Nini maana ya "Kuishi Vizuri na Watu"? Je, ni sahihi kuenenda ndivyo sivyo ili kujijengea taswira njema katika jamii?

Mwana una bore sana

How come utimbe maskani apeche alolo?

Day nyingine ukitimba tunakuweka bond...kwa dula mbabe!

Achaga mambo ya kiwaki...ishi vizuri na wana
Si kweli. Wana wenyewe masoro hivyo hamna dira ndo mnamlaani mshikaji kisa kawachana laivu makavu? Dua lenu la kuku mwewe hahusiki nalo. Chapeni lapa.
Mwana weekend timba tena na uwakazie hivyo hivyo uso wa Ngiri. Banzooka wakubwa hawa
 
kuishi vizuri na watu ungewaambia ndugu zangu nilikuwa napita tu nikasema niwasalimu tu hivyo sikutembea na hela yoyote zaidi ya bajeti ya safari yangu ila msijal siku nyingine nayo siku. Ila habari za kuanza kuwaeleza sijui labda misiba sijui ugonjwa huo ni uduanzi tena ujinga sana.
 
Ina maana nyingi kulingana na makuzi yako na utamaduni wa jamii inayokuzunguka

Ila tukiziungumzia mazingira yetu ya kitanzania, ni kama kushirikiana na jamii, kupractice maadili ya jamii kama vile kuheshimu wakubwa, kusaidia wazee, kuheshimu wazazi, kushiriki mambo ya kijamii kama misiba, sherehe nk kama unaishi mjini basi siku ukienda kijijini hakikidha unapita kwaaa majirani na ndugu kuwasalimu hata na kilo moja ya sukari, anapotokea mgonjwa katika jamii unayoishi unatenga muda hata wa kutoa pole, anapotokea mzazi kwente jamii unayoishi basi unatoa hongera na mambo kama hayo

Kwa kifupi maisha ya kiafrika ni magumu sana its all about satsifying people hata kama huna uwezo huo, ukienda kinyume kuna siku utapatwa na jambo kama msiba au sherehe jamii nzima inakususia inasema huyu hajui kuishi na watu[emoji849]
 
Umefafanua vema sana mkuu...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…