1. Kwanza hakikisha umetengeneza jina. Unaeza kutengeneza jina kwa kujitolea kufundisha shule fulani bila malipo au malipo kidogo.
Njia nyingine andaa notes za topic unazozikubali uchapishe halafu usambaze kwenye shule mbali mbali.
2. Tafuta sehemu ambayo imekaa vizuri kufungua tuition, unaweza kuomba chumba kwenye shule ya serikali. Au unaweza kujiunga na watu ambao wanafundisha tuition halafu mkaunganisha nguvu.(kama huna jina ni vizuri kuunganisha nguvu na wadau).
3. Vifaa vya kufundishia sio gharama kama una chumba kwa hiyo unaweza kuanza kufundisha.
Changamoto:
1. Kama uko kijijini mwamko wa elimu ni mdogo hivyo tegemea wateja watakua wachache au wazinguaji
2. Kama uko town hakikisha u unafundisha kwa moyo. Mara nyingi watoto wa town wanatabia ya kupima uwezo pamoja na kuzingua kwenye malipo. Usikate tamaa mwanzo utakua mgumu lakini baadaye mambo yatakua fresh