Nini Simba ifanye kuvuka group stage ya CAF CL

Nini Simba ifanye kuvuka group stage ya CAF CL

Joined
Nov 25, 2020
Posts
73
Reaction score
170
Ijumaa hii Simba ataanza kampeni yake ya kutinga robo fainali ya CAF CL kwa kumenyana na AS Vita Club ya DRC katika uwanja wa mashujaa pale Kinshasa. Pambano la mwisho uwanjani hapo alipoteza kwa 5–0 lakini mambo mengi yamebadilika katika vikosi vya timu zote mbili. Vita Club waliuza wachezaji wao hatari kama Francis Kazadi Kasengu, Fabrice Ngoma, Jean Jacques Makusu Mundele, Tuisila Kisinda n.k.

Simba wachezaji wa kikosi cha kwanza walioondoka ni wawili tu Emmanuel Okwi na kiungo mkabaji mghana lakini wakasajiliwa Tadeo Lwanga, Luís José Micquisson, Benard Morrison, Larry Bwalya, na Joash Achieng. Hawa wamedhihirika kuongeza ubora wa Simba. Pia wamemuongeza beki mzimbabwe Peter Muduhwa na striker mnaija Junior Lokosa. Hawa ubora wao haujafahamika bado ndani ya Simba.

Simba ya safari hii inaubora na uwezo wa kupata sare ama ushindi DRC na Sudan ikiwa watakuwa na utayari na ari ya kufanya hivyo. Lakini pia wanahitaji kufanya hivyo ili kujihakikishia nafasi mbili za juu. Msimu wa 2018-19 Simba licha ya kushinda mechi zake zote za nyumbani na kupata alama 9 bado ilihitaji wengine wamfanyie kazi na kweli Al Ahly alimfanyia kazi pale Algeria kwa kuwabana mbavu Saoura na kutoka nao sare.

Ilikuwa ni faida kwa Simba kwani kama Saoura angeshinda basi angemaliza na alama 10 na kufuzu huku Simba akibaki. Pia hao hao Saoura walimfanyia Simba kazi pale Kinshasa kwa kutoa sare ya 2-2 dhidi ya Vita club kwani Vita angeshinda basi angemaliza na alama 9 sawa na Simba lakini angemzidi Simba kwenye head-to-head, Vita alikuwa na magoli 6-2 hivyo angefuzu na kumwacha Simba.

Msimu huu hatuna uhakika kama El merrikh anaweza kufanya kazi hiyo pia hata hawa vita hatufahamu kama wanaweza kumzuia El merrickh (haijulikani yupi kati yao ni bora na anaubora kiasi gani) hivyo ni muhimu Simba akapata alama ugenini ili walau amalize na alama 13 yaani ashinde na kupata sare dhidi ya Vita na El merrikh (alama 4), kisha ashinde zote za nyumbani (alama 9).

Kwa kuzingatia ubora walionao na kutokuwepo mashabiki kwenye nchi hizo basi hili linawezekana kabisa. Hata hivyo wanapaswa kufahamu kuwa watajaribiwa sana kwa baadhi ya wachezaji kukutwa na covid-19 fake. Wawe na utayari wa mapambano.
 
General plan iwe kwanza kushinda zote kisha kupata ushindi mmoja tu Away au sare mbili.
Tactically.

Attacking: lazima tubadilike na kushambulia kwa kasi tunapoondoka zone yetu kwenda kwenye lango lao.
Defensive: ni lazima tuimprove zonal marking yetu hasa kwenye cross na mipira ya kutengwa.

Itatubidi pia tuweke juhudi kwenye kuwin mipira ya juu kwani tunatumia wachezaji wengi ambao hawapigi vichwa hata pale ambapo mpira unamlazimisha atumie kichwa mfano. Bwalya na chama.

Away Game approach tunaweza kutumia viungo asilia wa ulinzi wawili ili safu yetu ya ulinzi isifikiwe kirahisi au beki wa kati wawe watatu lakini nashauri hii itumike endapo tu nyoni atakuwa sehemu ya beki hao watatu wa kati kwa ajili ya kumaintain pressure ya mashambulizi.

Angalizo. Tucheze more collective hasa kwenye kulinda unaweza kurefer utofauti wa Morrison na Chikwende (ambaye nadhani haruhusiwi kucheza). Morrison anabak mbele hata tunapokuwa tunapoteza mpira tofauti na chikwende. Jambo ambalo hata Jana kwenye mechi ya azam lilitugharimu.

Ni vigumu kuyamaliza yote hayo niliyoyaainisha kwa kipindi kifupi ila tukiyazingatia baadhi basi tunaweza kufanya jambo. Kocha mpya ana kazi kubwa mno kama mgeni na anaenda kwenye mashindano makubwa.
 
Mimi nalia na beki zetu tu hizi aisee,beki zetu za simba wakati mwingine zinakuwa kama gari za mkaa tripu moja shamba nyingine gereji..umakini unahitajika vilivyo kabisa kwenye ulinzi wetu...
 
