Nini cha kufanya unapogundua unatumika kwenye uhusiano?

Nini cha kufanya unapogundua unatumika kwenye uhusiano?

MAMESHO

JF-Expert Member
Joined
Jul 5, 2011
Posts
1,432
Reaction score
1,738
Habari za leo. Awali niliwahi kuandika uzi kuelezea dalili zinazojitokeza ili kujua kama unatumika kwenye uhusiano.

Baada ya kukaa na kuangalia uhusiano ulionao, na kuona zile dalili unaweza kujua kuwa ni eneo gani umeathirika zaidi.

Yapo mahusiano yanaweza kuathiri akili yako, yako yanaweza kuathiri hisia zako, yapo yanaweza kukuathiri kiafya kwa maana ya mwili wako na maeneo mengine mengi.

Lengo la wengi kutumia watu wengine ni ili kuweza kukidhi hitaji lao. Kwa mfano hitaji la kimapenzi, hitaji la fedha, fursa, au kukamilisha lengo lolote walilo nalo.

Wakati mwingine wanaotumia watu wanaweza kuwa na ugonjwa wa kisaikolojia hivyo kuathiri afya yako kupitia ukatili wanaoweza kufanya. Katika jambo hili hakuna jibu la moja kwa moja. Jambo la msingi ni kutambua ni eneo gani unalotumika, hapo unaweza kutambua njia sahihi ya kujikwamua.

Moja ya namna ambayo unaweza kuitumia ni kuzuia lengo la anayekutumia lisifanikiwe, ila utaweza kugundua pale tuu ambapo utakuwa umegundua unatumika eneo gani. Ikiwa mpo kwenye mahusiano ya kudumu na mhusika, kwa mfano ndoa, unaweza kufanya tathimini ya uamuzi unaoweza kuchukua ili uwe salama.

Ngoja nikupe mfano mmoja.

Miaka mitano iliyopita rafiki yangu mmoja alikuwa nafanya kazi serikalini inayojihusisha na ukusanyaji wa mapato katika ngazi ya wilaya. Yupo mfanya biashara mmoja ambaye kila sikukuu alikuwa akimletea zawadi mbali mbali. Zawadi za vinywaji na zawadi za kuwapa watoto. Lakini alikuwa na lengo.

Kampuni yake ipatiwe makadirio nafuu. Kupitia vizawadi vya hapa napele maamuzi mazuri yaliweza kufanyika juu yake. Na alifanikiwa kwa alichokuwa anakitaka kwa muda mrefu sana. Lakini pale mhusika alipokuja kubaini aliweza kuziba mianya yote ambayo mhusika anaitumia. Haya mambo yapo kwenye kila eneo la maisha. Muwe na siku njema.
 
Kwa uzoefu nilionao ukiona umeanza kutumika katika mahusiano unatakiwa ufanye yafuatayo mapema before time it’s too late Ukaumia zaidi

1.Hatua ya kwanza anza kujitoa taratibu kwenye hayo mahusiano kimya kimya

2.hatua ya pili tafuta mpenzi mwingine taratibu na uanze kuamisha majeshi taratibu

3.hatua ya tatu hamisha hisia na moyo wako kwa mpenzi mpya na anza kumsifia mpenzi mpya

4.hatua ya nne punguza mawasiliano taratibu na uanze kujitenga na huyu mpenzi polepole

5.hatua ya tano anza kukimbiaa mitego yake aliyoitega mwisho wa siku usije ukaumia hapa nina usimtafute mpka yeye akutafuta

6.anza kumzungumzia vibaya kwa watu ikiwezekana muite mchawii

7.ukifanikiwa hatua zote Sita hatua ya mwisho anza kumpotezeaa mdogo mdogo
 
Ukiona furaha yako inategemea mpenzi wako afanye Jambo ndo ufurahi
Jua unatumika.

Ukiona mambo yake mengi ya kimaisha huyajui zaid ya nisaidie fedha nmekopa cement.
Jua unatumika.

Ukiona una mpenzi wako na mko kwenye mahusiano na akapata ujauzito na hujapiga una miezi 3-5 ulikuwa Safari.
Jua umetumika mbaka batani zimefubaa maneno.
Wanawake niwatakie jumatatu njema.
 
