Ninawashangaa sana Simba kuleta maneno maneno hadi mpinzani anatumia kila mbinu za kujihami. Hivi hamjifunzi kwao jamaa walifanyaje?

Ninawashangaa sana Simba kuleta maneno maneno hadi mpinzani anatumia kila mbinu za kujihami. Hivi hamjifunzi kwao jamaa walifanyaje?

kibaravumba

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2012
Posts
6,634
Reaction score
7,015
Ninasikitishwa sana na mbinu za maneno maneno kutoka club yangu ya Simba wakidhani yana msaada wowote katika ushindi.

Nimeona Kaizer chief wameanza kijihami ikiwa ni pamoja na kulalamikia waamuzi.Niliona watu wakishangilia baada ya kuona waamuzi wa mchezo huo kutoka Burundi,na hasa wachambuzi wa michezo ambao siku zote nawaona kama wachawi namba moja wa soka letu.Kuna haja gani ya kuanza kuanika mbinu kama zipo za ushindi?

Mbona jamaa wao walijifanya wajinga ikiwa ni pamoja na waandishi wao wa habari wakiisifu Simba na kujidai wameiogopa,jambo lililowahadaa wachezaji wetu wakajikuta wanashangazwa mapema kabisa.

Kwa ujumla Simba tumefeli kwani tulishindwa kunyamaza na kuanza kuitisha press conference ambayo naona labda ni kwa ajili ya kupata viingilio tu.Sioni kama kweli kuna nia thabiti ya kumtoa Kaizer Chief. Na bahati mbaya,wachezaji wetu ni kama walikuwa na mgomo fulani.Je huu mgomo umeisha?
 
Mbona mnapenda ramli Mkuu, huo mgomo uliibuka lini?
 
Huu weledi unaoutaka kwa Tanzania haupo na hii inatokana na elimu ndogo sana ya mambo hayo mamelody wanamjua manara kuliko kocha wa simba ila si tunamjua kocha wa mamelody na wachezaji
 
Simba wataonga ma refa wapewe penalty mapema, na natabiri penalti watapewa na refa.. ila kupita simba hawatapita.. maana refa hata umuonge vipi hawezi kutoa penalti 4
 
Simba ameishatolewa kwenye mashindano hizo ni mbwembwe tu za mazwazwa. Kwa mpira gani au ufundi gani mlionao wa kuweza kuwafunga CHIEF KAIZER.
 
Kaizer Chiefs na wao ni waoga sana, yaani wanavyolalamika ni kama enzi zile timu za Tz zikiwa zinaenda kwa nchi za kiarabu, na huu uoga wao ndio utawapoteza na kuwaletea mhaho.
 
Tatizo ni Manara...mpira wa mdomoni ndo unaiangusha Simba,....

Hebu fikiria, Manara anasema viongozi wamejiandaa kwa ajili ya mechi..,hivi wanaojiandaa ni wachezaji au ni viongozi?

Simba wapunguze tambo na kidomo domo mtandaoni, waandae timu...

hata hivo Kaizer atakufa tu hakuna namna....SIMBA NGUVU MOJA...
 
Kaizer Chiefs wasipoingiza timu Simba atapewa magoli matatu na pointi tatu, Kisha atatolewa
Hyo ni Sheria gani hao CAF lazima watapewa adhabu nyingne?? Kumbe nimeamini washabiki wa yanga hawajui mpira Basi ingekuwa hivyo PSG 2017 wasiingingize timu uwanjani ili Barcelona apewe point 3 Na goli tatu ili afuzu PSG au hawajui mpira wewe Ndo unajua washauri wasiingingize timu uwanjani kwenye soka hasa mpira chochote kinawezekana
 
Utopolo ni Ndezi na mashabiki wao ni Ndezi.
Ni ama zao ama zetu,Kaizer anakufa goli zaidi ya nne kwa Mkapa,asietaka anywe Chibuku akalale
Simba nguvu moja.
Woyooooooooooooooo,,,!
Alisikika mlevi fulani wa Congo pale mitaa ya msimbazi
 
Hyo ni Sheria gani hao CAF lazima watapewa adhabu nyingne?? Kumbe nimeamini washabiki wa yanga hawajui mpira Basi ingekuwa hivyo PSG 2017 wasiingingize timu uwanjani ili Barcelona apewe point 3 Na goli tatu ili afuzu PSG au hawajui mpira wewe Ndo unajua washauri wasiingingize timu uwanjani kwenye soka hasa mpira chochote kinawezekana
Anaonyesha maana ya utopolo wakigoma wanatolewa, faini na kufungiwa juu
 
Kaizer Chiefs wasipoingiza timu Simba atapewa magoli matatu na pointi tatu, Kisha atatolewa
Nadhani umesahau yaliyoikuta Mtibwa kwenye CAF competitions. hakucheza mechi ya marudiano dhidi ya Santos ya Afrika Kusini katika kombe la Shirikisho, matokeo yote yakafutwa, Mtibwa akaondolewa mashindanoni, akafungiwa kushiriki kwa miaka mitatu, akaadhibiwa ailipe Santos gharama za maandalizi kiasi cha $1,500. Hiyo ilikuwa ni mwaka 2004
 
Kaizer Chiefs na wao ni waoga sana, yaani wanavyolalamika ni kama enzi zile timu za Tz zikiwa zinaenda kwa nchi za kiarabu, na huu uoga wao ndio utawapoteza na kuwaletea mhaho.
Mbinu ya mchezo ile mkuu
 
Utopolo ni Ndezi na mashabiki wao ni Ndezi.
Ni ama zao ama zetu,Kaizer anakufa goli zaidi ya nne kwa Mkapa,asietaka anywe Chibuku akalale
Simba nguvu moja.
Woyooooooooooooooo,,,!
SEMA TENA, RUDIA SIJASIKIA
 
Back
Top Bottom