Nini chanzo cha shida hii kwa watoto wachanga? Madaktari piteni hapa

Nini chanzo cha shida hii kwa watoto wachanga? Madaktari piteni hapa

nosimo

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2015
Posts
247
Reaction score
50
Habari,

Ni kwanini watoto wanazaliwa na kichwa kikubwa kupata kiasi (wanaita kichwa kukaa maji) na mdomo wazi hawa wanakuwa wamepasuka kuanzia puani hadi mdomini hawawezi kufunga mdomo jamani, pia ugonjwa wa mgongo wazi Jana ndo nimeona StarTV wameachia kiasi kati katikati pale kwenye mkia,tusaidieni dada zenu.

Tule nini tufanye nini tusiwazalie wajomba wako hivi.

Tafadhali tiririkeni
 
mbona hamnipi elimu doctors wa JF njooni
 
Hiyo ya mtoto kuwa na kichwa kikubwa kupita kiasi na ikathibitika kuna maji, kitaalamu inaitwa hydrocephalus, hii ni kutokana na blockage ya kimiminika cha uti wa mgongo au Cerebral Spinal Fluid (CSF) kutoka kwenye brain hali inayopelekea maji haya kujaa katika membrane ya Cerebral layers.

Matatizo mengine yaliyobakia ya mdomo kutofunga kitaalamu inaitwa Cleft lip palet na kuwa na tundu mgongoni tunaita kitaalamu Spinal bifida ni matatizo ya kuzaliwa nayo mtoto yaani Congenital anomalies au malformations.

Hali hiyo mara nyingi huwa Idiopathic yaani hakuna sababu au kisababishi kinachoelekea kupata hali hiyo kinachojulikana.


Pia imethibitika mama mjamzito mwenye tatizo la kifafa, Epilepsy na ambaye anatumia dawa za Kifafa kama Phenytoin na the like kuna uwezekano mkubwa wa kuzaa mtoto mwenye matatizo tajwa hapo juu ukitoa tatizo la Kichwa kikubwa, Hydrocephalus.


Naamini kuna wataalamu zaidi huku watakuja kuongezea au kurekebisha pale nitakapokuwa nimekosea.
 
Back
Top Bottom