Ninaomba ushauri kuhusu kudhibiti maua ya mparachichi yasipukutike

Ninaomba ushauri kuhusu kudhibiti maua ya mparachichi yasipukutike

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
21,741
Reaction score
26,735
Kama kichwa cha Posti kinavyojieleza, ninaishi Dar es Salaam jiji la joto jingi baridi nadra labda tu ikitokea malaika wa baridi amefurahi kama ilivyotokea mwaka mmoja kati ya 90 ambapo watu waliota moto usiku, hiyo ndiyo hali ya hewa nilipo.

Ardhi ni mchanga zaidi usiojulikana mchanganyiko wake kutokana na tabia zetu mbovu za uchafuzi wa mazingira, hali ya hewa ni moshi mwingi kutokana na magari mengi yanayozurula kutwa kucha kuwa ni mitumba, pia uchomaji wa taka mitaani usioisha, natumai kwa utangulizi huu mtaalamu atanishauri nitumie nini kutatua tatizo la miti yangu.

Hii miti ukifika msimu wa kutoa maua hutoka ila hupukutika katika muda mfupi licha ya kujaribu kupulizia dawa ambayo huenda si sahihi, ombi langu kwa wenye uzoefu na utaalamu mnishauri nini cha kufanya ili kuzuia hayo maua yasipukutike kwani yakipukutika ni mpaka mwaka mwingine ndipo yachanue tena, kumbuka nami nitakua nimepunguza mwaka mmoja wa kula hayo matunda kwani nami ninakua.

Karibuni wataalamu wa miti ya matunda hasa miparachichi.
 
Watu wa SUA mje mtoe msaada huku
Bahati nzuri nilifika huko, wee isikie tu, mwaka jana nilikwenda nikakuta wameotesha mizabibu ikionesha matumaini kwani ilizaa, mwezi uliopita nilikwenda nione ikoje, mm! Sikuamini nikakuta wameitelekeza! SUA kampasi ya mjini wanalo eneo kubwa sana old Iringa Road ambalo wangelitumia kama shamba darasa kwa wananchi, limebaki pori tuu wanalitumia kiduchu sana hapo Apopo na Panya wa mabomu vitu visivyokuwa na tija yo moja kwa moja kwa wananchi.
 
Bahati nzuri nilifika huko, wee isikie tu, mwaka jana nilikwenda nikakuta wameotesha mizabibu ikionesha matumaini kwani ilizaa, mwezi uliopita nilikwenda nione ikoje, mm! Sikuamini nikakuta wameitelekeza! SUA kampasi ya mjini wanalo eneo kubwa sana old Iringa Road ambalo wangelitumia kama shamba darasa kwa wananchi, limebaki pori tuu wanalitumia kiduchu sana hapo Apopo na Panya wa mabomu vitu visivyokuwa na tija yo moja kwa moja kwa wananchi.
NIpo huku, lile eneo wangetukatia viwanja tujenge nyumba, lipo katikati ya mji na halitumiki kwa weledi na usahihi.
Naona elimu wanafanya kwa nadharia madarasani vitendo hakuna.
Moja ya sababu ya SUA kupewa yale maeneo makubwa ni kuyatumia kwa kilimo kama darasa kwa vitendo.
Wapime mipango mji wananchi tununue tujenge nyumba .
Walikupa ushauri gani kuhusu maua ya miti yako?
 
Hii ni hatari, inamaana hakuna anayejua jinsi ya kuzuia maua yasipukutike au wate wanapenda Posti za kula tunda kimasihara.
 
Bahati nzuri nilifika huko, wee isikie tu, mwaka jana nilikwenda nikakuta wameotesha mizabibu ikionesha matumaini kwani ilizaa, mwezi uliopita nilikwenda nione ikoje, mm! Sikuamini nikakuta wameitelekeza! SUA kampasi ya mjini wanalo eneo kubwa sana old Iringa Road ambalo wangelitumia kama shamba darasa kwa wananchi, limebaki pori tuu wanalitumia kiduchu sana hapo Apopo na Panya wa mabomu vitu visivyokuwa na tija yo moja kwa moja kwa wananchi.
Tanzania kitu tunaweza fanya Kwa pamoja na kikafanikiwa ni choir.

