The only
JF-Expert Member
- May 19, 2011
- 10,805
- 14,181
Ndondondo si churururu ! Ndivyo ilikuwa nianza kwa kupenda michango yake iliyopevuka iliyosheheni mapenzi ya kweli na nia ya utulivu uso kifani,Taratibu dozi ikaanza kuniingia lahaula la kwata nikajaa nikawa bingwa wa kufuatilia post zake kuliko hata navyofuatilia za mshana jr ,deo msando na gudume .
Najileta kwenu waungwana mninusuru kwani nishaona dalili kuwa mzigua90 ataninyanyasa sana kwani mtizamo wake juu ya mahusiano ni hasi na ni dhahiri ni mtu mtemi asieshaurika, na ukiweka na kauzigua (Tanga ndo yalikozaliwa) mimi mnyalu wa watu najiona nikiuza kiwanja cha urithi.
Nafwaa wajameni.
Najileta kwenu waungwana mninusuru kwani nishaona dalili kuwa mzigua90 ataninyanyasa sana kwani mtizamo wake juu ya mahusiano ni hasi na ni dhahiri ni mtu mtemi asieshaurika, na ukiweka na kauzigua (Tanga ndo yalikozaliwa) mimi mnyalu wa watu najiona nikiuza kiwanja cha urithi.
Nafwaa wajameni.