Nini kiliwapata Wamiliki wa hii Michuma? Tunyamaze hata kwa Dk. 3 kuwakumbuka

Wengine wamebadilisha majina kukwepa kufilisiwa na awamu hii
 
Kiswele nadhani lilikuwa na injili za rocket
 
Shabaha ilikuwaga na ndege juu, kipindi hicho ukiipanda hyo gari unahisi uko peponi tayari.
 
Kuna akamba pia saivi simuoni road tulikuwa tunapanda kutoka mwanza mnapita silali then kenya mpaka Namanga halafu tunachukua njia ya Arusha mpaka Tanga kipindi hicho mvua kidogo tu barabara ya kati hakupitiki Mlima senkenke ilikuwa sehemu korofi sana plus kutekwa, Mshua waliwahi kutekwa na Gari ya Maiti ikabidi wawaombe tu watekaji nao kuona vile waka waachia tu
 
Nami wa kanda ya ziwa nauliza hawa wa ma bus ya Tanganyika bus Na trans afrikan?
 
Tawaqal ipo bana, wanapiga route za nje ya nchi wako ofisi yao iko maeneo ya fire(faya) town
 
Ukisha jua ikusaidie ninj? Aiseee Group lisha poteza maana, badala ya kudiscus Idea tunaanza kudscus watu
 
Leo hujaenda shule? na mpaka unachanganya unadhani hii ni whatsapp. Mitihani ya form two mnafanya mwezi wa ngapi Munasia Rusida? (Murusi) hivi Munasia yule Rafiki yako Zaida yeye alifaulu mwaka jana?

Usome sasa umerudia sana kidato umri huo ulipaswa uwe kidato cha 5 kama sikoei. We ndo kwanza upo kidato cha pili. Punguza wanaume usome bint.

Ukisha jua ikusaidie ninj? Aiseee Group lisha poteza maana, badala ya kudiscus Idea tunaanza kudscus watu
 
Biashara za ushirikina lazima zianguke.
Biashara za kichawi hizo
Watu mna akili finyu sana
Badala ya kufanya business analysis kwa nini biashara zilikufa ninyi mnakimbilia kuwa zilikuwa na uchawi!!!

Rolling stock maintainance, spares etc?
Market study and niche?
Business Management?
Reinvestment into business?
Operational costs?

Uchawi huu wa kuanalyse ni mgumu zaidi kwa watu wengine!!!
 
Yaa nyuma ya seco pale mzee
Umenikumbusha huyu wa karibu na Lugalo dereva wake mmoja akijulikana Michael (RIP) na wa kule Frelimo mwanae nilisoma nae.Kwacha ilitufaa sana baada ya kuondokana na Railway
 
Biashara za usafirishaji zinachangamoto zake,kuna clip moja ukiisikiliza utagundua si rahisi kufanya hii biashara.
 
Nami wa kanda ya ziwa nauliza hawa wa ma bus ya Tanganyika bus Na trans afrikan?
Hawa tanganyika bus walihamishia biashara zao kwenye mahotel

HOTEL TILAPIA mwanza

KIJELESHI TENTED CAMP ramadi serengeti

MBALAGETI SAFARI CAMP serengeti

CHAMUGASA HOTEL ramadi

Na bado wanasafirisha watalii kuwapeleka mbugani
 
Biashara za mabasi zinachangamoto sana toka sumatra ilivyoanzishwa wafanyabiashara wa zamani wengi waliacha biashara hiyo na kuhamia kwenye malori,changamoto kubwa ilikuwa ni ile nauli ya kupangiwa bila kuangalia gharama halisi za uendeshaji wa mabasi mfano kwa zamani ilikuwa rahisi tu unachukua lori unaligeuza kuwa basi unatumia gharama kidogo ila faida kubwa tofauti na sasa hivi ambapo gharama ya kununua basi ni kubwa.

Mfano (zhongtong Climber bei yake ni $180000/=ushuru mil 86) na ukute hapo labda mtu kachukua ni mkopo alafu ukija kwenye hizi nauli zetu zilizopangwa na latra faida ni kidogo sana,kwa sababu gari mpya mpaka ije urudishe pesa yako inaweza kuchukua hata miaka mitatu hapo bado faida.

Ndio maana hao wa zamani walivyopiga hizo hesabu waliamua kuachana na hiyo biashara hata sasa hivi ukiangalia kuna kampuni zinakuja zinavuma kwa mda mfupi alafu zinapotea wengi wanaishia kuuza mabasi yao na baadhi yao benki wanaishia kupiga minada hayo magari
 
Wengine wamebadilisha majina kukwepa kufilisiwa na awamu hii
Kwani TISS hawapo BRELA, LATRA, TRA, POLICE?

Repositioning haihusiani na kukwepa serikali bali wananchi
 
Hawa tanganyika bus walihamishia biashara zao kwenye mahotel

HOTEL TILAPIA mwanza

KIJELESHI TENTED CAMP ramadi serengeti

MBALAGETI SAFARI CAMP serengeti

CHAMUGASA HOTEL ramadi

Na bado wanasafirisha watalii kuwapeleka mbugani
Kwa maelezo haya wewe ni mtu wa ndani
 
Mamba safari, kitu rangi ya njano Arusha to Mwanza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…