Watachanga hata laki5 Tano wanunue vyombo vya mziki vya kisasa na harambee kibao lakini kamwe Hawa Hawa hawawezi simamia kiwanda hata kama ni chakutengeneza sabuni.


Nirudi kwenye maada Yako mkuu. Nimegundua na kuelewa wasomi wetu wengi wanasoma Ii waje kuajiriwa na sio kujiajiri!!!


Mkuu hapa mtaani Kuna jamaa kasoma SUA pale miaka3 karudi akaanza kujifunza kunyoa na alipojua akafungua saloon yake.

Nilishangaa mshangao mkubwa mno nikajiuliza au hiki chuo chetu kimerogwa?

Ingia TikTok uwakute wakenya asee wako mbali mno sio kilimo Wala mifugo na watoto ni wasomi kitu wasichokuwa nacho wao ni ardhi ya kutosha tu.

Huyu jamaa nilijua Sasa tumepata mtatuzi wa maswala ya kilimo kumbe hamna kitu. Akili yote anasubiri kuajariwa saivi yupo kahama kahamishia kule ofisi yake!!


Ninachojua kuhusu mmea kupitisha maua kwanza ni Hali ya hewa either maji kuwa mengi au kukoswa maji hizi ndo changamoto kubwa.

Zingine ni kama magonjwa ya ukungu nk. Nakujibu kama mkulima tu mkuu sio mtaalamu Cha msingi onana na wakulima wenzio watakupa abc. Ahsantee sana
 
Hii ni hatari, inamaana hakuna anayejua jinsi ya kuzuia maua yasipukutike au wate wanapenda Posti za kula tunda kimasihara.
Dar es Salaam maparachichi yanazaa? Sina uhakika lakini pengine ni hali ya hewa hairuhusu. Hata ukichukuwa mnazi ikapanda sehemu kama Klimanjaro utaota vizuri lakini utakuwa hauzai nazi. Sina uhakika na maelezo yangu.
 
Dar es Salaam maparachichi yanazaa? Sina uhakika lakini pengine ni hali ya hewa hairuhusu. Hata ukichukuwa mnazi ikapanda sehemu kama Klimanjaro utaota vizuri lakini utakuwa hauzai nazi. Sina uhakika na maelezo yangu.
Ipo na inazaa vizuri tu, ila tatizo ni wadudu hushambulia maua.
 
Mkuu kuanguka kwa Maua au mti kupukitisha Maua Kuna sababishwa na vitu vifuatavyo
1. Magonjwa inapoteka mti umeathiliwa na ugojwa wowote ule kipindi cha mau inapelekea kupata mshtuko ivyo asilimia kubwa ya Maua hudondoka ili kuunusuru mti kufa

2. Uhaba wa virutubisho hasa Potassium na Phosphorus maana ni muhimu sana kwenye hatua ya mmea kutengeneza Maua

3. Uwingi wa virutubisho vya Nitrogen kwenye udongo maana upelekea kudhuia mizizi ya mmea kuchukua Potassium kwenye udongo ivyo inashauriwa kipindi cha Maua kiwango Cha nitrogen inabid kiwe chini au kiasi kwenye udongo ili kuruhusu mmea kupokea virutubisho vya Potassium

4. Hali ya hewa pale mvua itakap nyesha inapelekea Maua kudondoka au upepo ukiwa mkubwa ndio maana miti mingi hutoa maua kipindi cha ukame ili kuepukana na iyo kasumba

5. Kukuosekana kwa vichavushaji na urutubishaji ipo ivi baada ya ua kufunguka hasa kwa parachichi inabidi uchavushaji na urutubishaji utokee kwa kutumia upepo, wadudu na nk ikitokea akuna uchavushaji Wala urutubishaji basi ua lazima lidondoke maana kwenye parachichi ni vigumu kutengeneza tunda bila ya uchavushaji na urutubishaji

6. Maamuzi ya mti wenyewe pale inapo tokea idadi ya Maua ni mengi kuliko uwezo wa mti basi mti lazima udondoshe baadhi ya mau ili kupata matunda yenye size inayo faa uku mmea ukipata chakula chake kwa usahihi

