Nina mpango mkubwa wa kuanzisha studio ya muzuki wa Injili na online television

5997

JF-Expert Member
Joined
Jan 19, 2019
Posts
513
Reaction score
1,205
Habari

Rejea mada tajwa hapo juu nafahamu humu jf tupo watu Wa fani mbalimbali hivyo ndio maana nimeleta mada hii nikijua nitapata majibu kwenu

Nina mpango mkubwa Wa kuanzisha studio ya muzuki wa injili na online television
Naombeni msaada wenu kwa yeyote anaejua bei za vitu hivi inacost shilingi ngapi naomba anisaidie kunifahamisha

(I) Sound proof
(II) camera zenye uwezo Wa kirekodi video
(IIII) Piano

Vile vile kwa wenye uzoefu naombeni mnisaidie ni vitu gani na gani napaswa kuna navyo ili niweze kukamilisha mpango wangu na ndoto zangu hizo za siku nyingi

Nitashukuru kwa maoni yenu
 
I. Sound proof inategemea kuna special na za magodoro. Ukipata fundi sofa mzuri anaweza akatengeneza nzuri,

Zile za duka zinauzwa kwa Squire feet. Check ebay zipo kibao

II. Camera, zipo kama unataka za video Tafuta DSLR Canon Camera Kwa used andaa Budget kuanzia 2.5 Milion.

III. Piano/ Kinanda inategemea unataka cha Kazi gani. Kutengeneza musiki au kufanya live performance.

Kama ni kutengeneza Music tafuta Yamaha kuanzia PsR s.710 hadi 950 budget andaa 2Milion hadi 4m

Kama ni live performance tafuta Yamaha Motif Seriea, Korg Triton au Kurzweil Hutajutia
 
Asante sana sound proof kumbe hata mafundi sofa wanatengeneza?
 
Bila shida mkuu tafuta Idea mpelekee
Je, mkuu mbali na sound proof, piano , camera, computers na mic

Je, kuna vitu vingine vikubwa navyopaswa kuna navyo ili kukamilisha studio ya online television?
 
Je, mkuu mbali na sound proof, piano , camera, computers na mic

Je, kuna vitu vingine vikubwa navyopaswa kuna navyo ili kukamilisha studio ya online television?
Sijajua kama utakuwa unatumia You tube
Au kama utakuwa na Website yako kwa ajili ya kufanya streaming
 
Nina idea za vipindi vya channels za gospel mpaka nmechoka kuandika sasa, mkuu studio ikiwa tayari usinisahau kwenye ufalme wako ntafutahi kufanya patnership na wewe!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante sana sound proof kumbe hata mafundi sofa wanatengeneza?
Kuna tofauti kati ya soundproofing na acoustic treatment. Sound proofing ni kuzuia sauti ya ndani isitoke nje na ya nje isiingie ndani, acoustic treatment ni kuzuia reflection ya sauti ndani ya studio. Mara nyingi watu huwa wanachanganya sana na hii inapelekea mixing nyingi kuwa chini ya kiwango
 
Nikupongeze mkuu kwa kuwa na wazo hilo zuri. Binafsi ningependa kutoa maoni/ushauri hususani kwenye studio kwa kuwa nina uzoefu nayo na nmefanikiwa kuwa na studio pia. Kwanza kabisa uwekezaji wako mkubwa utumike kwenye vipaumbele vifuatavyo
1. Watu watakaohusika kuoperate studio( maana studio nyingi zimekufa kutokana na watu kukosa weledi au kuwa na maslahi binafsi)
2. Vifaa vitakavyotumika studio. Kwa uzoefu wangu vikinunuliwa mara moja huweza kukaa muda mrefu mpaka vitakaponunuliwa vingine na hapa itakubidi kuwa na vifaa vinavyoendana na wakati huu maana zama zimebadilika. Ninaweza kukupatia list ya vifaa vinavyohitajika ili kuepuka kununua vifaa visivyo na ulazima kwa sasa
3. Acoustic treatment. Kama ndugu hazchem plate alivyosema, unaweza kuagiza fundi sofa akutengenezee japo binafsi nahisi ni vyema kuunda zile zinazohamishika ( zinaundwa kwa kuweka frame ya mbao iliyowambwa na kitambaa cha sofa na kuwekwa godoro ndani kisha zinashikizwa ukutani na nati ili iwe rahisi kuhamisha
Kwa leo niishie hapa ila usisite kuwasiliana nami kwa maelezo zaidi.
 
Asante sana nitumie namba yako ya Wattsup
 
Kama utahitaji music producer, nicheck pm
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Labda niongezee kitu hapo kwenye sound proof ambapo kitaalamu tunaita acoustic treatment hiki kipengele kinahitaji weledi wa hali ya juu na sio kweli kwamba Fundi wa kawaida anaweza kuitengeneza katika viwango vinavyotakikana, ila kutokana na gharama zilizopo kumpata acoustic engineer ni gharama hivyo tunawatumia mafundi sofa. Ila ukihitaji kutengeneza studio tafuta mtaalamu akuorodhoshee vitu vinavyohitajika. Wasaalam

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…