Nina wazo la kufanya biashara ya malighafi zitokanazo na mifugo

Gemini Are Forever

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2019
Posts
1,508
Reaction score
2,619
Hi, hustlers! Poleni na majukumu.

Rejea title hapo juu. Nina wazo la kuanza biashara ya malighafi zitokanazo na mifugo kama vile ngozi, pembe, kwato, meno, mifupa, mbolea n.k. ambapo mimi nitakuwa supplier.

Naomba mwenye ufahamu wake kwa namna yoyote ile na wa masoko kwa Dar na Tanzania kiujumla.

Asanteni!

CHASHA FARMING

GLOBAL CITIZEN

CONTROLA

Malila
 
Vitu ulivyotaja vinatumika kutengeneza gundi,viatu na vyakula vya mifugo kwa ushauri jaribu kutembelea viwanda vya bidhaa hizo wewe mwenyewe
 
Damian j Ntundagi said:
Vitu ulivyotaja vinatumika kutengeneza gundi, viatu na vyakula vya mifugo kwa ushauri jaribu kutembelea viwanda vya vitu hivyo wewe mwenyewe
Asante sana ndugu. Viwanda/kiwanda kinapatkana wapi kwa Dar au TZ kwa ujumla? Naomba mwongozo.
 
Pembe zinahitanika ila ni boashara ngumu sana ni tani na tani ndo unapaswa kukusanya, Kuhusu ngozi ni kwamba Ngozi zetu zina shida ya quality na hii inasababishwa na aina ya mifugo tulio nayo ambayo haina ubora.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbolea inaweza kuwa nafaida kama unazalisha mwenyewe na si kwenda kunununa then uuze, na pia tambua wakulima wengi hasa wa harakaharaka hawatumii mbole hizi kwa sababu zina virutubisho vya kiwango cha chini sana kulinganisha na za viwandani.

Mbole labda uwe na shamba lako unatumia kwenye kilimo chako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante CHASHA FARMING kwa ufafanuzi. Je, vipi kuhusu viwanda vinavyotengeneza bidhaa ztokanazo na malighafi hiz zitokanazo na mifugo kwa hapa Bongo vipo?
 
Soko la mbolea ya mifugo eg mbolea ya kuku mie nnalo la uhakika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Okwonkwo II said:
Soko la mbolea ya mifugo, e.g mbolea ya kuku mimi nnalo la uhakika
Mkuu mim nimelenga ktk soko la mifugo kama ng'ombe, mbuzi na kondoo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…