Nini hasa kusudi la kuishi?

Nini hasa kusudi la kuishi?

Manyanza

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2010
Posts
16,464
Reaction score
35,629
Maisha ni safari ndefu yenye kila aina ya changamoto, na hakuna mwanadamu yeyote azaliwaye kwenye sura ya dunia hii bila kuzipitia. Changamoto huja kwa nyuso tofauti-tofauti kwa kila mmoja, na kamwe haziwezi kufanana wala kuwa na uzito wa aina ile ile kwa watu wote wanaozipitia.

Ikitegemea na hali, eneo, nyutu za watu, na mambo yanayowazunguka, sikuzote changamoto huwepo ndani ya maisha ya mtu kumsukuma awe na nia ya kupambana ili kujitoa ndani ya hizo na kuwa na maisha bora.

Tunaambiwa elimu ndiyo ufunguo wa maisha bora lakini hata watu wenye elimu ya juu bado huhangaishwa na matatizo mengi yanayowakosesha amani. Kila mtu mmoja mmoja anatamani kufikia sehemu nzuri maishani kiasi kwamba hata wale waliozifikia sehemu hizo bado wanakuwa hawaridhiki.

Ni tamaa yetu sote kuishi maisha yenye kuridhisha, lakini mivurugo ya maisha sikuzote huturudisha nyuma. Iwe ni kwa matajiri, au wenye hali za chini kiuchumi.

Kwa sababu ndivyo ambavyo sisi sote tumezaliwa na kukuta hali zikiwa namna hiyo tokea mwanaume wa kwanza alipoamua kumtandika ndugu yake mpaka akafa, imetubidi tuyaishi maisha kwa namna ambavyo yametutaka tuyaishi. Usione mtu anafanya jambo fulani ambalo linapingana na uasili wa kufanya mambo ukadhani hafai. La.

Ni kwamba maisha ndiyo yamemfanya akaona kufanya jambo hilo kuwa sahihi. Analazimika kuishi kwa njia hiyo aidha kwa kupenda ama kusukumwa tu, maadamu aishi.

Hivyo kamwe huwezi kuhukumu maisha ya mtu kwa kumtazama tu bila kujua kiundani ni mambo yapi yaliyopelekea mpaka akafikia hatua za kuishi namna aishivyo. Kujenga taswira nzuri mbele ya jamii ni jambo la muhimu, lakini maisha yanapokulazimu kuishi kwa namna ambayo jamii itayahukumu vibaya, unachopaswa kufanya ni kula ugali wako na kuvuta shuka kulala, ili kesho uamkie mambo mengine na kuendelea kuishi. Basi!

Naandika haya mimi siyo chizi. Mimi siyo mtunga mashairi wala nini. Ila nimeona tu nijaribu kuzama zaidi ndani ya vina virefu visivyoelezeka kwa mapana sana kuhusu neno hili: maisha. Maisha hayawezi kufanana kwa kila mmoja. Hayawezi kuendana. Hayawezi kuingiliana kwa asilimia zote na kumfanya mtu wa hali ya chini aweze kuwa kama kiongozi wa nchi hii kwa ufanisi aupatao kutokana na jasho la huyo huyo "mtu wa hali ya chini."

Kila mtu ana kisa chake mwenyewe cha maisha. Alipo fulani sasa hakufika kwa muujiza, kuna sehemu amepita. Unaweza ukashangaa kwa nini watu wanahangaika sana kufatilia maisha ya watu maarufu zaidi. Ni kwa sababu tayari wameshajijengea umaarufu.

Hawakuzaliwa nao, waliutafuta, wakaupata. Wanaoendelea kuwafuatilia tu wanaishia kuwa watu wa kutamani. Hata hao watu maarufu wamepitia changamoto nyingi maishani, lakini hakuna mtu hata mmoja aliyejisumbua kuzijua wala kuziulizia mpaka walipokuja kupata huo ufanisi na kuzigeuza changamoto hizo ziwe kitu cha kuwatia moyo wengine kupambana zaidi.

Hutajali saana kufatilia maisha ya ndani zaidi ya mwanamke abebaye sinia la karanga kichwani, akiwa amebeba mtoto mdogo mgongoni, sura yake ikiwa imechoka, akiziuza karanga hizo stendi ya mabasi na jua likiwa kali sana. Tayari tu una kitu ndani yako kinachojua kwamba ana changamoto zake, kama watu wote, kwa hiyo nawe utabaki kutulia na za kwako tu, si ndiyo? Angalau nunua hata hizo karanga basi, hata ya mia tu.

