Nini kinafanya viungo vya upande wa kuume kuwa na uwezo zaidi?

Shin Lim

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2012
Posts
7,837
Reaction score
14,198
Habari wana jamvi na pia poleni na majukumu ya kila siku. Nimekuwa nikijiuliza swali hili mara nyingi na nikashindwa kupata majibu ya kujiridhisha kutoka kwa baadhi ya watu kutokana na majibu kuwa mepesi au ya kufikirika tu. Sasa leo naomba wenye uelewa mnisaidie tafadhali.
Hivi ni kwa nini kiungo/viungo vya upande wa kuume vina nguvu au uwezo zaidi kuliko vile vya upande wa kushoto?

1.Jicho: Jicho la kuume lina uwezo zaidi kuliko la kushoto. Uthibitisho upo kwa wapiga picha wakati wa kupiga picha hasa kwa camera za kizamani mara nyingi hutumia jicho la kuume.

2.Mkono: Watu wengi tunatumia mkono wa kuume katika shughuli zetu mfano kuandika, kula nk. Uthibitisho upo kwa karibu kila mtu.

3.Mguu: pia mguu imekuwa vivyo hivyo ila tu kuna baadhi ya watu huwa wana uwezo wa kutumia miguu yote hasa katika mchezo wa mpira wa miguu. Viungo ambavyo sijataja sina hakika kama na vyenyewe vipo kwa mtindo huo.

Watu wengi wamekuwa wakisema eti ni kwa sababu kuna tofauti ya idadi ya mbavu kati ya upande wa kulia na kushoto, wengine wanasema moyo upo upande wa kushoto ndio maana umeathiri viungo hivyo kutokuwa na uwezo sawa na vingine, sasa je huo moyo umeathiri mpaka macho?

Wapiga wanalijua hilo. Naombeni majibu tafadhali.
 
Mwalimu wangu wa biology alinifundisha kuwa ubongo wa kulia ni mdogo kuliko wa kushoto,na ubongo wa kulia unacontrol upande wa kushoto wa binadamu kadhalika ubongo wa kushoto unacontrol upande wa kulia wa mwili wa binaadamu, so kwa kuwa ubongo wa kushoto ndo mkubwa hivyo kwa ukubwa wake unafanya upande wa kulia wa mwanadamu kuwa active zaidi ukilinganisha na kushoto.

Pamoja na story hii kuna siku nilisoma kitabu flani cha saikolojia walipinga hii habari kwa kusema no scientific proofs rather than just logical arguments.
 
Korodani la kulia ni kubwa kuliko la kushoto,titi la kulia ni kubwa kuliko la kushoto,unyayo wa mguu wa kulia ni mkubwa kuliko wa kushoto,jiulize pia
 
Mkuu hapa hamna la zaidi sana sana ni law of use and disuse ndo ina apply zaidi. Nyingine mbwe mbwe tu

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Korodani la kulia ni kubwa kuliko la kushoto,titi la kulia ni kubwa kuliko la kushoto,unyayo wa mguu wa kulia ni mkubwa kuliko wa kushoto,jiulize pia

Unyayo wa mguu wa kuume ni mkubwa kuliko wa kushoto? Hadi korodani pia zinahusika?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Hivi wanaotumia mkono wa kushoto hadi katika mouse za kompyuta hutumia mkono huohuo? Ni swali tu.
 
Hivi wanaotumia mkono wa kushoto hadi katika mouse za kompyuta hutumia mkono huohuo? Ni swali tu.

Kuhusu computer huwa kuna setting za mouse unaweza fanya ili kama unatumia left hand uweze kutumia mouse kama atumiayr right hand.
 
ukivishughulisha vivyo viungo vitapata nguvu pia sawa sawa na vya kulia, mfano wachezaji wa mpira wanafanyia mazoezi miguu yote na hivyo anaweza kuutumia mguu wa kulia sawa na wa kushoto
 
Swali zuri sana, hakuna suala la use and disuse! Ukweli ni kuwa upande wa kulia wa mwili upo imara zaidi pamoja na viungo vya upande huo!
 
Mimi mkono na mguu wa kushoto ni more active ukilinganisha na viungo hivyo vya kulia.
 
Ni kwasababu Adamu alitolewa ubavu mmoja [Biblia haispecify exactly ni upande upi]
ila inasadikiwa ni upande wa kushoto na kuumbiwa Eva hivyo mwanamume anakuwa na
upungufu kiasi wa nguvu ya utendaji kwa upande wake wa kushoto
ila mwanamke hananguvu ukilinganisha na za mwanamume kutokana na kuumbwa kutoka
kwa mwanamume!

MWANZO 2 : 21 - 23
2.21 Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake,
2.22 na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu.
2.23 Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume.
 
Naungana na mdau hapo juu ni law of use and disuse darwin wanao2mia mashoto wapo active na shoto sana.
 
korodani la kulia ni kubwa kuliko la kushoto,titi la kulia ni kubwa kuliko la kushoto,unyayo wa mguu wa kulia ni mkubwa kuliko wa kushoto,jiulize pia

umeulizwa swala la kuwa na nguvu nyingi au chache mbona wajibu tofauti mjomba?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…