Nini tofauti kati ya neno Jaji na Hakimu

Nini tofauti kati ya neno Jaji na Hakimu

Jaji ni mwamuzi wa kesi katika mahakama kuu. Cheo chake ni cha kuteulowa na raisi na anasimamia sheria za uamuzi zinazotumika katika mahakama kuu.

Hakimu ni mwamuzi wa masuala na kesi zinazowasilishwa katika mahakama ya mwanzo, wilaya na ya hakimu mkazi mkoa. Mamlaka yao huyapata kwa kuomba kazi na kuajiriwa na kama watumishi wengine wa serikali. Kwa ngazi ya kimamlaka suala likishidikana mahakama za chini zinazosimamiwa na mahakimu basi anayeona hajaridhishwa na huo uamuzi wao atakata rufaa kwenda kwa jaji.

Kuna masuala hutakiwa kuanzia kwa mahakimu na pia kuna masuala ni lazma yaanzie kwa jaji(mahakama kuu).
 
Jaji ni mwamuzi wa kesi katika mahakama kuu. Cheo chake ni cha kuteulowa na raisi na anasimamia sheria za uamuzi zinazotumika katika mahakama kuu.

Hakimu ni mwamuzi wa masuala na kesi zinazowasilishwa katika mahakama ya mwanzo, wilaya na ya hakimu mkazi mkoa. Mamlaka yao huyapata kwa kuomba kazi na kuajiriwa na kama watumishi wengine wa serikali. Kwa ngazi ya kimamlaka suala likishidikana mahakama za chini zinazosimamiwa na mahakimu basi anayeona hajaridhishwa na huo uamuzi wao atakata rufaa kwenda kwa jaji.

Kuna masuala hutakiwa kuanzia kwa mahakimu na pia kuna masuala ni lazma yaanzie kwa jaji(mahakama kuu).
[emoji1374]

Sent from my TECNO PR651H using JamiiForums mobile app
 
Hawa ni watu wawili wanaofanya kazi moja ya kuhukumu kesi mahakamani.

Utofauti wao ni kwamba;



1. Level: Hakimu ni kuanzia mahakama za mwanzo, wilaya na mahakama ya mkoa wakati jaji ni kuanzia mahakama za juu yaani mahakama kuu na mahakama ya rufaa ambayo ndiyo mahakama ya mwisho katika kutoa maamuzi nchini.



2. Upatikanaji wao: Hakimu anapata kazi kwa kuomba kazi utumishi na kuajiriwa wakati jaji anapatikana kwa kuteuliwa na raisi pekee kwa kigezo cha kufanya kazi za kisheria (hakimu, wakili n.k) kwa zaidi ya miaka 10 mfululizo na kuendelea.



3. Kuwafukuza kazi: Ni rahisi kumtimua kazi hakimu lakini kwa jaji hali ni tofauti hata kwa raisi mwenyewe. Maana inabidi raisi aunde tume ya majaji toka jumuiya ya madola ndio watoe mapendekezo juu ya makosa yake.
 
Hawa ni watu wawili wanaofanya kazi moja ya kuhukumu kesi mahakamani.

Utofauti wao ni kwamba;



1. Level: Hakimu ni kuanzia mahakama za mwanzo, wilaya na mahakama ya mkoa wakati jaji ni kuanzia mahakama za juu yaani mahakama kuu na mahakama ya rufaa ambayo ndiyo mahakama ya mwisho katika kutoa maamuzi nchini.



2. Upatikanaji wao: Hakimu anapata kazi kwa kuomba kazi utumishi na kuajiriwa wakati jaji anapatikana kwa kuteuliwa na raisi pekee kwa kigezo cha kufanya kazi za kisheria (hakimu, wakili n.k) kwa zaidi ya miaka 10 mfululizo na kuendelea.



3. Kuwafukuza kazi: Ni rahisi kumtimua kazi hakimu lakini kwa jaji hali ni tofauti hata kwa raisi mwenyewe. Maana inabidi raisi aunde tume ya majaji toka jumuiya ya madola ndio watoe mapendekezo juu ya makosa yake.
Nashukuru kwa elimu hii

Sent from my TECNO PR651H using JamiiForums mobile app
 
Nijuavyo mimi,

Jaji "Judge" ni kwa lugha ya Kiingereza,ni sawa na tunavyosema Shati "Shirt" Hakimu ni neno la kiarabu "Hakam" mtu anayehukumu.
Jaji (judge), hakimu (magistrate).
Tofauti yao ni mahakama wanazohudumu, jaji akiwa mahakama za juu iwe ni ya mkoa, Kuu au ya rufani. Hakimu ni kwa mahakama za chini, mfano ya mwanzo, ya wilaya.
 
Jaji ni mwamuzi wa kesi katika mahakama kuu. Cheo chake ni cha kuteulowa na raisi na anasimamia sheria za uamuzi zinazotumika katika mahakama kuu.

Hakimu ni mwamuzi wa masuala na kesi zinazowasilishwa katika mahakama ya mwanzo, wilaya na ya hakimu mkazi mkoa. Mamlaka yao huyapata kwa kuomba kazi na kuajiriwa na kama watumishi wengine wa serikali. Kwa ngazi ya kimamlaka suala likishidikana mahakama za chini zinazosimamiwa na mahakimu basi anayeona hajaridhishwa na huo uamuzi wao atakata rufaa kwenda kwa jaji.

Kuna masuala hutakiwa kuanzia kwa mahakimu na pia kuna masuala ni lazma yaanzie kwa jaji(mahakama kuu).
Mahakama ya Rufani je??
 
Prosecutor
Counsel
Plantiff

Hawa ni kazi zao ni zipi
 
Prosecutor
Counsel
Plantiff

Hawa ni kazi zao ni zipi
Prosecutor ni mwendesha mashitaka, mfano Serikali inapomshitaki mtu/ taasisi.

Counsel/lawyer/ attorney ni mwanasheria anayemtetea mtuhumiwa katika kesi.

Plaintiff ni upande unaoshitaki hasa kesi kati ya mtu/ taasisi dhidi ya mtu/taasisi.

Defendant ni upande unaoshitakiwa hasa kesi kati ya mtu/taasisi dhidi ya mtu/taasisi.
 
Jaji (judge), hakimu (magistrate).
Tofauti yao ni mahakama wanazohudumu, jaji akiwa mahakama za juu iwe ni ya mkoa, Kuu au ya rufani. Hakimu ni kwa mahakama za chini, mfano ya mwanzo, ya wilaya.
Kwa hiyo mahakama kuu hazina mahakimu?
 
Jaji Mfawidhi
Mahakama ya Rufani na Mahakama Kuu
Husikiliza rufani zote toka Mahakama za chini ya Mwanzo na Wilaya
Ana mamlaka ya kutengua hukumu ya Mahakama,a Chini

Hakimu Mkazi
Mahakama ya Mwanzo na Wilaya
Hawezi sikiliza kesi za Mahakama Kuu km rufani
Hutoa rufani kwenda Mahakama Kuu au Mahakama ya Rufani
Hana mamlaka ya kutengua hukumu ya Mahakama ya juu
 
Back
Top Bottom