Nini kifanyike kuwahamasisha Wanawake kushiriki katika sekta ya Sayansi?

Nini kifanyike kuwahamasisha Wanawake kushiriki katika sekta ya Sayansi?

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
378
Reaction score
766
Siku ya Kimataifa ya Wanawake na Wasichana katika Sayansi huadhimishwa Februari 11 kila Mwaka kuadhimisha mafanikio na michango ya Wanawake na Wasichana katika Sekta ya Sayansi, Teknolojia, Uhandisi, na Hisabati (STEM)

Siku hii inahamasisha Wanawake na Wasichana zaidi kufuata na kujiunga na taaluma za Sayansi na Teknolojia lengo likiwa ni kuvunja vizuizi na dhana potofu ambazo Kihistoria zimezuia Ushiriki wa Wanawake katika sekta hizi

Utafiti wa mwaka 2022 ulionesha kuwa mwanamke mmoja kati ya wawili walioko katika fani ya Sayansi wameripoti kukutana na unyanyasaji wa kijinsia kazini.

Licha ya upungufu wa ujuzi katika maeneo mengi ya kiteknolojia, wanawake bado wanachukua asilimia 28 tu ya wahitimu wa masomo ya Uhandisi na asilimia 40 ya wahitimu katika masomo ya sayansi ya kompyuta.

Chanzo: United Nations
 
Kwanza waanze na shule.
Wadau na serikali wakiina mtoto wa kike ni genius wampe scholarship ya maana hata kumpeleka shule za kishua hapa hapa bongo. Kwamfano mwaka juzi wanafunzi wa IST wametengeneza dones as a classroom assignment tu. Hawa wa kwetu mazingira Yao ya kujifynza yanawakost sana
 
Mazingira magumu na wazazi kutofatilia maendeleo ya kitaaluma ya mabinti zao inachangia kushusha moyo wa kusomea masomo hayo
 
Back
Top Bottom