Nina vitz yangu; naomba ushauri niiunge taxify au niiunge uber?

Giannis Antetokounmpo

Senior Member
Joined
Jan 16, 2017
Posts
134
Reaction score
65
Za kwenu wapendwa,, nna vitz yangu hapa sema nlikua naomba ushauri niiunge taxify au niiunge uber na je huwez kujiunga zote mbili? wenye uzoefu wanisaidie
 
unga zote mbili inawezekana na uber ndo iko poa zaidi kwa dereva
 
Kaka sijajua malengo yako na hii biashara lakini kwa sasa kitumbua kimeingia mchanga.. Biashara imekua ngumu sana kote... Utaumiza gari na utachoma mafuta... Bei zimekua za kijinga hlf abiria nao hakuna.. Imagine taxify bomba kutoka kariakoo had masaki elfu 2...
 
Malengo yangu ni kununua na kutafuta dereva aendeshe then nipate hela weekly..
 
Duh..... Noma
 
Jiunge sports bet, biko au tatumzuka, uber kwa sasa nasikia biashara mbaya mana kuna kodi lukuki na dreva kidogo ndiyo mnufaika. Taxify ni ngeni na hakuna wateja wengi kivile so bei iko chini
 
Mimi nimeagiza Gari kabla sjiampa Dereva nikaamua Nianze kuliendesha Mwenyewe Kwanza Kama dereva na Mmliki pia.

Nimejaribu kufata Hints zao vizuri ikiwemo kuingia barabarani mida ambayo Demand ni kubwa na pia Maeneo potential kama city center, Maeneo kama mlimani city, Upanga,Mwenge,Koko,Masaki,Kurasini(Uhasibu/Kota Bandari)

Kwakweli biashara ni ngumu. You can imagine siku nzima napata wateja wa tatu.Mara wawili, Na bei ni kama mnavofaham zipo chini sana.

Nimewahi kumtoa mtu Baruti mpaka Tabata segerea ndani ndani offroad. Usiku bei ikaja Elf12 na barabara ni mbaya hatare.

Kkoo kurasini Sh 3000
Baruti - Mawasiliano tower. Law school Sh 4000

Mind you kuna wakati unapaki mahali 2hrs hujapata request.Unaamua kubadili location.kwa Garama zako. Na huko uendako huna uhakika wa mteja pia. Au ndo ukapata wale wa 3000. Au mara ukakutana na mtu anaoffer.

Kuna siku asubuhi nimeweka mafuta ya 20k. Mpaka usiku wa saa nne. Nimepata sh 15 tu. Hata ile 20k yangu haikurudi.

Kuifupi hii mimi nimeona ni biashara kichaa. Anaefaidika nu Taxify na Mteja. Dereva na mmiliki hali ni tete kwa sasa ivi.

Kama una Gari Taxify/Uber unaletewa hesabu vizuri nakushauri kakague Gari lako.
 
biashara kichaa hizi, bei ziko chini mno na gari zetu zina cc kubwa uber au taxify inataka gar yenye cc chini ya 1000
 
Upuuz. Wameharibu Career za Ma dereva Tax wa zamani kwakule huu utapeli.

Rafiki yangu alitoa passo yake Uber kampa Dereva. Kweli kila siku alipewa 30k. Lkn kabla mwezi haujaisha.jamaa kampigia simu gari imekufa Gear Box.
Ngumu sana gari kuendeshwa kwa bei hizo.na bado pesa ya ku service gari ikapatikana.

Wanataka gari ya Engine ndogo wakati huo huo Gari inazunguka kuliko uwezo wake. Kwa Garama ndogo.

Nadhani walipoanza Magari ya likuwa machache request zilikuwa nyingi zaidi.ila saivi ni majanda siki nzima unaeza pata wateja wa tatu. Hapo ww mwenye hujala wala hujanywa Maji.
 
Angalizo inapotokea fursa km iz inatakiwa uchangamkie fursa mwanzoni kbsa then watu wakishakuwa wengi unajiweka pembeni coz izi zinazohusiana na teknolojia huwa ni nzuri kwa kukuzia mitaji basi sio biashara za kufanya miaka yote same to m pesa na tigo pesa zilipoanza watu waliochangamkia mapema walipata sana hela
 
Hapo wanasema When you see the band wagon you are too late.

Kwa tafsri ya haraka, kitu kikishakua fasheni umechelewa.
 
mmh hiyo imekuwa boda boda
 
Wakuu na hawa watu wa taxify au uber wanafaidika vipi??
 
Mbona nakatishwa tamaa na nilikuwa na mpango niweke huko kagari kangu
 
Hii ninkawaida ya jf, kila wazo litakalotokea kujadiliwa lazima wawepo wa kukurudisha nyuma na kukukatisha tamaa, hizi ni roho za kishetani , kama mhusika jaribu kuifanya uzione changamoto ukiwa humo.
 
Hii ninkawaida ya jf, kila wazo litakalotokea kujadiliwa lazima wawepo wa kukurudisha nyuma na kukukatisha tamaa, hizi ni roho za kishetani , kama mhusika jaribu kuifanya uzione changamoto ukiwa humo.
Huoni mdau alichosema hapa chini?Unless kama hutaki kuambiwa ukweli wenyewe wa biashara hio kwa sasa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…