Elections 2010 Nini Kimejiri Kyela Kwenye Kampeni za Dr. Slaa?

Elections 2010 Nini Kimejiri Kyela Kwenye Kampeni za Dr. Slaa?

Albedo

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2008
Posts
5,558
Reaction score
1,456
Jamani nasikia leo Dr. Slaa alikuwa Kyela, sasa wadau wa Kyela hebu tujulisheni kilichojiri japo kwa ufupi









KAMPENI KWA SIMU ZA MIKONONI NI ZAIDI YA KAMPENI ZA SHUKA KWA SHUKA ZA SALMA, PIGIA NDUGUYO MWELEZE UJUMBE WA MABADILIKO
 
Leo hata kwenye taarifa ya habari sijaona habari ya Dr kule Kyela, hajaenda na waandishi au?

Watu wa kanda hizo tunaomba habari!
 
kyela walisema ubunge mwakyembe ila urais ni dr slaa,atakuwa amefunika mbaya sasa wanaogopa umma kujua,dunia ya sasa hakuna cha kuficha
 
Leo hata kwenye taarifa ya habari sijaona habari ya Dr kule Kyela, hajaenda na waandishi au?

Watu wa kanda hizo tunaomba habari!


Mie na asume kama kawa kafunika mbaya...mwakyembe upooooooooooooooo
 
Kulikuwa na watu wengi sana na hasa vijana. Dr. Slaa alionekana kama anampigia kampeni Dr. Mwakyembe badala ya mgombea wao.

Vijana wengi walikuwa wanasema kura ya ubunge Mwakyembe lakini urais Dr. Slaa. Kundi kubwa la vijana ni lile linalomwunga mkono Mwakyembe na ambalo lilimpa ushindi kwenye kura za maoni.

Wazee na akina mama walikuwa wachache. Kafanya mikutano Matema, Ipinda na Kyela mjini. Sikuhudhuria mikutano ya Matema na Ipinda kwahiyo sijui ilikuwaje.

Watu walikuwa wengi sana kuliko ule mkutano wa JK. Ila wana CCM ambao mimi nawafahamu walikuwepo wengi, haijulikani kama wanataka kumpigia kura Dr. Slaa au walienda kusikiliza tu mkutano wake.

Kama hawa vijana wote wamejiandikisha, basi Dr. Slaa anaweza kuwa na kura zake nyingi kuliko nilivyokuwa nafikiria mwanzoni ingawaje bado JK ana nafasi ya kuongoza kwa Kyela kwasababu ya kura za wanawake na wazee na pia mtandao wa CCM ambao uko kila sehemu. CHADEMA hawana uongozi wa kuhakikisha hawa wafuasi wao wanafuatiliwa na kuhakikisha wanapiga kura. Kikubwa hawana watu ambao wako tayari kufa wakilinda kura zao. Washabiki wao wengi ni wale wale CCM ambao wakirubuniwa kidogo wanaweza kurudi CCM.
 
Mkulima, thank you for update. Keep it up
 
Kulikuwa na watu wengi sana na hasa vijana. Dr. Slaa alionekana kama anampigia kampeni Dr. Mwakyembe badala ya mgombea wao.

Vijana wengi walikuwa wanasema kura ya ubunge Mwakyembe lakini urais Dr. Slaa. Kundi kubwa la vijana ni lile linalomwunga mkono Mwakyembe na ambalo lilimpa ushindi kwenye kura za maoni.

Wazee na akina mama walikuwa wachache. Kafanya mikutano Matema, Ipinda na Kyela mjini. Sikuhudhuria mikutano ya Matema na Ipinda kwahiyo sijui ilikuwaje.

Watu walikuwa wengi sana kuliko ule mkutano wa JK. Ila wana CCM ambao mimi nawafahamu walikuwepo wengi, haijulikani kama wanataka kumpigia kura Dr. Slaa au walienda kusikiliza tu mkutano wake.

Kama hawa vijana wote wamejiandikisha, basi Dr. Slaa anaweza kuwa na kura zake nyingi kuliko nilivyokuwa nafikiria mwanzoni ingawaje bado JK ana nafasi ya kuongoza kwa Kyela kwasababu ya kura za wanawake na wazee na pia mtandao wa CCM ambao uko kila sehemu. CHADEMA hawana uongozi wa kuhakikisha hawa wafuasi wao wanafuatiliwa na kuhakikisha wanapiga kura. Kikubwa hawana watu ambao wako tayari kufa wakilinda kura zao. Washabiki wao wengi ni wale wale CCM ambao wakirubuniwa kidogo wanaweza kurudi CCM.

asante kwa kutuhabarisha, kweli watu sasa wameelimika siyo kama miaka ya 47, watu wametambua kuwa maendeleo yataletwa na uongozi wa Dr Slaa. heko
 
Back
Top Bottom