Itampa faraja kuona kwamba hata kesho anaweza kujikwamua na kuendelea kupambana kuzivuka changamoto zake ili ajenge maisha mazuri kwa kiwango ambacho Mungu atambarikia kukipata.

Sina lengo la kuandika mahubiri ili muanze kutenga sura na mistari. Ni kwamba tu nimeangalia hata maisha yangu mwenyewe na kugundua kwamba kuna changamoto nyingi zilizo ngumu maishani mwa mwanadamu, na japo kwa wengi zinatofautiana, mapenzi ni suala lizushalo changamoto kwa KILA MTU.

Kubali, kataa. Hakuna mtu apitaye upeo wa ujana bila kukumbwa na changamoto za jambo hilo. Kwa nini?

Kwa sababu hakuna lengo lolote la kuishi isipokuwa upendo. Ni kitu cha kiasili. Kila mtu anacho. Nazungumzia upendo wote, iwe ni wa kindugu, kirafiki, kishkaji, kihuni, vyovyote vile, ni lazima tu kuwe na changamoto nyingi sana. Sasa inapofikia kwenye ule upendo wa kijinsia ndiyo kabisaa! Watu mpaka wanauana kwa sababu ya kuumizwa na mapenzi.

Lakini kwa jinsi ambavyo mambo yamekuwa kufikia kipindi hiki, imeshaonekana kuwa jambo la kawaida sana kwa mapenzi kuwa kitu chenye kuumiza badala ya kutakiwa KUBAKI kuwa kitu chenye kuridhisha. Na kama nilivyosema mwanzoni, kwa sababu tumezaliwa na kuyakuta namna hiyo, basi ndiyo tunaendelea kuyaishi namna hiyo hiyo tu. Lakini kuyaishi namna hiyo hiyo tu si jambo linalofaa.

Ni muhimu kuishi kwa kusudi, na imenichukua visa vingi vilivyotokea katika maisha yangu mpaka kufikia sasa kutambua kwamba mapenzi ya kujifurahisha tu hayana faida yoyote. Yanapaswa kuwa na lengo.

Lakini kwa wengi, hata MIMI, hutuchukua muda mrefu mpaka kuja kumpata mtu anayeweza kukufanya ulitamani sana lengo hilo, haijalishi ni changamoto za aina gani utakazopitia, maadamu akiwa na wewe, unajua yote unaweza kuyashinda.

Credit: Elton Tonny
 
Maisha ni season hivo inategemeana umeamua binafsi kucheza kama nani!
Ndio maana wapo walio amua kucheza kama👇
Jambazi
Tapeli
Daktari
Fisadi
Askari
Mkulima
Mwizi
Mwalimu
Mchawi
Mganga
Nazaidi yahapo.
Hayo maisha yataendelea kua season katika maisha yako hadi pale utakapo amua kuishi maisha mengine kabisa ukiwa hai kwawakati huu au hapo utakapo zaliwa upya.
 
  • Tuna nafasi moja tu hapa duniani, nayo ni kuishi mpaka pale utakapo twaliwa kwenye hii ardhi.​
  • Ukiamua kuishi kwa furaha ni wewe tu, na ukiamua kujitesa ni wewe tu.​
  • Rizika na kipato chako na usitamani vya watu; kama pato lako ni 3000 kwa siku, ukirizika nalo utaishi kwa furaha; ila ukitaka kuishi kwa kujiringanisha, utaingia kwenye mambo mabaya, kuumia nafsi, pamoja na kupata matatizo ya magonjwa ya akili n.k​
  • Ishi kwenye dunia kama uko mwenyewe ndani ya bustani ya eden​
 
Maisha ni season hivo inategemeana umeamua binafsi kucheza kama nani!
Ndio maana wapo walio amua kucheza kama👇
Jambazi
Tapeli
Daktari
Fisadi
Askari
Mkulima
Mwizi
Mwalimu
Mchawi
Mganga
Nazaidi yahapo.
Hayo maisha yataendelea kua season katika maisha yako hadi pale utakapo amua kuishi maisha mengine kabisa ukiwa hai kwawakati huu au hapo utakapo zaliwa upya.
Dunia uwanja wa fujo - Kezilahabi
 
Maisha ni ufala sana aisee, unaweza ukawa mwema ila maisha yakakufuck
Kwa kweli kuwa nice guy na kuwa selfless kumechangaia pakubwa maisha kunila kavu kavu,

kuna shortcuts unaziona za kukuondolea utu na integrity zinakuja Ila unaona hapana Ila wengine wanapiga na kutoboa.

