Nini maoni yako katika suala la mwanaume kufunga kizazi?

Naomba kujua sababu inayokufanya usikubaliane na hili la wanaume kufunga uzazi
Kwanza sizani kama kuna kitabu cha dini kimeeleza kwamba kuna ulazima kufunga kizazi,
Pili mungu anasababu zake nyingi sana za kuniumba mimi niwe na uwezo wa kumpa ujauzito mwanamke,
Tatu tutu nikifanya hivyo wanaweza nipelekea kuwa muhuni, kuweza kutembea hata na wanafunzi nikiondoa hofu kuwa hata nikitembea nae hatopata ujauzito.
Tatu kwa sasa bado nahitaji kuwa na familia labda nikifikisha miaka sitini ndo nifanye hilo zoezi, hata ivyo itakuwa haina haja kwani nguvu zenyewe zitakuwa zoofu,
4. Ujue sijaoa ivo, kwa hiyo sihitaji kusikia hiyo kitu kabisaaaa

Umeridhika haya toa na ww maoni yako
 
Somehow nmeridhika. Ila huko kwenye imani naomba nisiguse. Lkn hapa kwenye kua muhuni:, Mmmmh!. Nadhan ni tabia tu ya mtu. Labda kwa hii ya mwisho kua unahitaji kua na familia, it's Ok!. Lkn unapofunga kwan c unapumzika na ukitaka kuzaa wanatoa kizuizi??. Kwa maoni yng Nash hii inafaa kwa walio kwen ndoa au wale wanaotaka kuzaa kwa mpango. Na kwa mwanaume ni kat tu kuonesha Upendo kwa mwenzie...., hv cjaona ubaya wa juu ya hili. TENA NNGEKUA MWAUME NNGEKUA WA KWANZA KUMSAIDIA MKE WNG KUFUNGA HII KITU.
 
Hii kwa wanaume unafanyiwa operation na unakuwa huna uwezo wa kutia mimba tena aisee, ndo maana siungi mkono
 
Naomba nikushawishi tuuu, hv km ww na mwenzio mmepanga kua na watoto wanne, na tayari mnao. Nambie ni wapi ilipo hofu yako??
Ok na ikitokea maafa ya watoto wako huku wewe huna uwezo wa kupata mtoto siunaona itakuwa ni maumivu mara mbili
 
Ok na ikitokea maafa ya watoto wako huku wewe huna uwezo wa kupata mtoto siunaona itakuwa ni maumivu mara mbili
Oooh, hapo ss ni sawa...., kwa maana hiyo mwanamke ndo aumieee!, au??. Napo ss hy itakua ni mipango ya Mungu.
 
Oooh, hapo ss ni sawa...., kwa maana hiyo mwanamke ndo aumieee!, au??. Napo ss hy itakua ni mipango ya Mungu.
Me nahisi kuna njia mbadala za uzazi wa mpango sioni kama kuna ulazima wa kufunga kizazi kabisa na usipate mtoto tena, me sishaur mtu afunge uzazi, nashauri tu atumie njia za uzazi wa mpango pindi akihitaji mtoto apate tu, au unasemaje hapo
 
Pamoja na wazungu kupendelea na kuhamasisha uzazi wa mpango bado kwa hili wanaume ulaya wanafunga breki!!
 
Anayetakiwa kufunga uzazi ni yule anayeshika mimba.Mwanaume tangu lini kashika mimba?Yeye ni kanyaga twende tu,shauri yake mwanamke .
 
Me nahisi kuna njia mbadala za uzazi wa mpango sioni kama kuna ulazima wa kufunga kizazi kabisa na usipate mtoto tena, me sishaur mtu afunge uzazi, nashauri tu atumie njia za uzazi wa mpango pindi akihitaji mtoto apate tu, au unasemaje hapo
Hahaaa, kiukweli umenimalizaaa. Umeongea neno haswaaa!.Sante sn.
 
ushoga unaanza hivo hivo yani taratiibu.baada ya kufunga kizazi atapata wazo la kupunguza na za kiume kabisa kisha akataifisha mgodi 0713
 
Ndio njia rahisi na isiyosumbua. Kufunga kizazi mwanamke ni Nguni kuliko dume. Wanaume wote fanyeni hii njia.
 
Kampeni ya kufungwa kufungwa kizazi kwa wanaume imezinduliwa Kenya na wanaume zaidi ya 30 walishiriki ktk zoezi hilo siku ya uzinduzi.

Na hapa Tanzania wanaume wanafunga uzazi lakini ni baada ya counselling sana kwani njia hautazaa tena.
Madness of rhe highest order.
 
Haya mambo ya mwanaume kufunga kizazi ndo mwanzo wa kujiletea tezi dume la mapema kabla hata hujafika miaka 50. Waendelee kufunga kina mama tu kama zamani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…