Ninahitaji mkopo wa machine hii:

Fadhili Paulo

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2011
Posts
3,211
Reaction score
993
Habari Wakuu,

Ninahitaji kampuni au mtu anayeweza kunikopesha mashine hii hapa kwenye picha, nahitaji chombo chenyewe kama kilivyo na siyo pesa lakini sina dhamana. Nitalirejesha deni hili (katika fedha) baada ya miezi 6 na nipo tayari kulipia riba ikiwa itakuwepo

Aliyetayari kunisaidia nitashukuru, nipo dar kwa sasa ila nikiipata tu naelekea mbeya.

Shukrani
 
Ina thamani ya sh ngapi?

Mtu anayetaka kukukopesha atakuwa na hakika gani kama utaweza kumrudishia pesa zake na hiyo riba?
 
Ina thamani ya sh ngapi?

Mtu anayetaka kukukopesha atakuwa na hakika gani kama utaweza kumrudishia pesa zake na hiyo riba?

1. Sijajuwa bei yake ya sasa hasa, lakini ni kati ya mil 2.5 hadi mil 5 inategemea unanuwa wapi.
2. Labda anaweza kunitaka mashahidi na tukafanya makubaliano kwa njia ya maandishi tu.

Karibu mkuu.
 
1. Sijajuwa bei yake ya sasa hasa, lakini ni kati ya mil 2.5 hadi mil 5 inategemea unanuwa wapi.
2. Labda anaweza kunitaka mashahidi na tukafanya makubaliano kwa njia ya maandishi tu.

Karibu mkuu.

Inatia wasiwasi kama kweli umejipanga vya kutosha. Kama hujui ni kiasi gani machine inauzwa unajuaje utaweza kurudisha deni na riba. Ni vyema ungeonyesha mchanganuo wa biashara yako ya kilimo ili watu waweze kukusaidia
 
Inatia wasiwasi kama kweli umejipanga vya kutosha. Kama hujui ni kiasi gani machine inauzwa unajuaje utaweza kurudisha deni na riba. Ni vyema ungeonyesha mchanganuo wa biashara yako ya kilimo ili watu waweze kukusaidia

Mkuu, we subiri mchanganuo hapo hapo nitakuandikia usijali. Hebu search ID yangu kwenye google halafu search na yako utagunduwa we ndo huaminiki. Dunia ya leo unahangaika kujuwa bei ya kitu?
 

Sijapata kusikia mikopo isiyo na rehani, hii mpya kwangu.
 
Jamaa anatafuta soln,kama huna weee potezea,think jinsi jamaa alivyo gather courage na kuamua kupost hii kitu,acheni kuwa na Phd(PullHimDown) mind wakuu alaa ,
 
Inategemea na uhitaji wako.. Wizara ya Kilimo ina mkataba na makampuni kadhaa.. ukiwa na hati ya kiwanja au shamba unafuzu kukopeshwa mashine... kazi ni kwako...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…