Kuna time kuna vitu unafanya unafanikisha vitu flani, mwingine anajaribu anaangukia pua ... Vice verse is true 😁😁😁

Yes kila siku tunapambana kujua maana ya maisha lakini dhidi ninavyowaona watu wanafariki na mipango na dreams zao ndivyo najua kuwa maisha ni sasa. Maisha yako ni zao la maamuzi unayoyachukua kwa maana yenyewe ndio yanaruhusu na kuzuia vitu vyote vinavyokutokea japo vingine vichache hututokea nje ya uwezo wetu..

Maisha ni actions za kila siku
Maisha ni mjumuisho wa makosa na vitu sahihi tunayoyafanya kila siku

Maisha ni historia ambayo tunaitengeneza kila siku kwa vitu nilivyoainisha hapo juu

Hutokaa uyaelewe maisha kwani jana ishapita, Leo ndio hiyo tunaingalia na kesho hatuijui..
 
Mi kusudi langu la kuishi ni kula mishangazi na hawa watu wa makamo...

Maana kwa sasa imekua too much kila nikigusa imoooo...
Hapa nawaza ni jinsi gani tamkwepa huyu mke wa mtu hiyo jumapili aiseee....

Bado mishangazi huyu atasema niende huku huyu atasema niende kule.
Kila napo jaribu kukaa mbali na hayo maisha naona kabisa siwezi..

Sasa nimejua kumbe kusudi la maisha yangu ni kuwapa raha hawa watu....
 
Maisha ni safari ndefu yenye kila aina ya changamoto, na hakuna mwanadamu yeyote azaliwaye kwenye sura ya dunia hii bila kuzipitia. Changamoto huja kwa nyuso tofauti-tofauti kwa kila mmoja, na kamwe haziwezi kufanana wala kuwa na uzito wa aina ile ile kwa watu wote wanaozipitia. Ikitegemea na hali, eneo, nyutu za watu, na mambo yanayowazunguka, sikuzote changamoto huwepo ndani ya maisha ya mtu kumsukuma awe na nia ya kupambana ili kujitoa ndani ya hizo na kuwa na maisha bora.

Tunaambiwa elimu ndiyo ufunguo wa maisha bora lakini hata watu wenye elimu ya juu bado huhangaishwa na matatizo mengi yanayowakosesha amani. Kila mtu mmoja mmoja anatamani kufikia sehemu nzuri maishani kiasi kwamba hata wale waliozifikia sehemu hizo bado wanakuwa hawaridhiki. Ni tamaa yetu sote kuishi maisha yenye kuridhisha, lakini mivurugo ya maisha sikuzote huturudisha nyuma. Iwe ni kwa matajiri, au wenye hali za chini kiuchumi.

Kwa sababu ndivyo ambavyo sisi sote tumezaliwa na kukuta hali zikiwa namna hiyo tokea mwanaume wa kwanza alipoamua kumtandika ndugu yake mpaka akafa, imetubidi tuyaishi maisha kwa namna ambavyo yametutaka tuyaishi. Usione mtu anafanya jambo fulani ambalo linapingana na uasili wa kufanya mambo ukadhani hafai. La. Ni kwamba maisha ndiyo yamemfanya akaona kufanya jambo hilo kuwa sahihi. Analazimika kuishi kwa njia hiyo aidha kwa kupenda ama kusukumwa tu, maadamu aishi.

Hivyo kamwe huwezi kuhukumu maisha ya mtu kwa kumtazama tu bila kujua kiundani ni mambo yapi yaliyopelekea mpaka akafikia hatua za kuishi namna aishivyo. Kujenga taswira nzuri mbele ya jamii ni jambo la muhimu, lakini maisha yanapokulazimu kuishi kwa namna ambayo jamii itayahukumu vibaya, unachopaswa kufanya ni kula ugali wako na kuvuta shuka kulala, ili kesho uamkie mambo mengine na kuendelea kuishi. Basi!

Naandika haya mimi siyo chizi. Mimi siyo mtunga mashairi wala nini. Ila nimeona tu nijaribu kuzama zaidi ndani ya vina virefu visivyoelezeka kwa mapana sana kuhusu neno hili: maisha. Maisha hayawezi kufanana kwa kila mmoja. Hayawezi kuendana. Hayawezi kuingiliana kwa asilimia zote na kumfanya mtu wa hali ya chini aweze kuwa kama kiongozi wa nchi hii kwa ufanisi aupatao kutokana na jasho la huyo huyo "mtu wa hali ya chini."

