Ninapotaka kumshtaki mtu Mahakamani natakakiwa nianzie wapi?

Ninapotaka kumshtaki mtu Mahakamani natakakiwa nianzie wapi?

Dali Mpofu

Senior Member
Joined
May 9, 2021
Posts
173
Reaction score
328
Habari zetu wote?

Ni utaratibu upi wa kufuata ukitaka kumpeleka mtu mahakamani (kumshtaki)? Ni lazima uanzie kituo cha polisi au? Msaada tafadhali
 
Hali ngumu?,,Hata uende wapi sikupi fidia ya pesa ndugu
 
Inategemeana na kesi, mfano ni kesi ya jinai au ni kesi ya madai?

Kama ni kesi ya madai (civil case) hutakiwi kwenda polisi kwa sababu polisi hawahusiki na kesi za madai wala hawaruhusiwi kumkamata mtu kwa kosa la madai (Ingawa in practice wanafanya hivyo lakini sio sahihi). Badala yake nenda Mahakamani moja kwa moja ukafungue kesi au mpe kwanza mdaiwa demand notice (demand letter) alafu muda uliompa kwenye hiyo notice ukiisha hajatekeleza madai yako nenda Mahakamani ukafungue malalamiko au kesi yako.

Kama ni kosa la jinai mfano wizi, mauaji, ubakaji, n.k. anzia kuripoti kituo cha polisi baadae mtuhumiwa atakamatwa, kuchukuliwa maelezo ya kosa na atapewa dhamana kama kosa linadhaminika, baadaye atafikishwa Mahakamani kusomewa mashtaka.

Kikubwa ujue aina ya kosa au aina ya madai

Kuna makosa au madai yanatakiwa kwenda Mahakama ya Mwanzo, mengine Mahakama ya Wilaya na mengine Mahakama Kuu.

Mara nyingi tunaangalia eneo tukio lilipofanyikia, mahali mdaiwa anapokaa na thamani ya kitu au kiwango cha pesa unayodai n.k.
 
Inategemeana na kesi, mfano ni kesi ya jinai au ni kesi ya madai?

Kama ni kesi ya madai (civil case) hutakiwi kwenda polisi kwa sababu polisi hawahusiki na kesi za madai wala hawaruhusiwi kumkamata mtu kwa kosa la madai (Ingawa in practice wanafanya hivyo lakini sio sahihi). Badala yake nenda Mahakamani moja kwa moja ukafungue kesi au mpe kwanza mdaiwa demand notice (demand letter) alafu muda uliompa kwenye hiyo notice ukiisha hajatekeleza madai yako nenda Mahakamani ukafungue malalamiko au kesi yako.

Kama ni kosa la jinai mfano wizi n.k. anzia kuripoti kituo cha polisi baadae mtuhumiwa atapewa dhamana kama kosa linadhaminika, baadaye atafikishwa Mahakamani.

Kikubwa ujue aina ya kosa au aina ya madai

Kuna makosa au madai yanatakiwa kwenda Mahakama ya Mwanzo, mengine Mahakama ya Wilaya na mengine Mahakama Kuu.
Asante sana kwa elimu hii
 
Habari zetu wote?

Ni utaratibu upi wa kufuata ukitaka kumpeleka mtu mahakamani (kumshtaki)? Ni lazima uanzie kituo cha polisi au? Msaada tafadhali
Inategemea na kesi inahusu nini,kama ninai unaweza kwenda polisi au mahakamani lkn kama ni madai nenda mahakamani
 
Back
Top Bottom