Nini maana ya masoko ya mitaji na dhamana?

Nini maana ya masoko ya mitaji na dhamana?

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
20210202_114109_0000.png


Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) ni taasisi ya serikali iliyo chini ya Wizara ya Fedha na Uchumi iliyoanzishwa na Sheria ya Masoko ya Mitaji na Dhamana ya mwaka 1994 ili kusimamia na kuendeleza masoko ya mitaji hapa Tanzania.

Majukumu makubwa ya mamlaka hiyo ni pamoja na:-

a) Kuanzisha na kuendeleza masoko ya mitaji Tanzania;

b) kuidhinisha uanzishwaji wa masoko ya hisa na mifuko ya uwekezaji wa pamoja, na kutoa leseni kwa wataalam wa masoko ikiwa ni pamoja na madalali, wachuuzi, wawakilishi wao, washauri wa uwekezaji, n.k.

c) Kusimamia masoko ya mitaji pamoja na wataalam wote wanaohusika na utendaji wa masoko hayo; na

d) Kuishauri Serikali kwenye masuala yote yahusuyo masoko ya mitaji na dhamana
 
Upvote 0
... kwani lengo la huu uzi ni kutuelimisha juu ya CMSA na majukumu yake au ni kutupa majibu ya swali "Nini maana ya masoko ya mitaji na dhamana?". Kama majibu yenyewe ndio hayo, kazi ipo!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom