyo vitu HAVIKWEPEKI!

Hakuna biashara isiyo na hasara
Hakuna biashara isiyo na changamoto
Hakuna biashara isiyo na usumbufu
Na biashara nyingi lazima kuna kutofautiana hata na mteja tu achilia mbali uliowaajiri

Ukishajihisi ni muoga wa kupoteza, muoga wa usumbufu, muoga wa kukosana na watu achana na biashara zinazohusisha watu kwasababu kwanza sio lazima kila mtu afanye biashara na wala si kila mmoja anaweza kufanya biashara

Ni kweli kabisa tunahitaji kuwa na kipato cha ziada ila kuna vitu havifanywi na kila mtu.

Ushauri wangu kwako

Kwasababu angalau mwenzetu unauwezo wa kupata mamilioni yote hayo, kuna uwekezaji ambao unaweza kufanya usio na usumbufu

Mimi huwa naamini uwekezaji ni tofauti kidogo na biashara japo vinashabihiana

Unaweza kufanya moja kati ya vifuatavyo:

1. Tafuta kampuni inayopata faida kanunue hisa huko

2. Tafuta eneo (sio lazima iwe dsm), jenga stoo (sijui ndo godown) ambapo wakulima watakuwa wanatunza mazao yao huko kwa kulipia ushuru

3. Nunua mashine ya kusaga na kukoboa weka kwenye hiyo stoo kupanua wigo wa mapato

Katika hivyo vitatu sio rahisi kuibiwa pesa kizembe, hazina stress, hazina purukushani wala hazikuhitaji kuwepo kila siku japo kwenye mashine hapo utahitajika kuweka ndugu yako au mtu unayemuamini atukuibia ila hatakuibia sana
 
Kama kweli umeamua kuingia kwenye biashara Watu wametoa mawazo mengi mazuri sana tu...yafanyie Kazi ondoa uoga kabisa.

Zaidi sana huu ni msimu wa mavuno ,mpunga,mahindi,maharange n.k..,binafis nakuomba ufanye biashara ya mpunga ndani ya miezi mitano hii,yaan sita hadi wa 11 utaweza Ku pata faida nusu au zaidi ya mtaji wako.(sio uanze na pesa zote hizo).. Anza hata na million 10 tu,zingine wekeza tena kwenye biashara zingine.

Biashara ya mpunga au mchele kwa miezi hii ,kuna uwezekano mzuri sana wa kupata faida,ingia porini nunua mpunga kwa bei rahisi nenda kakoboe mashineni uza mchele..zama tena porini.

Kama unaweza zaidi tunaweza kusaidiana kwa makubaliano ya kisheria tukafanya pamoja hiyo biashara kwa sababu nina ujuzi na uzoefu wa kutosha.

Tuwasiliane na pia angalia ushauri wangu na mawazo yangu ambayo nilishawahi kuandika humu...uone labda tunaweza kufanya kitu kwa pamoja.

Asante.
 
Umemwambia ukweli haswa...,ni yeye sasa kama kweli atakuwa serious afanye maamuzi sahihi.
Usiogope kufanya biashara
 
True.
 
Nakusahuri rudisha hizo pesa ulipozichukua, usitumie hata mia.
Unawezaje kuchukua mkopo hujui cha kufanya??

Vipi hiyo biashara ikibuma si utaugua kisukari bure hapa , usianze biashara na hela ya mkopo mzee ni hatari na nusu.

Mkopo ni wa kuendeleza biashara na siyo kuanza.
Narudia tena rudisha hizo hela ulipotoa, utakuja nishukuru baadae


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Fuga kuku wa nyama na mayai,kabla ya kuanza tafuta mtaalamu akupe ABCs za hiyo bizne$$.
 
Fuga kuku
WA nyama
Na kuku wa kienyeji..


Ila unaweza Jenga nyumba na ukauza ni sure bussines kipindi hujaiuza unapangisha
Koote huko nimezurula ila hili wazo ndo la kupumzika sasa.hapa ni uhakika hamna inzi.(big up anko kidevu)
 
Hapa elimu inahitajika kidogo Mkuu,...Watu wengi wanaofanya biashara wala hawafanyi au kukaa karibu na biashara zao muda wote.,,kwa hyo kwenda kazini,au kuwa bize kiasi ngani hakukufanyi uogope kufanya biashara.

Tafuta watu sahihi,wafanye biashara sahihi kwa wakati sahihi... Jitahidi tuwasiliane tushauriane.
 
Hiyo biashara ya bajaji njoo uifanyie Dodoma..
 
@kisumapai
Nimesoma kwa utulivu ulichokiandika na nimeona haya
1. Katika siku 30, Mshahara wako na mwenza wako unatosha kwa siku kadhaa (tarehe 14 huwa hamna fedha za kutosha).
2. Hamna uzoefu wa biashara.
3. Umesha shauriana na mwenza wako aina za biashara.
Kwa mtazamo wangu fedha igawanye katika namna hii;
1. Biashara A. Hii iwe biashara ambayo itakupatia pesa ya kusaidia kuwezesha matumizi ya familia yako ya kila siku. Hii biashara iwe na uwezo wa kuingiza pesa ambayo ukiichukua haiwezi kuathiri biashara yenyewe.
2. Biashara B. Hii iwe biashara inayoingiza pesa itakayokuwa inahifadhiwa kama kukuza mtaji wenu wa biashara. Hii biashara iwe na uwezo wa kuingiza pesa kwa mwezi angalau faida ya asilimia 30% ya mtaji ulio wekewa (baada ya kutoa garama zote).
3. Biashara C. Hii iwe biashara ambayo itaweza kuingiza faida ya angalau 50% ya mtaji kwa kipindi cha kuanzia miezi mitano hadi nane au mwaka na iwe biashara ambayo unaweza kurudisha faida uliopata na kuongeza kama mtaji na kuipanua biashara hiyo.
Sasa aina gani ya biashara itakua ni biashara A, B na C inategemeana na vitu hivi;
1. Eneo unaloishi au utakalo amua kufanyia biashara
2. Muda utakao kuwa katika usimamizi na uangalizi wa biashara
3. Ujuzi juu ya usimamizi wa biashara ama kuwepo mtu wa kuweza kuangalia taarifa za biashara yako na kuweza kujua mwelekeo wake na kuweza kukushauri nini cha kufanya (iwapo mwelekeo hasi unatokea)
4. Utayari wa kupoteza mtaji (aidha kiasi ama wote).

Biashara inamengi huwezi kuwekeza leo kesho upate faida zingatia hilo na pili kuna tofauti ya mauzo (au pato kutoka kwenye biashara) na faida ya biashara.
 
Nimesoma kwa makini post yako lakini hujanishauri nifanye kipi na kipi niache ndugu

Wekeza kwenye Carwash ya kisasa.

Tafuta Location
Mikocheni warioba, Sinza Bamaga, Sinza Palestina, Kinonondoni Morroco-Mkwajuni, Sayansi.

Kwanini CARWASH
1)Sustainable; Siku zinavyoenda ndivyo Soko linapanuka ratio ya ununuzi wa vyombo vya usafiri uko speed miaka inavyosonga, uwezi funga kisa hakuna soko.

2)Managable, usimamizi ni ndogo sana unahitajika na hakuna mahesabu mengi.

3)Risk, biashara ina Assert zinazoeleweka alishindwa biashara unaiwezo wa kuuza na kurudisha pesa chapu.

Fanya uwekezaji mkubwa sana kulingana na ratio za Mtaji wa biashara husika, Design, Muonekano, Location...hata ukiwa unapata faida ndogo kwasasa miaka inavyozidi kwenda gari zinaongezeka soko lake lakueleweka.


Daladala & Bodaboda unamuda kadhaa wa kuchekelea na muda mwingi wa kulia baadae.

Kama huna muda wa kufatilia najiri mimi kutafuta Location, wataalamu wa ku-design mpaka inaanza kazi | utanilipa.
 
Yaan ni yeye tu ,ushauri mzuri kila mahali,...kama kweli ataamua kuufanyia Kazi atafaidika.
 
Bodaboda mpya ni kuanzia 2.2-2.5 kama sijakosea sana, wengi wamelia na hii biashara(sio wote

Nataka nikupe mbadala wa biashara hii, ni idea tu wala sijawahi kuifanya

Tafuta wamama ambao wako tayari kufanya biashara ya mama ntilie(idadi utajua mwenyewe, hata wakiwa 100 ni wewe tu na visenti vyako vya mkopo)kila mmoja mnunulie vifaa vyote anavyotaka kwa biashara hiyo(vijiko, sahani n.k) najua vifaa vyote havitofika 2.2 kwa mmoja mmoja(bei ya boda moja)

Kila mmoja mwambie akuletee hesabu(mtaelewana wenyewe sh ngapi) ila haitopishana sana na hesabu ya boda boda

Nb. Faida ya hiyo biashara hata siku ukizinguana na mama chanja una uhakika wa sehemu za kwenda kula.
 
Mzidi kuajiriwa tu 9am-5pm...
Kama ni kweli, nyie siyo wajasiriamali...haiingii akilini, vichwa viwili mume na mke mchukue mkopo halafu kama mazuzu hamjui nini mnataka kufanya..
Mzitoe hizo hela benki mlale nazo kitandani!

Everyday is Saturday.......................... 😎
 
1.Weka mashine ya kusaga nafaka Kama mahindi uwe unafanya packaging na kuuza kwa jumla au rejareja... Kwa kipindi hiki biashara yenye moderate risk ni biashara inayohusisha kula ...


2. Fungua duka la spaire za gari hizi ndogo ndogo Kama vitz, spacio au IST. Unaweza kuanza hata na million 25. Hii biashara inalipa Sana ndugu yangu. Fanya research yako kuhusu hili.


3. Tafuta eneo ufunguo carwash



Hayo ni mawazo yangu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…