Nini kimempata Netanyahu? Atishiwa kuuawa na hajasikika

Nini kimempata Netanyahu? Atishiwa kuuawa na hajasikika

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Mkazi mmoja wa maeneo ya kati ya Israel amekamatwa na kikosi cha kijasusi cha Shin Bet kutokana na kutoa vitisho vya kutaka kumuua waziri mkuu wa Israel.

Wiki iliyopita kitisho kama hicho kilitolewa kwa waziri wa wa mambo ya usalama wa taifa,,Itamar Ben-Gvir ambaye ni mmoja wa mawaziri wenye kutoa matamshi makali daima kwa wapalestina ikiwemo matumizi ya bomu la nyuklia.

Hayo yakidhihirika waziri mkuu huyo tangu afanyiwe upasuaji wa ngiri siku chache zilizopita hajasikika akitoa yale matambo yake dhidi ya Hamas.

Operesheni hiyo ilifanyika kwa mafanikio ambapo mara alipozinduka aliweza kuongea na raisi Biden kuhusiana na mikakati yake ya kivita na kujibu lile karipio la rais huyo wa Marekani juu ya kupeleka jeshi la ardhini eneo la Rafah.

Netanyahu vie vile hajasikika (sijamsikia) akizungumzia kwa undani juu ya kupunguzwa kwa askari wake kutoka eneo lote la Gaza.

Kikawaida wagonjwa wanapofanyiwa upasuaji mkubwa hutakuwa kupata mapumziko na wajizuie kusema sana.

Katika siku za karibuni maandamano ya kumpinga waziri mkuu huyo na sera zake za vita dhidi ya Hamasa yamekuwa makubwa sana na kuongezeka kila uchao.

Muandamanaji mmoja alisikika akitoa maneno ya kudharau operesheni nzima ya Gaza akisema kwamba waliahidiwa kurudishiwa mateka wao lakini kinachotokea kila siku wanatuletea maiti za mateka hao.

Thousands of Israelis protest against government, urging captive deal

 
Ukiwa kiongozi wa umma huwezi pendwa na wote na hayupo kiongozi mkubwa kama rais au waziri mkuu ambaye hajatishiwa maisha, ni vitisho tu vinatofautiana
Ni kweli kabisa
 
Ukiwa kiongozi wa umma huwezi pendwa na wote na hayupo kiongozi mkubwa kama rais au waziri mkuu ambaye hajatishiwa maisha, ni vitisho tu vinatofautiana
Na hata ukiacha uongozi inabidi upatiwe ulinzi wa kutosha yasije yakakupata yaliyompata yule waziri mkuu mstaafu wa Japan.

Kwa Netanyahu nadhani itabidi awe analala kwenye mahandaki daima.
 
Mkazi mmoja wa maeneo ya kati ya Israel amekamatwa na kikosi cha kijasusi cha Shin Bet kutokana na kutoa vitisho vya kutaka kumuua waziri mkuu wa Israel.

Wiki iliyopita kitisho kama hicho kilitolewa kwa waziri wa wa mambo ya usalama wa taifa,,Itamar Ben-Gvir ambaye ni mmoja wa mawaziri wenye kutoa matamshi makali daima kwa wapalestina ikiwemo matumizi ya bomu la nyuklia.

Hayo yakidhihirika waziri mkuu huyo tangu afanyiwe upasuaji wa ngiri siku chache zilizopita hajasikika akitoa yale matambo yake dhidi ya Hamas.

Operesheni hiyo ilifanyika kwa mafanikio ambapo mara alipozinduka aliweza kuongea na raisi Biden kuhusiana na mikakati yake ya kivita na kujibu lile karipio la rais huyo wa Marekani juu ya kupeleka jeshi la ardhini eneo la Rafah.

Netanyahu vie vile hajasikika (sijamsikia) akizungumzia kwa undani juu ya kupunguzwa kwa askari wake kutoka eneo lote la Gaza.

Kikawaida wagonjwa wanapofanyiwa upasuaji mkubwa hutakuwa kupata mapumziko na wajizuie kusema sana.

Katika siku za karibuni maandamano ya kumpinga waziri mkuu huyo na sera zake za vita dhidi ya Hamasa yamekuwa makubwa sana na kuongezeka kila uchao.

Muandamanaji mmoja alisikika akitoa maneno ya kudharau operesheni nzima ya Gaza akisema kwamba waliahidiwa kurudishiwa mateka wao lakini kinachotokea kila siku wanatuletea maiti za mateka hao.

Thousands of Israelis protest against government, urging captive deal

Kwahiyo unataka tukusaidie nini?
 
Wengi wanahasira na jinsi Netanyahu alivyofeli hadi Magaidi wa Hamas kuvamia na kuua watu.

Lakini wengi pia wanasapoti nia yake ya kuwamalizia mbali Magaidi wa Hamas.
 
Wengi wanahasira na jinsi Netanyahu alivyofeli hadi Magaidi wa Hamas kuvamia na kuua watu.

Lakini wengi pia wanasapoti nia yake ya kuwamalizia mbali Magaidi wa Hamas.
Kuhusu Hamas hajaweza kuwamaliza ndio mambo yamezidi kuvurugika.
 
Back
Top Bottom