Ninavyomkumbuka baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mwalimu mtu wa watu 2

Ninavyomkumbuka baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mwalimu mtu wa watu 2

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
NINAVYOMKUMBUKA BABA WA TAIFA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE
MWALIMU MTU WA WATU 2

Mwalimu alikuwa mtu kutoka bara, Mkristo Mkatoliki.

Alianza siasa hasa za kudai uhuru wa Tanganyika katika mazingira ya Dar es Salaam akiwa kazungukwa na Uislam na Waislam.

Kulikuwa na tofauti kubwa katika ya kiongozi huyu na wale aliokuwa akiwaongoza.

Siku hizo Mwalimu kijana mdogo wa miaka 30.

Kivazi chake kilikuwa kaptula na siksi ndefu, stokingi.
Mavazi rasmi ya wasomi.

Katika TAA, Mwalimu aliwakuta vijana wengine kama Abdul na Ally Sykes, Hamza Mwapachu, Steven Mhando na Zuberi Mtemvu.

TANU ilipoundwa mwaka wa 1954 kukawa na baraza la wazee chini ya Sheikh Suleiman Takadir.

Baraza hili lilijumuisha wazee wengi maarufu wa mjini na masheikh. Katika hali kama hii ungejihisi kuwa Mwalimu yupo ugenini.

La hasha, Mwalimu alienea vyema katika kundi hili la Waswahili na masheikh.

Mwalimu aliwanyenyekea na kuzungumzanao katika lugha waliyoielewa. Mwalimu akizungumza Kiswahili safi na fasaha bila ya lafidhi ya kwao Musoma.

Kwa aliyekuwa hamfahamu Mwalimu ilikuwa vigumu kuweza kujua kama alikuwa Mzanaki wa Musoma, tena vijijini.

Mwalimu aliwavutia zaidi wazee wale kwa ustadi wake wa kucheza bao.
Sehemu za pwani mchezo wa bao kwa kawaida ni mchezo wa wazee.

Aghlabu vijana kuucheza mchezo huu.
Wazee wa tano wengi wao walikuwa wapenzi wa bao.

Mchezo wa bao ni mchezo wa kupanga mikakati na kupiga hesabu namna ya kumpiku mpinzani wako.

Mwalimu alilimudu sana bao.

Wazee wa TANU walimuheshimu sana Mwalimu walipokuja kugundua kuwa alikuwa bingwa wa kete.

Kati ya marafiki zake katika enzi zile walikuwa wapinzani wake wakubwa katika bao,
Mzee Mshume Kiyate, Mwinjuma Mwinyikambi, Boi Singizi, Jumbe Tambaza na wengine wengi.

Picha inamuonyesha Mwalimu Nyerere akiwa na Mshume Kiyate kulia Max Mbwana na Mwinjuma Mwinyikambi na hiyo nyingine ni Ally Sykes na Julius Nyerere.
 

Attachments

  • MSHUME, MAX MBWANA....jpg
    MSHUME, MAX MBWANA....jpg
    43.2 KB · Views: 3
  • NYERERE NA ALLY SYKES.JPG
    NYERERE NA ALLY SYKES.JPG
    22.2 KB · Views: 3
Naomba kuuliza ! kati ya Hayati Mwalim JK na Moringe Sokoine nani alikuwa ni mtu wa watu & na Mzalendo kuliko mwenzie? Please don't be biased
 
NINAVYOMKUMBUKA BABA WA TAIFA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE
MWALIMU MTU WA WATU 2

Mwalimu alikuwa mtu kutoka bara, Mkristo Mkatoliki.

Alianza siasa hasa za kudai uhuru wa Tanganyika katika mazingira ya Dar es Salaam akiwa kazungukwa na Uislam na Waislam.

Kulikuwa na tofauti kubwa katika ya kiongozi huyu na wale aliokuwa akiwaongoza.

Siku hizo Mwalimu kijana mdogo wa miaka 30.

