Kwani Ulimwengu mbona hazungumzwi sana?!! Au kwa kuwa hafungi kama Samata?!! Naona kwenda Mazembe pia kulisaidia kupata exposure zaid katika soka la ushindani na la kibiashara. Alipata advantage km ya Ulimwengu ukifananisha na hawa wengine.
Vilabu vyetu bado sana kwenye kukuza kipaji cha mchezaji nje ya juhudi,bidii au nidhamu ya mchezaji husika.
Wangapi tumewapeleka majaribio ya soka nje?! Idadi bado ndogo ikichangiwa na hao mawakala ambao kimsingi sio wengi TZ. Kiufupi bado kuna changamoto nyingi sana kwa hao wachezaji na vilabu vyetu. Km kikosi cha kwanza timu/klabu kubwa waTz wanahesabika,ni wazi hatuna hazina ya kutosha kwenye vilabu vyetu. Na hata hao wanao anza,ukiangalia uwezo wao kutoka timu husika bado kwa kweli.
Spain na brazil,una beki tatu na beki mbili wazur kibao wanagombea namba moja,leo tz hilo bado ndoto. Akitoka mhusika,anayeingia ni kawaida tu.
Naskia Maximo ndio alikuja na kutoa elimu kuhusu vyakula kwa wachezaji,sasa kama vitu vya msingi kwenye vilabu vyao hawapati unategemea nin!? Tuwe na academies za kutosha,vijana wapikwe tokea wadogo kiufundi,misosi husika,nidhamu,bila shaka matunda tutayaona tu. Hawa wazee wengi wao jua lishazama