Kila mtu ana kisa chake mwenyewe cha maisha. Alipo fulani sasa hakufika kwa muujiza, kuna sehemu amepita. Unaweza ukashangaa kwa nini watu wanahangaika sana kufatilia maisha ya watu maarufu zaidi. Ni kwa sababu tayari wameshajijengea umaarufu. Hawakuzaliwa nao, waliutafuta, wakaupata. Wanaoendelea kuwafuatilia tu wanaishia kuwa watu wa kutamani. Hata hao watu maarufu wamepitia changamoto nyingi maishani, lakini hakuna mtu hata mmoja aliyejisumbua kuzijua wala kuziulizia mpaka walipokuja kupata huo ufanisi na kuzigeuza changamoto hizo ziwe kitu cha kuwatia moyo wengine kupambana zaidi.

Hutajali saana kufatilia maisha ya ndani zaidi ya mwanamke abebaye sinia la karanga kichwani, akiwa amebeba mtoto mdogo mgongoni, sura yake ikiwa imechoka, akiziuza karanga hizo stendi ya mabasi na jua likiwa kali sana. Tayari tu una kitu ndani yako kinachojua kwamba ana changamoto zake, kama watu wote, kwa hiyo nawe utabaki kutulia na za kwako tu, si ndiyo? Angalau nunua hata hizo karanga basi, hata ya mia tu. Itampa faraja kuona kwamba hata kesho anaweza kujikwamua na kuendelea kupambana kuzivuka changamoto zake ili ajenge maisha mazuri kwa kiwango ambacho Mungu atambarikia kukipata.

Sina lengo la kuandika mahubiri ili muanze kutenga sura na mistari. Ni kwamba tu nimeangalia hata maisha yangu mwenyewe na kugundua kwamba kuna changamoto nyingi zilizo ngumu maishani mwa mwanadamu, na japo kwa wengi zinatofautiana, mapenzi ni suala lizushalo changamoto kwa KILA MTU. Kubali, kataa. Hakuna mtu apitaye upeo wa ujana bila kukumbwa na changamoto za jambo hilo. Kwa nini?

Kwa sababu hakuna lengo lolote la kuishi isipokuwa upendo. Ni kitu cha kiasili. Kila mtu anacho. Nazungumzia upendo wote, iwe ni wa kindugu, kirafiki, kishkaji, kihuni, vyovyote vile, ni lazima tu kuwe na changamoto nyingi sana. Sasa inapofikia kwenye ule upendo wa kijinsia ndiyo kabisaa! Watu mpaka wanauana kwa sababu ya kuumizwa na mapenzi.

Lakini kwa jinsi ambavyo mambo yamekuwa kufikia kipindi hiki, imeshaonekana kuwa jambo la kawaida sana kwa mapenzi kuwa kitu chenye kuumiza badala ya kutakiwa KUBAKI kuwa kitu chenye kuridhisha. Na kama nilivyosema mwanzoni, kwa sababu tumezaliwa na kuyakuta namna hiyo, basi ndiyo tunaendelea kuyaishi namna hiyo hiyo tu. Lakini kuyaishi namna hiyo hiyo tu si jambo linalofaa.

Ni muhimu kuishi kwa kusudi, na imenichukua visa vingi vilivyotokea katika maisha yangu mpaka kufikia sasa kutambua kwamba mapenzi ya kujifurahisha tu hayana faida yoyote. Yanapaswa kuwa na lengo. Lakini kwa wengi, hata MIMI, hutuchukua muda mrefu mpaka kuja kumpata mtu anayeweza kukufanya ulitamani sana lengo hilo, haijalishi ni changamoto za aina gani utakazopitia, maadamu akiwa na wewe, unajua yote unaweza kuyashinda.

Credit: Elton Tonny
Ni kutawaliwa, kuchezewa na uhai wetu kufujwa na wanasiasa
 
Mi kusudi langu la kuishi ni kula mishangazi na hawa watu wa makamo...

Maana kwa sasa imekua too much kila nikigusa imoooo...
Hapa nawaza ni jinsi gani tamkwepa huyu mke wa mtu hiyo jumapili aiseee....

Bado mishangazi huyu atasema niende huku huyu atasema niende kule.
Kila napo jaribu kukaa mbali na hayo maisha naona kabisa siwezi..