Kivazi chake kilikuwa kaptula na siksi ndefu, stokingi.
Mavazi rasmi ya wasomi.

Katika TAA, Mwalimu aliwakuta vijana wengine kama Abdul na Ally Sykes, Hamza Mwapachu, Steven Mhando na Zuberi Mtemvu.

TANU ilipoundwa mwaka wa 1954 kukawa na baraza la wazee chini ya Sheikh Suleiman Takadir.

Baraza hili lilijumuisha wazee wengi maarufu wa mjini na masheikh. Katika hali kama hii ungejihisi kuwa Mwalimu yupo ugenini.

La hasha, Mwalimu alienea vyema katika kundi hili la Waswahili na masheikh.

Mwalimu aliwanyenyekea na kuzungumzanao katika lugha waliyoielewa. Mwalimu akizungumza Kiswahili safi na fasaha bila ya lafidhi ya kwao Musoma.

Kwa aliyekuwa hamfahamu Mwalimu ilikuwa vigumu kuweza kujua kama alikuwa Mzanaki wa Musoma, tena vijijini.

Mwalimu aliwavutia zaidi wazee wale kwa ustadi wake wa kucheza bao.
Sehemu za pwani mchezo wa bao kwa kawaida ni mchezo wa wazee.

Aghlabu vijana kuucheza mchezo huu.
Wazee wa tano wengi wao walikuwa wapenzi wa bao.

Mchezo wa bao ni mchezo wa kupanga mikakati na kupiga hesabu namna ya kumpiku mpinzani wako.

Mwalimu alilimudu sana bao.

Wazee wa TANU walimuheshimu sana Mwalimu walipokuja kugundua kuwa alikuwa bingwa wa kete.

Kati ya marafiki zake katika enzi zile walikuwa wapinzani wake wakubwa katika bao,
Mzee Mshume Kiyate, Mwinjuma Mwinyikambi, Boi Singizi, Jumbe Tambaza na wengine wengi.

Picha inamuonyesha Mwalimu Nyerere akiwa na Mshume Kiyate kulia Max Mbwana na Mwinjuma Mwinyikambi na hiyo nyingine ni Ally Sykes na Julius Nyerere.
Mbona waisilamu hawakuonekana tena, baada ya uhuru hata kwenye serikali yake mlikuwa wachache wakati mnadai nyie ndo mlimpokea mualimu na kumuelekeza la kufanya?
 
Mbona waisilamu hawakuonekana tena, baada ya uhuru hata kwenye serikali yake mlikuwa wachache wakati mnadai nyie ndo mlimpokea mualimu na kumuelekeza la kufanya?

Mzanaki aliji Mwambafy kila Sehemu atajwe Yeye tu

Kambarage alikuwa Kibaraka wa Wachina na Warusi
 
Naomba kuuliza ! kati ya Hayati Mwalim JK na Moringe Sokoine nani alikuwa ni mtu wa watu & na Mzalendo kuliko mwenzie? Please don't be biased
. Ebu mwacheni baba Wa taifa hili apumzike kwa amani amefanya mengi Leo Hii tuna peruzi humu jF ni kwa jitihada zake na wazee wengine walio shikamana naye nadhani si busara Sana kuwa kila siku iibuke mijadala juu ya kile alicho kifanya katika namna ya kubeza IWENI NA SHUKRANI
 
Naomba kuuliza ! kati ya Hayati Mwalim JK na Moringe Sokoine nani alikuwa ni mtu wa watu & na Mzalendo kuliko mwenzie? Please don't be biased
As...
Naandika historia ya Nyerere 1950s kafika Dar es Salaam harakati za kudai uhuru zinaanza...
 
