Ninasikitishwa na kitendo cha mwanariadha mtanzania Gabriel Geay kutomaliza mbio za Boston Marathon. Ni ukosefu wa uzalendo

Ninasikitishwa na kitendo cha mwanariadha mtanzania Gabriel Geay kutomaliza mbio za Boston Marathon. Ni ukosefu wa uzalendo

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
Nimesikitishwa sana na kitendo cha mwanariadha Mtanzania Gabriel Geay kutomaliza mbio za Boston Marathon na kuachia katikati mara baada ya kuvuka 21km.

Huu ni ukosefu wa uzalendo na kukata tamaa. Hii sio mara ya kwanza kwa kijana wetu kufanya hiki kitendo cha hovyo. Mbio sio kuanza ni kumaliza. Kijana jifunze walivyofanya wakongwe kina John Steven Akhwari na Filbert Bayi...

Mzee John Steven alihakikisha anamaliza mbio huko Mexico akiwa ameumia mguu ambapo kila mwaka familia ya riadha duniani hukumbuka kitendo chake hicho cha kizalendo.

Hata Mzee Filbert Bayi alipoanza kukimbia Marathon kuna baadhi ya mbio alikuwa haingii hata top 30 lakini alikuwa anahakikisha anamaliza mbio. Geay aelewe kwamba sio kila siku atakuwa mshindi au kuingia top ten. Kuna siku zingine huwa mbaya.
 
Tena kitendo hicho Sio tu Ukosefu Wa Uzalendo Bali ni Ufujaji Mkubwa Wa Kodi za Wananchi ikiwemo Kodi Yangu...!

Na tunao Vijana Wengi Wengi tu ambao hiyo nafasi Wanaitaka... !

Huyo kashajiona Star,Wa Nini Kumng'ang'ania..? Apigwe Chini tu next time.

Naunga mkono hoja!
 
Hiyo ni Kazi yake kama zilivo kazi nyingine, hajaipeperusha vyema bendera yetu aliyokabadhiwa.
 
hadi nimepata hasira huyo akirudi tz achapwe vboko 15 pale uwanja wa ndege halafu tumachpe viboko 34 uwanja wa benjamin mkapa mbele ya umma tena iwe tarehe 20 labla ya mechi kuanza
 
Labda kama pumzi ilikata,wakati unakimbia unaambiwa uusikilize mwili wako unasema nini,sio unakimbia tu kwa kutafuta uzalendo,utafia kwenye pitch...
 
Back
Top Bottom