Sasa nimejua kumbe kusudi la maisha yangu ni kuwapa raha hawa watu....
Chizi wewe 😂
 
LENGO LA KUISHI DUNIANI NI

1)Aliyetuumba Mungu kwa tunaomwanini Mungu na kuamini tumeumbwa na Mungu na hii duniani na ulimwengu mzima na vyote vikivyomo ni mali ya Mungu.
Mungu ametukabidhi dhamana ya kutunza mazingira yetu na kuyatawala mazingira yetu na kujitunza
2)Ametupa akili pia ametupa vipaji talanta ujuzi mbali mbali tuutumie vyema kuzalisha kuongezeka kustawi kisaidia wengine kupendana sisi kwa sisi na kumpenda Mungu na kumpendeza Mungu
3)Ametupa user manual au muongozo wa namna ya kuishi duniani NENO lake sheria yake mafundisho yake tuyafuate
4)pia ametupa maonyo tujue kuwa TUTAKUFA baada ya kifo ni peponi au jehanamu ya moto,kulingana na matendo yetu ya hapa duniani
5)muda mfupi tunaoishi duniani ni mtihani wa kuishi maisha mema,mana hatujui kesho yetu ,tutajibu hesabu ya matendo yetu hapa duniani,tutende yaliyo haki,tusijihangaishe sana na kesho mana kesho yetu ni siri,tusiwe na tamaa,tusijilimbikizie tisiwe wabinafsi,tusaidie wanyonge familia zetu,jamii yetu,tushike sheria za Mungu,sala,toba tuishi maisha ya HAKI na tuwe msaada kwa wengine .

UFUPISHO
Ni rahisi kujua kusudi la kuishi kama ukijua chanzo cha maisha ni Mungu.
Ukijua chanzo cha uhai wako ni Mungu basi utaishi kwa kusudi la Mungu.
1)TUPENDANE SISI KWA SISI BILA KUBAGUANA BILA KUHUKUMIANA
2)TUMPENDE MUNGU MUUMBA WETU.
 
Mi kusudi langu la kuishi ni kula mishangazi na hawa watu wa makamo...

Maana kwa sasa imekua too much kila nikigusa imoooo...
Hapa nawaza ni jinsi gani tamkwepa huyu mke wa mtu hiyo jumapili aiseee....

Bado mishangazi huyu atasema niende huku huyu atasema niende kule.
Kila napo jaribu kukaa mbali na hayo maisha naona kabisa siwezi..

Sasa nimejua kumbe kusudi la maisha yangu ni kuwapa raha hawa watu....
Ujana usikutapeli aisee na usiishi kama Ted Jorgensen
 
Mi kusudi langu la kuishi ni kula mishangazi na hawa watu wa makamo...

Maana kwa sasa imekua too much kila nikigusa imoooo...
Hapa nawaza ni jinsi gani tamkwepa huyu mke wa mtu hiyo jumapili aiseee....

Bado mishangazi huyu atasema niende huku huyu atasema niende kule.
Kila napo jaribu kukaa mbali na hayo maisha naona kabisa siwezi..

Sasa nimejua kumbe kusudi la maisha yangu ni kuwapa raha hawa watu...

Manyanza

JF-Expert Member​


AKIWA Kijana, alifanya tukio. Hakujuta. Na akasahau. Akaishi miaka 44 mingine. Ndipo akatokea mtu akamkumbusha kile alichokifanya. Akaumia. Akatamani asahihishe makosa yake. Hakupata fursa hiyo. Miaka mitatu baadaye akafariki dunia akiwa mwenye huzuni kubwa.

Zingatia, ujana ni tapeli mkubwa wa maisha. Ujana utakulaghai na kukufanya uone maisha ni hayohayo uliyonayo katika wakati uliopo. Ujana unaweza kukughilibu na kukusahaulisha ujio wa kesho. Ujana hufumba macho na huziba masikio. Si walisema ujana maji ya moto?

Ted Jorgensen, alipokuwa na umri wa miaka 17, alikutana na binti mrembo, Jacklyn Gise, aliyekuwa na umri wa miaka 16. Wakapendana. Wakaanza safari ya mapenzi. Jacklyn akanasa ujauzito.

Wakati Jacklyn anashika mimba, alikuwa mwanafunzi wa high school. Ted alikuwa mcheza sarakasi aliyekuwa na ndoto za kufanikiwa kwenye mchezo huo.

Januari 12, 1964, mtoto akazaliwa. Jeffrey ndilo jina walilompa. Jeffrey alipozaliwa, Ted alikuwa ameshatimiza umri wa miaka 18, Jacklyn miaka 17. Na sababu ya mtoto na malezi, ndoto za masomo zikayeyuka. Ted na Jacklyn wakafunga ndoa.

