Nini tofauti kati ya uchochezi na ukweli

Aman Ng'oma

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2011
Posts
961
Reaction score
533
Ni maneno mawili yanayochanganya sana,ikitokea mtu anasema ukweli anaambiwa ni mchochezi/anakashifu.Mfano Gazeti la Mwanahalisi.mpaka likafungiwa kwa kile kinachodaiwa uchochezi.Kwa hiyo serikali au mtu akikosea asiambiwe ukweli kwa kuwa ukweli unageuzwa kuwa uchochochezi?Waislamu siku zote wamekuwa wakiiambia serikali ukweli,wanakuja na tuhuma kuwa hawa watu ni wachochezi.Nataka anayejua aelezi nini tofauti ya ukweli na uchochezi.

Najua ukweli siku zote unauma,na watawala siku zote hawataki kuambiwa ukweli.Lakini tukae tukijua ukweli pekee ndio humuweka mtu huru.Tukiambiana ukweli uovu na ufisadi hautakuwepo,watu wataheshimiana na amani itatamalaki nchini kwetu.

Tukiendelea kuwashutumu wanaotuambia ukweli hatutafika.Dawa kujirekebisha.

Naipenda nchi yangu Tanzania.
 
Kuna wachochezi walisema Kanisa limeingia MOU na serikali wakati ukweli ni kwamba Kanisa liliingia MOU na Ujerumani.
 
Kuna wengine ni wachochezi ingawa wafuasi wao wanawaona ni mashujaaa mfano;
ilunga, ponda n co.
 
Kuna wachochezi walisema Kanisa limeingia MOU na serikali wakati ukweli ni kwamba Kanisa liliingia MOU na Ujerumani.

Acha kupotosha.kanisa limeingia mou na serikali na viongozi wa kanisa walikiri hilo ktk tamko lao la siku ya mkesha wa krismas.au hufuatilii vyombo vya habari?
 
Ilunga na ponda hawakurupuki ktk kile wanachoongea.wanaushahidi wa kutosha ktk hoja zao.wanaposema mfumo kristo hukuuona pale pinda alipo watoa ndani mapadri baada ya wenzao kumwambia hawapo tayari kuongea nae mpaka wenzao watoke jela?vipi kwa upande wa mashekh mbona na wao walipowataka viongozi wao kuachiwa mbona pinda alikataa?we unafikiri waiskam wanamuelewaje?we dont intertain double standard during treating people who have the same crime.
 
nimpongeze aliyeleta hii , kwa mtazamo wangu uchochezi ni kitendo cha kuhamasisha kufanyika kwa jambo lolote ambalo si halali kisheria na kwa kutumia njia ambazo si halali kisheria. hili linaweza kufanyika kwa kusema kupitia vyombo vya habari au kwa njia za kiharakati za chini chini ambazo kinachofuatia ni matokeo ya uchochezi .UKWELI ni jumla ya mabo yote ambayo hayapingiki kwa kutumia mazingira ya jambo husika au ni tofauti ya mambo yasiyo na uhusaino na yanayohusiana aidha kidhaanifu au kiyakinifu
 
Kuna wengine ni wachochezi ingawa wafuasi wao wanawaona ni mashujaaa mfano;
ilunga, ponda n co.

Haya ndio maneno mtoa mada anayaongelea.
Unapo muita mtu mchochezi ili kuihakiki kauli yako huna budi kutoa na mifano hai!

Kusema tu kwa ufupi. Kuwa fulani na fulani ni wachochezi ,
si tu kuna potoa jamii. Bali ni namna ya uchokozi. !

Sababu wale wenye kuwaheshimu na kuwafuata viongozi uliowataja hapo.

Wanaweza kukutolea maneno yasio na maana.

Na ndio vyanzo vya vurugu nchini!

Na mimi pia naipenda nchi yangu Tanzania.!
 
Kama hivyo basi mjerumani kaingia mkatabb na zanzibar wa kukodisha ardhi ya coastal area of mainland kwa miaka 99 je nalo bado linazingatiwa?
Kuna wachochezi walisema Kanisa limeingia MOU na serikali wakati ukweli ni kwamba Kanisa liliingia MOU na Ujerumani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…