Mpendwa jina la Mtwara ni kama majina mengine ya KIARABU hapa nchini...KM :-(Dar/tanga/Tabora/kigoma/singida nk nk) !! Mtwara kwa kiarabu ni UPGRADED yaani imeboreka/ubora tulipa jina Mtawara hivyo iliboreshwa kwa kadri ya mazao yenye neema huko!!Kama tujuavyo majina mengi ya miji au sehemu yanakuwa na historia yake au chanzo chake, mimi leo hii naomba kujua maana ya jina mji wa mtwara,
Ki ukweli ingawa nimezaliwa na kusoma mtwara lkn cjawahi kusikia source ya jina hili, na ikumbukwe pia kuwa mtwara leo hii ni mji muhimu sana ktk uchumi wa inchi yetu, ingawa zamani ulikuwa ni mji wa adhabu kwa wafanyakazi wa serikali, sasa sio mbaya leo hii tukijua historia ya mji huu ulikoanzia, najua kuwa makabila enyeji wa mji huu wamakonde, wamakua, na wamwera,
Je wewe ujua nini kuhusu mtwara au gas town ( karibu sana)
mimi ningependa kujua maana ya Nangwanda Sijaona
Yeah, Lawi Nangwanda Sijaona, moja ya malengendary wa Mtwara enzi hizo hasa za Awam ya Kwanza. Ni mdau muhimu katika mkoa mzima wa Mtwara. Inatajwa hata ile barabara ya Mtwara hadi Masasi(km201) ni kwa influence zake. Hii ilikua na lami tangu miaka ya 80.Japo kwa sasa imeanza kuchoka. Bila yeye Mtwara au kusini kwa ujumla lami ilikua ni anasa.Huyu ni mzee maarufu Mtwara Mzee Sijaona. Watoto wake wapo akiwemo mama Sijaona alikuwa balozi wetu Japan