Maisha ya ndoa yakawa magumu. Ted alikuwa mlevi kupindukia. Mara arudi nyumbani alfajiri au asirudi kabisa. Ted alikuwa na kipato kidogo lakini hakukitumia kulea familia, bali starehe zake binafsi.

Baada ya miezi 17 ya ndoa, Jacklyn akaomba talaka. Ted akakubali. Wakaachana. Jacklyn akarudi kwa wazazi wake. Miaka miwili baadaye, Jacklyn akapata mwanaume mwingine, Miguel Bezos. Wakafunga ndoa. Bezos akaomba kumuasili Jeffrey awe mwanaye kisheria. Ted akasaini nyaraka zote kuhalalisha mtoto wake atwaliwe na Bezos.

Mwaka 2012, mwandishi Brad Stone alipokuwa anakusanya taarifa ili aandike kitabu “The Everything Store” kilichohusu maisha ya bilionea mmiliki wa kampuni ya Amazon, Jeff Bezos, alimfikia Ted. Akamuuliza kama alikuwa na habari kuhusu mwanaye aliyezaa na Jacklyn mwaka 1964.

Ted akavuta kumbukumbu, kisha akajibu: “Nimekumbuka. Hivi yule mtoto bado yupo hai kweli?” Brad akamjibu: “Yupo hai. Ndio huyu bilionea mmiliki wa Amazon.” Ted akasikitika, lakini akakiri hakuwa baba bora kwa Jeffrey wala mume mzuri kwa Jacklyn.

Kuanzia hapo, Ted alianza kutafuta nafasi ya kuonana na mwanaye Jeffrey, angalau wazungumze, japo amtambue. Nafasi hiyo angeipata wapi?

Mwaka 2014, Ted aliumwa sana. Akaandika barua nyingi kwa Jeffrey, kumjulisha hali yake na kiu yake ya kumuona kabla hajaaga dunia. Hakupata majibu.

Hakuna ajuaye kama Jeffrey aliziona hizo barua na kumkaushia au hakuziona kabisa. Ila ni uhakika kuwa alitambua kuwa baba yake mzazi alikuwepo.

Mwaka 2015, Ted alifariki dunia bila kuonana na mwanaye wa damu, Jeffrey. Aliishia kumsoma na kumuona kwenye vyombo vya habari kama watu wengine.

Kuhusu maisha ya Ted; baada ya kuachana na Jacklyn, aliendelea na mitikasi yake ya kucheza sarakasi na ulevi. Miaka 10 baadaye, akagundua maisha aliyokuwa akiishi hayakuwa na kesho nzuri. Akaacha ulevi. Akafungua duka la kuuza baiskeli. Hiyo ndio ikawa kazi yake mpaka alipofariki dunia.

Ted baada ya kuachana na maisha ya ulevi, alimuoa mwanamke mwingine, jina lake Linda. Hakupata mtoto mwingine. Mkewe, Linda, alikuwa na watoto wanne.

Miaka miwili baada ya kifo cha Ted, taasisi ya utafiti wa mali na utajiri duniani ya Forbes, ilimtangaza Jeffrey kuwa tajiri namba moja duniani. Akimpita tajiri namba moja wa muda mrefu duniani, Bill Gates.

Kwa sasa, Jeffrey ana utajiri wa dola 183.6 billioni, ambazo ni sawa na Sh242.4 trillioni.

Jeffrey anatambua kuwa Ted ni baba yake, kwani cheti chake cha kuzaliwa na kumbukumbu zote za hospitali zinamtaja Ted ndiye baba yake.

Hiyo ni stori kuhusu tajiri namba moja duniani, Jeff Bezos na baba yake mzazi, Ted Jorgensen. Story kuhusu ujana na utapeli wake.

Ted angejua? Maskini hakujua. Alikufa akijuta. Angejua Jeff ndiye mwanaye wa pekee, angekubali kumwacha kwenye mikono ya baba mwingine? Angefunuliwa kuwa Jeff angekuwa tajiri namba moja duniani, unadhani angemtelekeza?

Hata hivyo usimlaumu sana Ted. Alitapeliwa na ujana. Siku zote elewa hili, ujana ni tapeli mkubwa mno kwenye safari ya maisha.
 
Maandiko yanasema tunaangamia ajili ya kukosa maarifa, hili ndo fumbo la mateso yetu ktk maisha.
 
Back
Top Bottom