7. Aina ya parachichi apa Kuna aina mbili tuu A & B Sasa ipo ivi parachichi A huwa maua yake huwa yakike asubuhi ya siku ya kwanza na Kisha kuwa jinsia ya kiume siku ya pili mchana kwa upande wa parachichi B ni kinyume chake Cha Parachichi B. Ivyo inashauriwa mkulima kuwa na ana zote za parachichi shambani kwako ili kupunguza kudondoka kwa Maua kutokana urutubishaji hafifu



Sasa kutokana na izo sababu utachunguza mwenyewe ipi imesababisha kudondoka kwa Maua Yako
 
Mkuu kuanguka kwa Maua au mti kupukitisha Maua Kuna sababishwa na vitu vifuatavyo
1. Magonjwa inapoteka mti umeathiliwa na ugojwa wowote ule kipindi cha mau inapelekea kupata mshtuko ivyo asilimia kubwa ya Maua hudondoka ili kuunusuru mti kufa

2. Uhaba wa virutubisho hasa Potassium na Phosphorus maana ni muhimu sana kwenye hatua ya mmea kutengeneza Maua

3. Uwingi wa virutubisho vya Nitrogen kwenye udongo maana upelekea kudhuia mizizi ya mmea kuchukua Potassium kwenye udongo ivyo inashauriwa kipindi cha Maua kiwango Cha nitrogen inabid kiwe chini au kiasi kwenye udongo ili kuruhusu mmea kupokea virutubisho vya Potassium

4. Hali ya hewa pale mvua itakap nyesha inapelekea Maua kudondoka au upepo ukiwa mkubwa ndio maana miti mingi hutoa maua kipindi cha ukame ili kuepukana na iyo kasumba

5. Kukuosekana kwa vichavushaji na urutubishaji ipo ivi baada ya ua kufunguka hasa kwa parachichi inabidi uchavushaji na urutubishaji utokee kwa kutumia upepo, wadudu na nk ikitokea akuna uchavushaji Wala urutubishaji basi ua lazima lidondoke maana kwenye parachichi ni vigumu kutengeneza tunda bila ya uchavushaji na urutubishaji

6. Maamuzi ya mti wenyewe pale inapo tokea idadi ya Maua ni mengi kuliko uwezo wa mti basi mti lazima udondoshe baadhi ya mau ili kupata matunda yenye size inayo faa uku mmea ukipata chakula chake kwa usahihi

7. Aina ya parachichi apa Kuna aina mbili tuu A & B Sasa ipo ivi parachichi A huwa maua yake huwa yakike asubuhi ya siku ya kwanza na Kisha kuwa jinsia ya kiume siku ya pili mchana kwa upande wa parachichi B ni kinyume chake Cha Parachichi B. Ivyo inashauriwa mkulima kuwa na ana zote za parachichi shambani kwako ili kupunguza kudondoka kwa Maua kutokana urutubishaji hafifu



Sasa kutokana na izo sababu utachunguza mwenyewe ipi imesababisha kudondoka kwa Maua Yako
Nina zaidi ya mmoja, kwa ushauri wako mzuri itabidi niiulize upi ni dume na jike ni upi, kisha jike niuvishe shanga kuweka kumbukumbu.
 
Kama shida ni kupukutisha mauwa inaweza kuwa shidaya wadudu au hali ya hewa.

Kama ni hali ya hewa ningeshauri labda upulize CHLOROTHALONIL
lakini kama ni wadudu, wapige PROFENOFORCE 72% (Nenda pale Kisutu sokoni ghorofa ya juu kabisa kuna maduka ya Kilimo) nunua Profenoforce 72% ukapulize.
Na hiyo ya hali ya hewa ulizia CHOLOROCARE.
 
Dar joto ni kali hivyo wadudu kama thrips, chawa wekundu na buibui nanasuck sap kwenye mimea hivyo ipelekea mara kupukutika hivyo tumia dawa ya sulphur ya unga na cabaret ya maji , kuhusu mbolea tumia ya mara mira winner na booster za maji zenye high k kwa wingi . Nina mashamba niliyoyasimamia na kuyaludisha katika uzalishaji mzuri huko nyanza za juu kusini.
 
Back
Top Bottom