Ninawaza kufungua Duka la Vinywaji

Na hela ya kupangisha ipo ndani ya hicho kiwango ulichokitaja?
Mm nafanya.....hyo budget yako ni ndogo kwa kile unachotaka kuwa nacho na tena uuze jumla na rejareja...
 
Nina passion kubwa ya kuwa mfanyabiashara japo naogopa kuangukia kichwa
Huwez kuanguka kaka .km kweli unania ya dhati kabisa


Ila discipline...discipline.... narudia tena discipline ndo msingi mkuu wa chochote kile

Usisite site mkuu ukiamua jambo lifanye ..usiogope utaanzia chini muhimu ni focus yako ...yan una vision gan kwenye hiyo biashara so ikiwezekana weka na target unayotaka kufika baada ya muda flan na hakikisha unapambana mpaka kufikia
 
Mkuu hiyo business inahitaji ujiandae kwelikweli, kwanza kreti tupu hapo lazima zikule pesa si chini ya milioni 2 au 3. maana kwa sasa kleti tupu ni 12,000 sasa piga bia (TBL na SBL) piga soda (coca na Pepsi) ukichukua mia mia maana yake upo kwenye milioni 5 kasoro huko. ukichukua mfano Bia ziwe 50 ukumbuke kuna TBL na SBL na ndani ya hizo kuna categories yaani safari ndogo na kubwa, castle lite, kili ndogo na kubwa, yaani nyinginyingi. Kwahiyo ukichukua chache unajikuta mteja mmoja akija kuchukua kili ndogo kleti 3 tayari ndio kamaliza utakuwa huna kili ndogo hadi uagize. Ni changamoto sana. Anza na mtaji angalau milioni 7 unaweza kufungua kwa kuanzia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…