Ijumaa hii Simba ataanza kampeni yake ya kutinga robo fainali ya CAF CL kwa kumenyana na AS Vita Club ya DRC katika uwanja wa mashujaa pale Kinshasa. Pambano la mwisho uwanjani hapo alipoteza kwa 5–0 lakini mambo mengi yamebadilika katika vikosi vya timu zote mbili. Vita Club waliuza wachezaji wao hatari kama Francis Kazadi Kasengu, Fabrice Ngoma, Jean Jacques Makusu Mundele, Tuisila Kisinda n.k.

Simba wachezaji wa kikosi cha kwanza walioondoka ni wawili tu Emmanuel Okwi na kiungo mkabaji mghana lakini wakasajiliwa Tadeo Lwanga, Luís José Micquisson, Benard Morrison, Larry Bwalya, na Joash Achieng. Hawa wamedhihirika kuongeza ubora wa Simba. Pia wamemuongeza beki mzimbabwe Peter Muduhwa na striker mnaija Junior Lokosa. Hawa ubora wao haujafahamika bado ndani ya Simba.

Simba ya safari hii inaubora na uwezo wa kupata sare ama ushindi DRC na Sudan ikiwa watakuwa na utayari na ari ya kufanya hivyo. Lakini pia wanahitaji kufanya hivyo ili kujihakikishia nafasi mbili za juu. Msimu wa 2018-19 Simba licha ya kushinda mechi zake zote za nyumbani na kupata alama 9 bado ilihitaji wengine wamfanyie kazi na kweli Al Ahly alimfanyia kazi pale Algeria kwa kuwabana mbavu Saoura na kutoka nao sare.

Ilikuwa ni faida kwa Simba kwani kama Saoura angeshinda basi angemaliza na alama 10 na kufuzu huku Simba akibaki. Pia hao hao Saoura walimfanyia Simba kazi pale Kinshasa kwa kutoa sare ya 2-2 dhidi ya Vita club kwani Vita angeshinda basi angemaliza na alama 9 sawa na Simba lakini angemzidi Simba kwenye head-to-head, Vita alikuwa na magoli 6-2 hivyo angefuzu na kumwacha Simba.

Msimu huu hatuna uhakika kama El merrikh anaweza kufanya kazi hiyo pia hata hawa vita hatufahamu kama wanaweza kumzuia El merrickh (haijulikani yupi kati yao ni bora na anaubora kiasi gani) hivyo ni muhimu Simba akapata alama ugenini ili walau amalize na alama 13 yaani ashinde na kupata sare dhidi ya Vita na El merrikh (alama 4), kisha ashinde zote za nyumbani (alama 9).

Kwa kuzingatia ubora walionao na kutokuwepo mashabiki kwenye nchi hizo basi hili linawezekana kabisa. Hata hivyo wanapaswa kufahamu kuwa watajaribiwa sana kwa baadhi ya wachezaji kukutwa na covid-19 fake. Wawe na utayari wa mapambano.
Kwanza wazidi kufanya mazoezi na kicha atafute mbinu za kuwapanga morison,mikisone,chama na bwalya pamoja,na kule nyuma babu anyangi hayupo kaumia atafute mbadala
 
Kuroga na kuwanyunyizia sumu changin room hapo taifa watakapocheza na timu za kutoka nje
 

Attachments

  • VID-20210207-WA0025.mp4
    3 MB
Kikubwa wanachoweza kufanya ni kupunguza idadi ya magoli na wapate angalau sare mbili nyumbani
 
Sasa hivi simba ina wachezaji wawili ( Jose Luis Miquisone na Morrison) wanaoweza kubadili matokeo katika mazingira magumu hata ya ugenini ..so tuwe na amani ndugu zangu watanzania!
 
Tuwe makini kwenye umaliziaji maana huku tunapoenda kosa kosa tano hakuna. Na pia chama aache kumsubiria mtu ampige chenga au kanzu, inatakiwa tuchambulie kwa kasi na kukaba,siyo tunasubiria opponents wajipange ndio tunaanza mashambulizi
 
Kikubwa wanachoweza kufanya ni kupunguza idadi ya magoli na wapate angalau sare mbili nyumbani
Mkuu Mwaka juzi mlisema hhaya tukatoboa ...si vibaya ukikutaa wanaume wanaongea ukapita tu !
 
Watumie viungo wakabaji wawili....napendekeza Thadeo awe chini... Mkude juu.....kwenye beki wa kati sijui itakuaje...Onyango na Elasto wote majeruhi...Ame na Kenedy sijui kama wataweza kusaidia....juu ya Mkude akae Konde boy...Kagere...chama na kushoto Bwalya....beki za pembeni Kama kawaida...sub...chikwende..... mwanasheria msomi ...na wengine.
 
Siku hiyo kocha ajilipue tu....nyuma Kati Wawa,Erasto Ame,Bwalya ...dimba la Kati,.pembeni Morrison Na Konde Boy,then Kagere au Boko!
Sub HD ,Mkude,Chikwende
 
Kila la heri AS Vita, National Al Ahly na El Mereikh

Pigeni huyu Paka Fc arudi kwao, maana amesajili Genge la wahuni na kuzindua jezi ziso na maana

Piga hao Simba mpaka waache tabia zao za misemo yao mara Do or Die, tiki taka mpaka kwa mpaka, War in Dar, Next Level....

Tumewachoka sioni jipya watakalofanya warudi wajipange tu
 
Back
Top Bottom