Kuchakachua ni kitendo cha kuchanganya vimiminika viwili tofauti na kufanya kimiminika kimoja, mfano kuchanganya mafuta ya petroli na mafuta ya taa, lakini neno hili sasa limeongezwa matumizi na kuwa linatumika kueleza aina tofauti ya udanganyifu, na kama ulivyoona matumizi ya neno hili sasa yameingia kila mahali kuanzia kwenye kuvuruga matokeo ya uchaguzi hadi kwenye kuelezea watu wadanganifu kwa wapenzi wao1 kwa kifupi sasa ni kama limepoteza ile maana yake ya awali. na inasemekana neno hili asili yake ni uzigua na hasa wazigua wa maeneo ya zaraninge na msata mkoani pwani!