Ningelikuwa Nape Nnauye ningekuwa nimejiuzulu

Ningelikuwa Nape Nnauye ningekuwa nimejiuzulu

Mhafidhina07

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2014
Posts
3,340
Reaction score
4,659
Salaam wanajenzi.

Natambua kuwa nchi yetu ni mwanachama wa Umoja wa Mataifa (UN), umoja wa kikanda (SADC na EAC) ambapo kwa pamoja wameridhia kuongoza kwa kutumia katiba za nchi zao ambazo zimedhibiti sheria za kikanda na kibara kama ilivyotanabaishwa katika mfululizo wa vifungu na sheria za kimataifa mfano uhuru wa habari, uhuru na haki za binadamu pamoja na uhuru wa asasi za kiraia na vyama siasa.

Mwanasiasa mkubwa ambaye anadhama ya cheo anaropoka hadharani kwenye kipindi karibu na uchaguzi mkuu na kuzua taharuki kwa raia,ni dhahiri kuwa amevunja na kuivua heshima ya serikali ya CCM pamoja na rais wake.

Si hivyo tu, pia Nape Nnauye ameiabisha na kuidhalilisha tume ya uchaguzi na watendaji wake, amedhalilisha mfumo mzima wa utawala/siasa.

Binafsi naona kuna ulazima wa kung'atuka kwenye nafasi aliyopo anaipaka tope taasisi na cheo cha waziri wa habari.

Nakumbusha.

PIA SOMA
- Kuelekea 2025 - Nape Nnauye: Matokeo ya kura inategemea nani anahesabu na nani anatangaza, ili mradi ukimaliza unasema Mungu nisamehe!
 
Jana katukana
Haitoshi akaja X katukana Tena kasema tumemsikia vibaya hatuna masikio sisi?
Amepata katerero usiku asubuhi anaomba msamaha.... Kwaniaba ya Wana jf sijakusamehe muheshimiwa mpumbavu
ni upuuuzi wake
 
Ukiacha kubebwa kwa Nape na mfumo bado ni bogus pia wa kuweza kuchanganua athari ya lolote analofanya ama kusema.

Kila siku nasema qualification pekee anayomiliki Nape ni jina la Nnauye, kinyume na hapo ni mweupe kabisa.

Tofauti pekee ya Nape na Mwijaku katika kuropoka ni kuwa mmoja ana back up ya system.
 
Ukiacha kubebwa kwa Nape na mfumo bado ni bogus pia wa kuweza kuchanganua athari ya lolote analofanya ama kusema.

Kila siku nasema qualification pekee anayomiliki Nape ni jina la Nnauye, kinyume na hapo ni mweupe kabisa.

Tofauti pekee ya Nape na Mwijaku katika kuropoka ni kuwa mmoja ana back up ya system.
anaonekana hajielewi kbs
 
yeye ndiye wa kwanza kutoa kauli tata toka nchi hii na serikali kwa ujumla zikae madarakani?

"we are the image of our........." by Chinuamulog Albert Achebe in Things Fall Apart
 
Alichokisema ni kweli...
Inabidi ajengewe sanamu kwa kusema ukweli, amefanya kosa gani mpaka ajiuzulu.
 
Alafu yeye anasema eti asamehewe ulikua ni utani tuu kama alivyo fanya buana ndumba rooooo😄😄
 
Basi na Samia ajiuzulu maana na yeye aliwahi kusema kuwa kura hata uwapigie wapinzani, zinakuwa za CCM.
 
Back
Top Bottom