Nini Hatma ya Ukraine baada ya Mzozo na Urusi?

Nini Hatma ya Ukraine baada ya Mzozo na Urusi?

Doncho kun

Member
Joined
Jan 11, 2019
Posts
11
Reaction score
10
Sasa ni siku zaidi ya 50 ya kinachoitwa operation ya kijeshi inayofanywa na shirikisho la Urusi ambapo upande unaoshambuliwa (Ukraine) umejaribu kila namna kuzuia mashambulizi makali ikiwa ni pamoja na kuomba mataifa ya Magharibi kuiwekea vikwazo Urusi, kuharibu zana za kivita za Urusi na kulipiga jeshi la Urusi kwa kuingia uwanja wa mapigano.

Hadi sasa zimerekodiwa hasara kubwa kwa pande zote mbili, ambapo nchi hizo zimepoteza wanajeshi, miundombinu ya kijeshi na kirai, vifaa vya kijeshi na raia (kwa upande wa Ukraine) ambao ni nguvu kazi ya taifa.

Swali ni je nini hatima ya taifa la Ukraine kiuchumi na kisiasa baada ya vita hii ambayo kwa kiwango kikubwa imewaacha katika maumivu makubwa?

Je, nini kitarajiwe kutuliza maumivu hayo kutoka nchi za magharibi ambazo zinaonekana zikiunga mkono Ukraine? Je, kujiunga kwa Ukraine kwenye umoja wa ulaya (EU) kutasaidiaje kupooza maumivu hayo?
 
Zelensky kaonyesha kiburi Cha kijinga sanakwa kuingia vitani akijua uwezo wakushinda Vita Hana Bali kuwategemea NATO na EU wangelikua upande wake.

Matokeo yake wamemtenga kabaki mkiwa.
 
Zelensky kaonyesha kiburi Cha kijinga sanakwa kuingia vitani akijua uwezo wakushinda Vita Hana Bali kuwategemea NATO na EU wangelikua upande wake.

Matokeo yake wamemtenga kabaki mkiwa.
Vip uonavyo wewe hawa watampunguzia maumivu aliyoyapata baada ya mzozo huu?
 
Ukraine inaelekea kua Zimbabwe ya ulaya,

Huu mgogoro ungepata Raisi wa Ukraine asiye na mihemko na anayeamini na kuheshimu diplomasia na mazungumzo sidhan Kama wangefika uko.
Kabisa mkuu.

Simuungi mkono putin kwa alichofanya,ila ilikuwa ni bora zaidi ukraine awe na urafiki na urusi kwa sababu ndio jirani yake.

Zelensky amepoteza sana hata akisema leo hajiungi nato keshachelewa tayari.

Katika maisha ni bora ufala ambao utakuweka salama kuliko kiburi ambacho kitakuweka hatarini.
 
Sasa ni siku zaidi ya 50 ya kinachoitwa operation ya kijeshi inayofanywa na shirikisho la Urusi ambapo upande unaoshambuliwa (Ukraine) umejaribu kila namna kuzuia mashambulizi makali ikiwa ni pamoja na kuomba mataifa ya Magharibi kuiwekea vikwazo Urusi, kuharibu zana za kivita za Urusi na kulipiga jeshi la Urusi kwa kuingia uwanja wa mapigano.

Hadi sasa zimerekodiwa hasara kubwa kwa pande zote mbili, ambapo nchi hizo zimepoteza wanajeshi, miundombinu ya kijeshi na kirai, vifaa vya kijeshi na raia (kwa upande wa Ukraine) ambao ni nguvu kazi ya taifa.

Swali ni je nini hatima ya taifa la Ukraine kiuchumi na kisiasa baada ya vita hii ambayo kwa kiwango kikubwa imewaacha katika maumivu makubwa?

Je, nini kitarajiwe kutuliza maumivu hayo kutoka nchi za magharibi ambazo zinaonekana zikiunga mkono Ukraine? Je, kujiunga kwa Ukraine kwenye umoja wa ulaya (EU) kutasaidiaje kupooza maumivu hayo?
Hatima yake ni uharibifu wa mali, tazama jinsi miji ya Kharkiv, Mariupol, Odessa na miji mingine ilivyogeuka magofu.

Inauma ukitazama vile majengo yalivyokuwa vifusi, inasikitisha ukifikiri jinsi vile walevi wa Ukraine watakavyoteseka Clubs, Bar, Pubs zimevunjwa vunjwa zote, sijui watalewa wapi tena rafiki zangu
 
Sasa ni siku zaidi ya 50 ya kinachoitwa operation ya kijeshi inayofanywa na shirikisho la Urusi ambapo upande unaoshambuliwa (Ukraine) umejaribu kila namna kuzuia mashambulizi makali ikiwa ni pamoja na kuomba mataifa ya Magharibi kuiwekea vikwazo Urusi, kuharibu zana za kivita za Urusi na kulipiga jeshi la Urusi kwa kuingia uwanja wa mapigano.

