Nini maana ya kukonyeza?

mimiks

JF-Expert Member
Joined
Mar 17, 2013
Posts
1,416
Reaction score
2,794
Swali langu ni kama lilivyo hapo juu, nini maana ya kukonyeza.

Kama wewe ni wa kike ukakonyezwa na mwanaume ni nini kitakuja kwenye akili yako yani utatafsiri vipi konyezo hilo na utajisikiaje na kama wewe ni wa kiume, binti akikukunyeza unaweza ukatafsiri vipi na utajisikia vipi?

Kwenye hizi smart phones na gadgets nyinginezo utakuta mtu anakutumia ki-emoji cha 'wink' 😉 ama barabarani, mgahawani ama mahala popote panapokutanisha watu unaweza kuta mtu anakukonyeza.

Je wajua maana yake na wakati gani mtu akitumia konyezo ni halali na wakati gani ni jinai?
 
Kwa uelewa wangu ni njia ya kuflirt au kutongoza lakini mimi binafsi mtu akinikonyeza namchukulia kama malaya….Kuna rafiki yangu mmoja aliniambia kwao hio ni ishara ya salamu!!!
 
niangalie machoni halafu fanya hivi.. umeona eeh! hiyo ndo maana ya kukonyeza
 
Mazingira au context ya konyezo hilo ndo yatafafanua nin kinamaanishwa.eg askar wapelelezi hutumia ishara hiyo kazin
 
Kwa uelewa wangu ni njia ya kuflirt au kutongoza lakini mimi binafsi mtu akinikonyeza namchukulia kama malaya….Kuna rafiki yangu mmoja aliniambia kwao hio ni ishara ya salamu!!!

Asante kwa mchango wako. Yani mtu anapokukonyeza u feel uneasy
 
Maana inategemea na mazingira
kuna kumkonyeza mtu kama anataka kuongea kitu hapo ina maanisha unamstopisha asiongee
mpo kwenye watu wengi ukamkonyeza hiyo ni salamu
uuuh hilo konyezo lingine ndo nalipenda mie ila sijui lina maanisha nini
nikikonyezwa na mtu nnaempenda huwa nalegea kabisa....
 
Kukonyezana ni kama mchombezo fulani hvi ambao una maana kati ya wawili hao,mkonyeza na mkonywezaji!
 
kukonyeza ni kama indiketa kwenye gari...najua wote mnajua kazi ya indiketa...
 
stranger akinikonyeza,naona kaniona mal aya,sidhani kama nimewahi konyeza me.
 
Basi mimi ni malaya niliyekubuhu maana napenda sana kukonyeza si mwanaume wala mwanamke wote wa saizi yangu na watoto.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…