Ninamuhitaji mwanaume (hiv+)

Sweety Juma

Member
Joined
Nov 8, 2013
Posts
13
Reaction score
10
Salam wana JF. Mimi ni mwanamke mwenye umri miaka 48 ambaye naishi na VVU natafuta mwanaume wa kuishi nae au kufunga ndoa, kama yupo tayari. Awe na umri kuanzia miaka 50-55, kwa ufupi nilikuwa na mume ambae nilimuamini na kumpenda sana yeye ni mfanyabiashara nje na ndani ya nchi baada ya miaka 4 alianza mabadiliko ya kutowasiliana tena na mimi. Mwaka uliofuta nilipata mchumba na tulihitaji kufunga ndoa nikaona niende ANGAZA kuangalia afya yangu lakini haikuwa siku nzuri kwangu kwani nilijikuta nimeshapata maambukizo sikuwa na jinsi. Nilimuomba Mungu katika sala zangu anisaidie na kunitia nguvu katika maisha yangu ya upweke. Kwa vile nimezoea kuwa na mwenzangu kuishi peke yangu ni vigumu kwangu, nami naomba kujitokeza mimi nipo katika ukweli (serious) na tutalindana.
 
kila la kheri ndugu na Mwenyezi Mungu akusaidie na akujaalie haja za moyo wako kwa kadiri ya rehema zake.
 
Kila la kheri my dia naamini yupo atakaekuwa rizki yako ila iwe ndoa sawa,
 
... Sweet Juma pole sana kwa upweke ulionao ila nikuambie kitu dada yangu, usithubutu kumtafuta huyo mwanaume kwa presha sana, wewe tulia muombe Mwenyezi Mungu na ninaamini atashusha rehma zake na utampata ambaye unamhitaji..ukifanya kwa haraka sana (desperately), unaweza kupata pasua kichwa akakuumiza tu akili yako..utafanikiwa na ninakutakia kila la kheri inshaallah!
 
Last edited by a moderator:
Umri na status haitoshi, weka dini yako ikiwezekana na wapi unakaa.
Mungu akupe hitaji la moyo wako.
 
Asante dada nimekuelewa nasema Inshaallah kwa uwezo wa Mungu. Ck njema.
 
Sasa miaka 48,tena mwanamke bado tu unahitaji kuolewa,mbona kama miaka emeenda sana?
 

Pole, maisha ndivyo yalivyo. Nafikiri wahusika wamekusoma na huenda wakakutafuta. Pengine pia kwenye maeneo yale ya vituo vya kuchukulia dawa, huwa watu wenye status hii wapo pia .....

Nakutakia kila la kheri.
 
sweety juma , pole sana naamini mungu atazidi kukupigania na utapata hitaji lako .. na pia nakupa hongera kwa ujasiri wako ulioonyesha kwa kujikubali na kufanya maamuzi ambayo yatarudisha furaha katika maisha yako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…