Hadi sasa zimerekodiwa hasara kubwa kwa pande zote mbili, ambapo nchi hizo zimepoteza wanajeshi, miundombinu ya kijeshi na kirai, vifaa vya kijeshi na raia (kwa upande wa Ukraine) ambao ni nguvu kazi ya taifa.

Swali ni je nini hatima ya taifa la Ukraine kiuchumi na kisiasa baada ya vita hii ambayo kwa kiwango kikubwa imewaacha katika maumivu makubwa?

Je, nini kitarajiwe kutuliza maumivu hayo kutoka nchi za magharibi ambazo zinaonekana zikiunga mkono Ukraine? Je, kujiunga kwa Ukraine kwenye umoja wa ulaya (EU) kutasaidiaje kupooza maumivu hayo?
Ukraine itasalim amri kwa lazima na itakua koloni la urusi na urusi itaijenga upya ukraine! Utapata rais atayeiunga mkono urusi!
 
Zelensky kaonyesha kiburi Cha kijinga sanakwa kuingia vitani akijua uwezo wakushinda Vita Hana Bali kuwategemea NATO na EU wangelikua upande wake.

Matokeo yake wamemtenga kabaki mkiwa.
unaongea bila kujua kwanz huyo zele kwanza alipatikanaje? hjwez kuserve ila jins master wako anavokuamrisha. nahurumia tu wananchi wa kawaida ambao wamewekewa mtu aliyekuwa na kaz maalum nauyo mdio hio tumeona kaifanya. ppupet leader

Sent from my TECNO CF7 using JamiiForums mobile app
 
Joti wa Ukraine, yeye alijua NATO inaingiza Jeshi la umoja wa ulaya, ndo maana akaota pembe!nakoukweli ndo ulikuwa mpango wao mezani! ila wale wanaoitwa War Analyst wakasema tukiingia kama NATO tutakuwa tumeanzisha vita ngumu, Na Russia akasema atakayeingiza jeshi yeye ni adui wangu na makombo ya kwanza yataanzia pale kwa West Minister 10 Street na lingine Birmingham Castle wakaona duh huyu atafanya kweli! Wakala kona sasa Joti akaanza mbwembe na jamaa wakabadili Gia angani wakasema tunakuoa Aid assistance
 
Zelensky kaonyesha kiburi Cha kijinga sanakwa kuingia vitani akijua uwezo wakushinda Vita Hana Bali kuwategemea NATO na EU wangelikua upande wake.

Matokeo yake wamemtenga kabaki mkiwa.
Mkuu namna gani unasema Zelenski aliingia vitani? Kwanza nasikia mara kwa mara hakuna vita ni special opereation tu. Pili si operesheni ya Zelenski ni ya Putin. Ila swali la hekima au ujinga liko kweli!
Maana ni kjweli hekima kuanzisha mapigano ukishindwa kumaliza kwa ushindi hata baada ya siku 100?
 
Sio mkiwa, wamekodi majeshi (wadahi mamluki) kila Kona ya Dunia na kutuma siraha.
Nahisi wanazidiwa mbinu za kivita.
 
Uamuzi wa kujiunga au kutojiunga na NATO sio wa Zelenskyy, ni wa bunge la Ukraine.

Halafu lini Ukraine walisema wanataka kujiunga na NATO?
Kabisa mkuu.

Simuungi mkono putin kwa alichofanya,ila ilikuwa ni bora zaidi ukraine awe na urafiki na urusi kwa sababu ndio jirani yake.

Zelensky amepoteza sana hata akisema leo hajiungi nato keshachelewa tayari.

Katika maisha ni bora ufala ambao utakuweka salama kuliko kiburi ambacho kitakuweka hatarini.
 
Rais anayeunga mkono Urusi aliondolewa kwa maandamano wa raia mwaka 2014 baada ya kukataa kusaini mkataba wa biasharana EU. Wa-Ukraine wengi hawataki ukaribu na Urusi bali wanaona ukaribu na EU pamoja na US ndio wenye faida kubwa kwao.
Ukraine itasalim amri kwa lazima na itakua koloni la urusi na urusi itaijenga upya ukraine! Utapata rais atayeiunga mkono urusi!
 
Urusi yenyewe bado ina sehemu kubwa tu ambayo haijajengwa mpaka leo na iko nyuma kimaendeleo, Kwa upendo gani na hizo pesa za kuijenga Ukraine itazipata wapi??
Ukraine itasalim amri kwa lazima na itakua koloni la urusi na urusi itaijenga upya ukraine! Utapata rais atayeiunga mkono urusi!
 
Back
Top Bottom