crankshaft
JF-Expert Member
- Jun 12, 2019
- 1,427
- 3,438
Nakumbuka miaka kadhaa iliyopita hawa jamaa(madrid na barca) walikuwa wakimtaka mchezaji hauchomoi. Hazard 120m,de jong 80m griezmanm 120m n.k. Lakini leo barca hata lewandowski anayepatikana kwa bei chee imekuwa ngumu sana kumpata. Alba rudiger depay aubameyang aguero traore wote wamewapata bure.Epl ndo naona wanatamba siku hizi lukaku 90m haaland 60m nunez 80m sancho 80m grealish 100m na sio mda wanamchukua de jong. Sajili nyingi la liga siku hizi zimekuwa ni za bure tena wachezaji wenyewe wanaenda kupunguziwa mishahara hasa barca. Ni nini kimewakuta hawa jamaa mpaka wamefikia hatua ya kukodisha uwanja kwa ajili ya harusi??