Nina wasiwasi Tanzania hatuna genes za ukanda wa Afrika mashariki ,mbona sisi tupo nyuma sana kwenye riadha

junky

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2017
Posts
413
Reaction score
978
Katika mashindano ya mita 10,000 yaliyofanyika juzi huko London nimefurahishwa na jambo moja katika top4 wote sana asili ya Afrika masharika.

1.Amezaliwa somalia/Asili yake ni Afrika Mashariki

2.Aliyeshika nafasi ya pili ni mkenya anatokea ukanda wa Afrika Mashariki

3.Aliyeshika nafasi ya 3 ni Mganda ,nafasi ya 4 muEthiopia na nafasi ya 5 ni MuEritrea wote wanatokea ukanda wa Afrika Mashariki.

Hata kwenye Mashindano ya Olimpic mwaka Jana kwenye 10k na 5k Metre ukanda wa Afrika Mashariki ulifanya vizuri kasoro Sir Mo Farah tu muingereza

Najiuliza hivi sisi Tanzania tuna genes za ukanda huu wa Afrika Mashariki kweli ,mbona tupo nyuma sana wenzetu Uganda,Kenya ,Ethiopia ,Eritrea hata Burundi wanafanya vema hata vijana 2 wenye asili ya kisomali/wakimbizi mmoja mcanada na mwingine Muingereza wanafanya vizuri kwenye riadha kwanini sio sisi.Katika mbio ndefu dunia inajua wazi kuwa watu wa ukanda wa Afrika mashariki ndio tishio lakini sie TZ tumelala

Tanzania nchi yangu "kichwa cha mwendawazimu" nina wasiwasi sisi huenda hatuna genes za ukanda huu .



 
Sisi ndo tuna genes kweli za Afrika Mashariki.... Hao wengine ndo wakuja!!!!
 
Tatizo sio genes bali investments ..

Hata diamond platnumz aliinvest pesa ndo imemfikisha hapo alipo hadi kuchukua tuzo za mtv lakini tukija upande wa michezo ,tuna muamko hafifu na hatufanyi michezo kama biashara wakati wenzetu wanapata pesa kupitia michezo...

Yule jamaa wa arusha alianza kupata airtime baaada ya kuingia tano bora ya olympic katika riadha ..Sasa hivi ana indorsements za makampuni lakini makampuni hayo hayo bado hayajawekeza zaidi ili kupata watu wengine zaidi ..yaani makampuni na serikali husubiri watu waliofanikiwa kwa kuhangaika sana yaani ready made na hii ndio tofauti yetu na wao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Simbu yuko nafas ya tatu at 1:56:18

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…