Mbona waisilamu hawakuonekana tena, baada ya uhuru hata kwenye serikali yake mlikuwa wachache wakati mnadai nyie ndo mlimpokea mualimu na kumuelekeza la kufanya?
SERIKALI ALIYOIONGOZA MWALIMU HAIKUWA NA WAISLAMU WALA WAKRISTO ,BALI #WATANGANYIKA PEKEE hayo mnayo yawaza sasa havikuwa vipaumbele vya mashujaa wale
 
NINAVYOMKUMBUKA BABA WA TAIFA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE
MWALIMU MTU WA WATU 2
Mwalimu alikuwa mtu kutoka bara, Mkristo Mkatoliki.
Alianza siasa hasa za kudai uhuru wa Tanganyika katika mazingira ya Dar es Salaam akiwa kazungukwa na Uislam na Waislam.
Kulikuwa na tofauti kubwa katika ya kiongozi huyu na wale aliokuwa akiwaongoza.
Siku hizo Mwalimu kijana mdogo wa miaka 30.
Kivazi chake kilikuwa kaptula na siksi ndefu, stokingi.
Mavazi rasmi ya wasomi.
Katika TAA, Mwalimu aliwakuta vijana wengine kama Abdul na Ally Sykes, Hamza Mwapachu, Steven Mhando na Zuberi Mtemvu.
TANU ilipoundwa mwaka wa 1954 kukawa na baraza la wazee chini ya Sheikh Suleiman Takadir.
Baraza hili lilijumuisha wazee wengi maarufu wa mjini na masheikh. Katika hali kama hii ungejihisi kuwa Mwalimu yupo ugenini.
La hasha, Mwalimu alienea vyema katika kundi hili la Waswahili na masheikh.
Mwalimu aliwanyenyekea na kuzungumzanao katika lugha waliyoielewa. Mwalimu akizungumza Kiswahili safi na fasaha bila ya lafidhi ya kwao Musoma.
Kwa aliyekuwa hamfahamu Mwalimu ilikuwa vigumu kuweza kujua kama alikuwa Mzanaki wa Musoma, tena vijijini.
Mwalimu aliwavutia zaidi wazee wale kwa ustadi wake wa kucheza bao.
Sehemu za pwani mchezo wa bao kwa kawaida ni mchezo wa wazee.
Aghlabu vijana kuucheza mchezo huu.
Wazee wa tano wengi wao walikuwa wapenzi wa bao.
Mchezo wa bao ni mchezo wa kupanga mikakati na kupiga hesabu namna ya kumpiku mpinzani wako.
Mwalimu alilimudu sana bao.
Wazee wa TANU walimuheshimu sana Mwalimu walipokuja kugundua kuwa alikuwa bingwa wa kete.
Kati ya marafiki zake katika enzi zile walikuwa wapinzani wake wakubwa katika bao,
Mzee Mshume Kiyate, Mwinjuma Mwinyikambi, Boi Singizi, Jumbe Tambaza na wengine wengi.
Picha inamuonyesha Mwalimu Nyerere akiwa na Mshume Kiyate kulia Max Mbwana na Mwinjuma Mwinyikambi na hiyo nyingine ni Ally Sykes na Julius Nyerere.
ubarkiwe mzee wetu kwa kutupatia chakula cha ubongo
 
Aghalabu - Mara kwa Mara, often

Nadra - Mara chache, Rare
 
Mkuu acha jazba kama unalojibu sahihi basi tupe na kama hauna acha kumkingia kifua
 
Halafu kuna watu wanatudanganya Tanzania tunaongea Kiswahili shauri ya Mwalimu Nyerere, sasa yeye Kiswahili alikijulia wapi huko Musoma kama yeye ndiyo sababu ya watu wa Musoma na kwingineko kuongea Kiswahili?
 
Halafu kuna watu wanatudanganya Tanzania tunaongea Kiswahili shauri ya Mwalimu Nyerere, sasa yeye Kiswahili alikijulia wapi huko Musoma kama yeye ndiyo sababu ya watu wa Musoma na kwingineko kuongea Kiswahili?
Nyerere alichangia ukuzi na uwenezi wa kiswahili tu.....ila kiswahili kilimsaidia sana katika harakati za kudai Uhuru na kutawala wa tanganyika bila kuhoji kabila lake dogo
 
Back
Top Bottom