Akili Unazo!
JF-Expert Member
- Feb 18, 2009
- 3,930
- 4,912
Baada ya Hukumu ya Miaka miwili nini hatima ya Mkataba wa Lulu na Azam,,,,,..... Au
------
Chaneli ya Sinema Zetu inayopatikana katika Televisheni ya Azam, leo imetangaza rasmi uzinduzi wa Tamasha lake lakutoa Tuzo na mchango wa tasnia ya Bongo Movies maarufu 'Sinema Zetu International Film Festival' litakalofanyika kuanzia January Mosi, 2018 hadi February 28, 2018.
Katika Tamasha hilo pia kutakuwa na Shindano litalokusanya Filamu zaidi ya 150 kutoka Mikoa mbalimbali kama Morogoro, Mwanza, Dodoma ambapo jumla ya Mikoa nane.
Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Kiongozi Mkuu wa Tamasha hilo, Jacob Joseph amesema kuwa watazunguka Mikoa Sita kwa ajili ya kuzungumza na Wadau wa tasnia hiyo ikiwa sambamba na kutoa elimu yakutosha na kuweka uelewa juu ya Tamasha hilo.
Mshauri wa Tamasha hilo, Prof. Martin Mhando amesema kuwa Shindano hilo la Filamu katika Televisheni litakuwa na vipengele vitatu ambapo litahusisha Bongo Movies 'Filamu Kubwa', Filamu Fupi za dakika 45, pia Makala za Filamu nazo zitahusika.
Balozi wa Tamasha hilo, Elizabeth Michael 'Lulu' ameshukuru kupewa ubalozi katika Tamasha hilo ikizingatiwa kwamba yeye ni Msanii atakayebeba Nembo ya Taifa la Tanzania katika nchi jirani zitakazoshiriki Tamasha hilo kwa Ukanda wa Afrika Mashariki.
------
Chaneli ya Sinema Zetu inayopatikana katika Televisheni ya Azam, leo imetangaza rasmi uzinduzi wa Tamasha lake lakutoa Tuzo na mchango wa tasnia ya Bongo Movies maarufu 'Sinema Zetu International Film Festival' litakalofanyika kuanzia January Mosi, 2018 hadi February 28, 2018.
Katika Tamasha hilo pia kutakuwa na Shindano litalokusanya Filamu zaidi ya 150 kutoka Mikoa mbalimbali kama Morogoro, Mwanza, Dodoma ambapo jumla ya Mikoa nane.
Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Kiongozi Mkuu wa Tamasha hilo, Jacob Joseph amesema kuwa watazunguka Mikoa Sita kwa ajili ya kuzungumza na Wadau wa tasnia hiyo ikiwa sambamba na kutoa elimu yakutosha na kuweka uelewa juu ya Tamasha hilo.
Mshauri wa Tamasha hilo, Prof. Martin Mhando amesema kuwa Shindano hilo la Filamu katika Televisheni litakuwa na vipengele vitatu ambapo litahusisha Bongo Movies 'Filamu Kubwa', Filamu Fupi za dakika 45, pia Makala za Filamu nazo zitahusika.
Balozi wa Tamasha hilo, Elizabeth Michael 'Lulu' ameshukuru kupewa ubalozi katika Tamasha hilo ikizingatiwa kwamba yeye ni Msanii atakayebeba Nembo ya Taifa la Tanzania katika nchi jirani zitakazoshiriki Tamasha hilo kwa Ukanda wa Afrika Mashariki.