Kwa uzoefu nilionao ukiona umeanza kutumika katika mahusiano unatakiwa ufanye yafuatayo mapema before time it’s too late Ukaumia zaidi

1.Hatua ya kwanza anza kujitoa taratibu kwenye hayo mahusiano kimya kimya

2.hatua ya pili tafuta mpenzi mwingine taratibu na uanze kuamisha majeshi taratibu

3.hatua ya tatu hamisha hisia na moyo wako kwa mpenzi mpya na anza kumsifia mpenzi mpya

4.hatua ya nne punguza mawasiliano taratibu na uanze kujitenga na huyu mpenzi polepole

5.hatua ya tano anza kukimbiaa mitego yake aliyoitega mwisho wa siku usije ukaumia hapa nina usimtafute mpka yeye akutafuta

6.anza kumzungumzia vibaya kwa watu ikiwezekana muite mchawii

7.ukifanikiwa hatua zote Sita hatua ya mwisho anza kumpotezeaa mdogo mdogo
Mmh hiyo namba sita kiboko. Hivi ukihamisha majeshi je utakuwa na uhakika na unakoamia? Isijekuwa unahamia kambi ya adui?
 
Mmh hiyo namba sita kiboko. Hivi ukihamisha majeshi je utakuwa na uhakika na unakoamia? Isijekuwa unahamia kambi ya adui?

Lengo la kuhamisha majeshi mkuu ni kupunguza maumivu yanayoweza kujitokeza pindi Kamba itapokatika utakuwa umeshajianda
 
Haya mahusiano yalinisumbua sana.
nimpenda sana mdada mmoja kwa lengo niwe nae yaan mke,maana sikutaka macho kufikiria wengine.

Nilimpa kila anachokiitaji na mpaka kodi nilitoa,ada ya shule,simu,computer na mambo mengine ya msingi nikamnunulia.

alipogundua udhaifu wangu nampenda sana akaanza vituko,nilitamani kumuacha lakini maneno ya waenga "nitapenda wangap" yalinipoteza.nikasema maybe atabadili lakn wapi...

nilitumia njia zote za kutaka kumuacha nilifel,naweza kukaa wiki moja nakomaa bila kumtafuta lakini mwisho wa siku namtafuta,...

siku moja nilimwambia kitu akanigomea,siku iliofuata akanipiga mzinga nimpe kiasi fulan cha pesa.nikawaza hivi jana tu kanigomea mimi leo anataka pesa yangu.nikasema hapana huyu hupo kimasilahi.nikawaza saaa nafanya na nini ndo hvyo siwezi kumuacha.

niliamua kutompa pesa zangu anapokuwa na shida na kila anaponiomba nimwambie sina tena naongea kwa huzini why nimeshindwa kumsaidia.

pita pita nikaanza mahusiano mapya,nikawa busy na demu mpya akanifanya kabisa nimsahau hata kumtumia demu wa zamani salamu,mwisho wa siku akapotea akilini kabisa,bila kutumia nguvu

kumbe dawa ilikuwa tu demu mwingine
 
Kiukweli Wanaume wengi Sana tunatumika.

1. Unaingia mahusiano na singo Mother, anakutumia kumlea yeye na mwanae.
Unalipa Kodi, Ada, chakula,matibabu n.k
Hapo Unatumika

2. Zero IQ unaingia mahusiano na denti wa chuo,
Wanakutumia wapate uhakika wa KIEPE YAI kila siku.
Hapo unatumika.[emoji1]

Kikubwa sio kulalamika, unatakiwa kujua lengo la mahusiano ulokuepo na kuchukua hatua.

Ila Ukiangalia upande wa pili wa shillingi,
SISI WANAUME NDO TUNAONGOZA KWA KUWATUMIA wale TUNAOINGIA NAO KWENYE MAHUSIANO (wanawake).

Unamtongoza Mdada kwasababu umemuona ana chura,

LENGO lako umtumie tu kukata kiu yako (umchakate).
 
Kiukweli Wanaume wengi Sana tunatumika.

1. Unaingia mahusiano na singo Mother, anakutumia kumlea yeye na mwanae.
Unalipa Kodi, Ada, chakula,matibabu n.k
Hapo Unatumika

2. Zero IQ unaingia mahusiano na denti wa chuo,
Wanakutumia wapate uhakika wa KIEPE YAI kila siku.
Hapo unatumika.[emoji1]

Kikubwa sio kulalamika, unatakiwa kujua lengo la mahusiano ulokuepo na kuchukua hatua.

Ila Ukiangalia upande wa pili wa shillingi,
SISI WANAUME NDO TUNAONGOZA KWA KUWATUMIA wale TUNAOINGIA NAO KWENYE MAHUSIANO (wanawake).

Unamtongoza Mdada kwasababu umemuona ana chura,

LENGO lako umtumie tu kukata kiu yako (umchakate).
Natumika huku nikitumia Papuchi yake tramuu
 
Back
Top Bottom