Ningependa kufahamu kama kuna hatimiliki ya Kuku wa Makange

Ningependa kufahamu kama kuna hatimiliki ya Kuku wa Makange

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
KUKU "MAKANGE RECIPE" (MAKANGE CHICKEN) IRINGA

Wakati ni wa chakula cha mchana na niko katika mgahawa mmoja katikati ya mji wa Iringa jina lake Coffee Shop.

Mwanangu anatoa "order," anaomba kuku wake atengenezwe "Makange."
Mimi ikawa nimesikia kama kasema "makande."

Nimesikia hivyo kwa kuwa tuko sehemu ya maakuli na makande ni aina ya chakula.

Ndani ya nafsi yangu ikawa nimeguna kimoyomoyo nikijiuliza, "Huyu bwana toka lini kaanza kula makande?"

Mbali ya kujiuliza kama kuna hoteli wana makande kwenye "menu.''
Nilipomuuliza akaniambia yeye ameagiza, "Kuku Makange."

Ndipo haraka ikanijia kuwa kuku wa marehemu Robert Makange amewasili Iringa.

Nikamuuliza huyu mwenyeji wangu kama anamjua Robert Makange.
Hakuwa anamjua.

Nataka kumweleza nani Robert Makange yeye tayari keshawasiliana na Mwalimu Google namsikia ananisomea, "Robert Makange muasisi wa Kuku wa Makange..."

Kidogo sikupenda.

Yaani Robert Makange anatambulishwa na Prof. Google kwa kuku wake watamu na si kwa kuwa alipigania uhuru wa Tanganyika?

Ningependa kufahamu kama kuna hati miliki ya Kuku wa Makange.

Picha ya kwanza ni Robert Makange mmoja wa wahariri wa gazeti la Mwafrika.

Picha ya chini ni ''Makange Chicken.''

1656350376985.png

1656350585825.png
 
Weka weka nyama basi sisi kizazi Cha digital tumjue
David...
Idd Faiz alikuwa mmoja wa viongozi wa chama walioanzisha TANU Press iliyokuwa katika njia panda ya Mtaa wa Mchikichi na Livingstone mjini Dar es Salaam.

TANU Press ndiyo ilikuwa ikichapisha na kusambaza jarida la TANU, Sauti ya TANU lililohaririwa na rais wa chama, Julius Nyerere, na baadaye kuchapisha Mwafrika chini ya uhariri wa Rashid Heri Baghdelleh na Robert Makange.

Kampuni hiyo ya kupiga chapa ilimilikiwa na Mwananchi Development Corporation TANU ilimteua Abdul Faraj kuiongoza kampuni hiyo.

Mwafrika,gazeti la kila wiki chini ya uhariri wa Heri Baghdelleh na Robert Makange, lilichapisha habari za Sheikh Suleiman Takadir katika ukurasa wa kwanza, likitangaza kufukuzwa kwake kutoka TANU kwa wino mzito, picha yake akiwa amevaa kanzu na kofia ya mkono akikodoa macho ikachapishwa gazetini.

Picha ya Sheikh Takadir iliwekwa pale ili wote wauone uso wa ''msaliti,'' anaetaka kuchelewesha uhuru kwa kutaka Waislam wapewe uthibitisho wa hali yao ya baadae kwa sababu ya mchango wao katika harakati za kudai uhuru.

Wakati wa mkasa wa Sheikh Takadir, Mwafrika lilikuwa likifaidi mauzo makubwa kwa sababu TANU ilisusia gazeti la Baraza gazeti la kila wiki la serikali. Baghdelleh na Makange walikuwa wamechapisha makala moja ambayo serikali iliiona ni ya uchochezi.

Baghdelleh na Makange walipatikana na hatia na kufungwa miezi sita gerezani.

TANU ililipa kisasi kwa kuwataka wananchi wasusie gazeti la Baraza.

Hakuna Mwafrika aliyenunua gazeti hilo na kwa ajili hii yake mauzo ya Mwafrika yalipanda sana, hivyo kuipa sakata ya Sheikh Takadir katika Mwafrika nafasi kubwa gazetini.

Baraza ilikuwa katika ukingo wa kufa kabisa kama isingelikuwa juhudi na mbinu za kidiplomasia za meneja wake, Page Jones na Meneja wa Tanganyika Standard, Nihill waliokwenda makao makuu ya TANU kusuluhisha baina ya gazeti hilo la serikali na TANU.

Nihill alifanya mazungumzo na makamu wa rais wa TANU, John Rupia; kaimu katibu mwenezi, Amos Kissenge; katibu wa TANU Youth League, Dr. Michael Lugazia; Dossa Aziz na Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya TANU Idd Faiz.

viongozi waandamizi wa TANU walitoa amri ya kusitisha ususiaji wa gazeti la Baraza.

Kwa kitendo hiki TANU ilikuwa imejieleza vyema na ilikuwa imeonyesha nguvu zake.

(Kutoka kitabu cha Abdul Sykes (1998)
Picha: Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam Bi. Kate Kamba akiwa ofisini kwake ameshika kitabu cha Abdul Sykes.View attachment 2275011
 
Hizi ndio history tunataka zifundishwa shuleni sio mambo ya Wazungu kuwa wagunduzi wa mwanzo nchini. Leo mpigania uhuru anajulikana kama KFC boy(Makange chicken)na google??



Kukuuuu [emoji239][emoji239][emoji239]
 
Back
Top Bottom