Nionavyo, Wizara ya Mambo ya Ndani inahitaji Mtu Mkali sana

zandrano

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2017
Posts
7,893
Reaction score
8,816
Kwa jinsi ilivyo wizara ya mambo ya ndani kuwa na hekaheka za matukio ya kihalifi nadhani wizara ya mambo ya ndani ilipaswa iwe na mtu mkali. Ukali wenye maana na kwenye mambo ya msingi.

Kimsingi kila Waziri kwenye eneo lake anapaswa kuwa mkali kwenye mambo ya msingi vinginevyo mambo hayawezi enda. Baadhi ya watu hawawezi enda au kufanya bila mjeledi.

Viongozi wetu hawana budi kuwa wakali. mfano; hata majumbani mwetu baba na mama wasipo kuwa wakali lazima watoto wataharibikiwa.

Naomba viongozi tuache upole sana. Wizara ya Ardhi imepooowa kama hakuna waziri, wizara ya Afya imepowa kama haina waziri. Wananchi wanataka viongozi mchape kazi na kukemee mambo yasiyo faa.
 
Tatizo ni kwamba, hata huyo Waziri atakayepewa hio Wizara nae ni product ya wizi wa kura wa CCM kwa kusaidiwa na Hao Watu wa Wizara ya Mambo ya Ndani, ndio maana tunasema tupate VIONGOZI ambao sio product ya wizi wa kura.
 
No gentleman, uongozi unahitaji uthubutu, weledi, hekima na busara tu na si vinginevyo 🐒
 
Naomba viongozi tuache upole sana. Wizara ya Ardhi imepooowa kama hakuna waziri, wizara ya Afya imepowa kama haina waziri. Wananchi wanataka viongozi mchape kazi na kukemee mambo yasiyo faa.
Inahitaji akili zaidi kuliko kitu kingine chochote.
 
Tatizo ni mfumo mbovu wa CCM hili genge liondoke kwanza.
 
Wizara haihitaji "mtu mkali sana". Wizara inahitaji "mtu professional and effective".
 
Kama ukali tu alikuwapo Augustine Lyatonga Mrema kashawapa sana watu siku saba, kiko wapi sasa?

Tuna tatizo sana la kutaka kuendesha nchi kwa personalities badala ya policies.
 
Ukali utasaidia Nini wakati Kuna magenge yameshapewa go ahead kufanya yanavyotaka na system
 
Wizara ya mambo ya ndani aliiweza kangi lugola.Alipambana na polisi watekaji na Wala rushwa hadharani. Hii wizara inatakiwa iongozwe na mtu ambaye amepotia ujeshijeshi ili kuwanyoosha Hawa makamanda wa polisi Kwa matendo Yao maovu.
 
Kangi Lugola ndie pia alitoa tafsiri ya kosa la ubovu wa gari ni moja sio mara kosa la taa atakuja ataandika kioo apatikane mtu kama yule sio hao wengine ni drama za kutosha.
 
Kama ukali tu alikuwapo Augustine Lyatonga Mrema kashawapa sana watu siku saba, kiko wapi sasa?

Tuna tatizo sana la kutaka kuendesha nchi kwa personalities badala ya policies.
Sure
 
Na aliyewekwa sasa hivi alishasema haiitaji kufoka foka ukiwa na umri kuanzia miaka 40 ili uonekane wewe ni mkali , watu wazima wanahitaji mtu anayeelekeza bila temper na watamwelewa zaidi kuwa yuko serious kuliko anayefoka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…