kitaa_hustler
New Member
- Dec 31, 2024
- 1
- 2
Habari zenu wakuu, Nimekuwa nikijiuliza hili swali mara nyingi kutokana na hali ilivyo katika nchi yetu , kila mmoja wetu tokea siku ameanza kujitambua mapambano yamekuwa kutafuta uelewa ama fursa ambayo itaweza kumsaidia kuboresha maisha yake binafsi pamoja na ya watu wanaomzunguka, kupitia elimu kujifunza ujuzi mbalimbali na vinginevyo lakini kila sehemu imekua na changamoto mbalimbali ambazo kila mmoja wetu kapitia kwa namna moja ama nyingine. Tatizo kubwa la watu wengi limekuwa ni kulalamika pasipo kutoa suluhisho la nini kifanyike na ni mazingira gani yatengenezwe na kwa hatua zipi yatengenezwe ili kuweka mfumo ambao ni mzuri kwetu sote na kwa kizazi cha kesho,
Basi ni nini kifanyike?
Basi ni nini kifanyike?