Nini kilipelekea Twaha Kiduku kupoteza pambano lake dhidi ya msauzi?

Soloma TV Online

Senior Member
Joined
Jun 26, 2023
Posts
104
Reaction score
291
Kwa namna ambavyo tunamfahamu Twaha Kiduku akiwa Ulingoni, mazoezini unahisi nini kimechangia Bondia huyu mwenye kundi kubwa la Mashabiki kila kona ya Tanzania kuchakaa katika ardhi ya nyumbani?
 
Pambano lilikua zuri sana.Nimefurahi sana kwasababu kiduku kakutana na mpinzani mwenye sifa nyingi ulingoni tofauti na mabondia wengi aliokua akikutana nao.Twaha ni bonge ya bondia,utulivu wake ulingoni unampa nafasi kubwa yakumiliki pambano ila anakosa maamuzi ya mwisho kwa wakati sahihi,hana sababu yakua nunda kwakuvumilia makonde ya mpinzani wakati yeye apigi na akipiga anakua kachelewa.

Kwenye ilo pambano alitakiwa kubadilika mapema kwa kumpiga mpinzani wake body bunch zakutosha badala yakufocus tu kutaka kupiga kichwa wakati mpinzani wake alishaonyesha ataki amsogelee.Mwili anao,nguvu anazo anachotakiwa ni kubadilika uchezaji wake.Akafanyie kazi mapungufu yake atafika mbali.
 
Uchambuzi mzuri. Pamoja sana.
 
Yule msouth alishamshtukia Twaha staili yake ya kutaka akubananishe kwenye kamba.
 
Msauth alikua smart sana na mtulivu katika kurusha ngumi. Alitumia jab kama njia ya kuji guard hivyo kuharibu mipango ya kiduku alokua anavizia muda wote apige sehemu za points.

Ufupi wa kiduku pia ulichangia kwani muda mwingi alikua akirusha ngumi bila kumfikia msauth. Hata akimkaribia msauth alimshika hivyo kuharibu malengo.

Hii inanikumbusha enzi zile za Tyson alikua akishaona mpinzani wake yuko fit kumliko alikua anafanya chini juu amalize mpambano round za awali Kayla hajafikishana name mbali.
 
Kupigwa ni sehemu tu ya mchezo, Twaha yupo vizuri aendelee kupata mapapambano mengi ya nje itamuongezea makali yake.

Don't give up Twaha you'r the best fighter💪💪
 
Umemaliza.pia naona ana same style of playing,hana jab na hizo body Punch ndo hapigi kabisa ana guard mda mwingi sana wa mchezo kutafuta K,O.
 
Twaha anahojiwa anakuambia alizidiwa kila kitu kuanzia mbinu mpaka hesabu.

Humu tunaulizwa sababu. Unataka atokee jamaa mmoja akuambie mganga wake alikasirika au siyo?
 
Sasa kama hataki asogelewe body punches ili zifike inabidi akubali shuruba kabla hajacounter na body punches.

Ila mpinzani alikua bora katika mbinu. Hiyo AKA ya Predator inaendana naye kabisa,

Out boxers wengi hua hawana miili mikubwa au instincts za KO badala yake wanakua na tech na pumzi ya kukuchosha. Nafikiri Twaha aimarishe chin, aimprove kwenye guard na counter punch
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…