Ushauri wangu achana na unywaji wa vinywaji kama chai au kahawa yenye caffeine Badala yake mwambie mama watoto akyandalie chai yenye viungo vya asili vya chakula kama vile Tangawizi (zipo zilizosagwa) kitunguu swaumu, unga wa haradali, pilipili manga, mdalasini, sweet basil, coriander na kungumanga hivi vyote ukienda au akienda sokoni anavipata kwa urahisi Mwambie achanganye uwe unapata chai angalau Mara 2 kwa siku asubuhi na jioni,lakini pia unaweza kuandaa juisi ya tende na maziwa pia ni nzuri mwambie wifi ajitahidi kukupikia vyakula vya asili kama muhogo wa makopa na samaki wa kuchemsha n.k na kama unavuta sigara punguza au acha kabisa na kama wanywa pombe pia punguza ikibidi acha kabisa.